Ijumaa, 3 Septemba 2021

MAJI YA MACHO


Unapozungumzia maji ya macho hapo nazungumzia maji yanayotirirka kutoka machoni yanayozungumza kwa lugha ambayo, kwa yule yanayomtoka uwa anaielewa!

Na maji haya yanaweza kutoka kwa mtu baada ya kufurahishwa au kuumizwa na kitu au hali fulani katika maisha yake.

Ni kama machozi ya samaki yasivyoweza kuonekana maana yanaishia majini, na uwa samaki maji ya macho yake yanatoka pale  aliyoyategemea na kutarajia kuwa tofauti na matarajio yake japo wewe unaweza usielewe ila yeye na walio katika ulimwengu wake wanaelewa vizuri.

Ni sawasawa na ndege au wanyama mathalani kuku au mamba na hata kondoo pamoja na mbuzi uwa wana lugha zao kuelezea hali zao kufurahishwa na kuhuzunishwa kwao, wako wanaotoa lugha ya machozi na wengine mingurumo na miemko katika muonekano wao.

Naam ni kama mtu aliyetegemea nguzo katika kujistili kama egemeo lake katika siku za maisha yake lakini pindi anapoona wageni mchwa wakiweka makazi ndani ya nguzo yake ya mbao aliyoipenda na kuitegemea basi hapo moyo wake uweza kuinama na kuruhusu maji adimu yatoke machoni.

Watu wengi ulia pindi wanapoona mchana unaondoka na usiku unakuja maana huo ni wakati ambao hataweza fanya yale anayoyataka maana ni giza tu litakuwa linatawala mboni ya jicho lake alitaweza kuimiri.

Kilio kikubwa katika familia ni pale anapoona anaumwa/wameondokewa na tegemeo au nguzo katika familia japo wote  ni sawa lakini kila mtu ana nafasi yake katika familia na hapo ndipo panapoonyesha umuhimu wake.

Mathalani mwanamke aliyefiwa na mume (mjane ) mbali na kumpenda sana lakini kama alikuwa tegemezi pekee katika familia hapo uweza kulia katika kiwango cha juu sana sawa na utamaduni wa kabira lake uku akijua kuwa ni kama ndege imepoteza mwelekeo angani na rubani ajui afanyi nini ili aokoe maisha ya watu ( abiria ).

Ndo maana hata nyumba ikipata itilafu yoyote kabla ya kukarabati wataalamu uwa wanaangalia namna ya nguzo zilivyoathirika je! Zinaweza kuimiri au zibadilishwe ili kufanya jengo kuwa imara.

NINAPO IANGALIA KESHO UWA MAJI YA MACHO YANATOKA!

Karibu!

Kuna vitu katika mwili wa mwanadamu vinafanyika kwa hiari yako au nje ya hiari yako,

Kuna vitu vingine mwilini unafanya kutegemea nguvu ya vionjo vyake, mathalani kuna baadhi ya maneno ukiambiwa tu unaweza jikuta umekaa chini hata bila kujua umekaaje hapo chini na inaweza kuwa ni habari ya kuuzunisha au kukufurahisha.

Tumekuwa tukijua kuwa nguvu inapotikisika hapo jengo kuanguka ni jambo linategemewa kutokea tu.

Moja ya kitu kinachoweza kumfanya mtu asitishe kufanya jambo ni pale anapoona kesho haiwezi kuwa ni sawa na picha iliyomo katika kichwa chake hama sawa na ndoto yake.

Na kuna mtu anafanya kitu uku akijua baada ya miaka kadhaa hata weza fanya tena na hana njia nyingine na hata kuwa njia nyingine hawezi  kuandaa kesho itakayo mpa kicheko uwa anafanya tu na jioni ikifika maji adimu machoni pake ndo yana kuwa usingizi wake.

Unaweza kukuta mtu anachukua maamuzi ya kujinyonga au akazidi kuwa chini pindi pale anapogundua kesho yake imejaa giza.

Ni muhimu utambue maadam kwakuwa ulikuwa na mwanzo basi una mwisho, hivyo unavyo ona giza katika jambo fulani jua hivyo ni ishara ya asili yako kwakuwa kutakuwa na mambo tu utakosa majibu hata kama unakitu gani maadam unaishi hapa duniani?

Maadam kuna mahali akili zako zilipata uelewa fulani jua mwisho wa uelewa hapo ndipo mpaka uweza wa akili yako kuona majibu katika maswali/ kuona dhahabu katika mawe mengi.

Unamuhitaji Mungu mwenyewe kuijua kesho kwakuwa kesho yeye anaijua anaimudu, ishi maisha uku ukijua unahita neema yake.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………….………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni