Ijumaa, 25 Februari 2022

NGUVU YA PENZI



Katika dunia kuna vitu vinasemekana kuwa na nguvu mathalani maji,upepo na hata matetemeko ya ardhi hata vinaweza kuzamisha au kuondoa vitu kama sio kudondosha fahari ya dunia: mathalani majengo makubwa na hata milima mikubwa lakini haijafikia nguvu iliyojificha ndani ya PENZI!

Niseme tu, mahali penye penzi ni mahali ambapo ni makimbilio ya kila kitu: wanyama, binadam na hata viumbe vingine.

Mahali penye penzi unaweza usione ajabu chizi,mgonjwa aliyepalalaizi au kuvunjika akapona na kuwa msaada kwa wengine.

Ndomana hata wanyama wakihisi mahala hapa pana upendo hawatapenda kuondoka mahali hapo miguuni pa mwenye upendo.

Ni kubaliane kuwa upendo sio kucheka,kuongea wala kula pamoja tu bali pia kunauhusisha kukubali na kuingia gharama kwa ajili ya kuhakikisha furaha ya mtu haipotei wala aipungui bali inaongezeka siku baada ya siku.

Ni kweli mahali penye kutimiza uhitaji wa watu/viumbe, viumbe au watu uweza kuja ili kukizi uhitaji wao mathalani nzi upenda kutoa kwenye kidonda lakini awezi kuweka makazi hapo lakini mahali penye upendo hata mtu akishapata uhitaji uweza kuyaamisha maisha yake na kuweka kituo mahali penye upendo.

Ni pende kusema hitaji kubwa la binadamu ni PENZI na wala sio kitu chochote kinachoonekana kuwa kina kifaa hama kuvutia.

Mtu mwenye akili uweza kukataa pesa na kulipokea penzi litokalo katika moyo wa mtu aliyobeba dhamira njema japo kuwa anaweza kuwa na matakwa mengi lakini tulizo la moyo wake lazima lianzie katika penzi la dhati.

Ukweli unaweza kuwa na vitu vingi lakini vikapukutika lakini sio PENZI mahala penye penzi hilo lenyewe alijali pesa au kitu kipo au akipo lenyewe lipo tu,

Karibu!

PENZI KAMA CHOMBO CHA MAREKEBISHO SALAMA,

Kama kuna kitengo kigumu basi ni hiki kitengo cha marekebisho!

Siko tofauti na kutumia adhabu kali ilete mabadiriko au marekebisho kwa mtu hususa tabia yatokee.

Lakini iko njia rahisi na yenye uhakika inaitwa NGUVU YA PENZI:

Katika njia hii hakuna kitu kikashindwa kurekebishwa haijalishi itachukua muda gani lakini hipo siku mabadiriko yatadhihirika siku moja.

Na ukitumia njia hii vizuri uwezi kushindwa kupata matunda uliyo yakusudia hasa yaliyo mema.

Unapoonyesha penzi katika tatizo la mtu unavumbua thamani yake na kuonyesha namna ya kuitunza ili thamani isipotee.

Mahali penye pendo la kweli hata tabia ikiwa ngumu kiasi gani mahali penye upendo endelevu mabadiriko yatatokea.

Nguvu ya penzi inayo uweza kumuonyesha mtu majukumu yake na kuyatekeleza kwa uaminifu hata bila ya usimamizi bali nguvu inampa kujisimamia.

Na penzi linapozidi linamfanya mtu azidi kujibidisha pasipo kuangalia vikwazo vyovyote bali anapoona mahali penye mashaka na yeye uaminifu uweza kupungua na bidii upotea kabisa hatimaye kushindwa kuendelea mbele.

Mahusiano yanatunzwa na nguvu ya penzi na sio uchumba wala ndoa bali vyote ubebwa na mwamvuli wa penzi maana anapopungukiwa mtu au kukosa inakuwa sio yeye amekosa bali unajiona wewe ndio umekosa kwakuwa unajiona wewe katika maisha yake.( unavaa viatu vyake ).

Unapoongea na mtu katika penzi uwa mtu anaona deni/na kujipa wajibu ili kujibu penzi analoliona katika sura yako ya kidhihirishwa kwa maneno yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………………….0764 018535

Ijumaa, 11 Februari 2022

MUNGU ASIPOTOA DUNIA ITATOA?

 



Uhitaji moja ya ishara ya kuwa kiumbe hai, japo kunatofauti ya uhitaji lakini hali ni ileile tu, UHITAJI.

Naam ili kupata kitu lazima mchakato upitie katika usaidizi wa Mungu au Dunia kufanikisha jambo unalolihitaji.

Hivyo ili upate kitu ni lazima dunia ikupe au Mungu akupe.

Luka 4:3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.

 4 Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu.

 5 Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.

 6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.

 7 Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.

 8 Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.

 

Japo dunia au mbingu imepanga kukupa lakini kila utawala unapokupa kitu chake unakuwa una matakwa yake ni muhimu utambue matakwa ya kila utawala kabla ujaingia mahali ambapo utajuta kwa nini upo hapo!

 

Ili mradi tu unahitaji basi jua dunia na mbingu ziko mbele yako zikisubiria maamuzi yako.

 

Kumbukumbu la Torati 30:15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;

 

Maamuzi yako ndio ukombozi wako! Basi utaamua nini ndivyo itaamua hatma yako na sio unavyotaka.

 

Kila kitu alichonacho au alichonacho mtu kina pande mbili Mungu ametoa au dunia imetoa, na tunapozungumzia dunia sio lazima utumie nguvu za giza bali yenyewe kutokana na kanuni zake iliyo asili yake.

Mathalani ibrahimu, Ishmael mwanae ambaye dunia ilitoa na isaka naye ni mwanae lakini Mungu ndiye alitoa………………..japo wote ni watoto lakini ni mfumo miwili tofauti!

Hivyo sio kuwa na kitu tu bali iko kitu umepokea kutoka katika mikono ya dunia au mbingu hilo lina maana sana hasa katika ustawi na mstakabali wako.

Na umuhimu utambue kila kitu kitoe au kikupe kina utaratibu wake kinategemea sana akili yako na namna yako ili kukufuata.

Usipokuwa mwangalifu dunia inaweza kukupa ukafikiri Mungu amekupa ukamshukuru yule asiyestahili na aliyekupa akigundua anaweza kukichukua.

Siri kubwa ya kukipata kitu chochote ni umakini wa kusikiliza, kitu gani umekipa uzito wa ndani wa kumsikiliza hivyo ukamsikiliza vizuri Mungu basi utavipata vyake hivyohivyo ukiisikiliza vizuri dunia na kuifuata basi utavipata vile vilivyo vyake.

Na muhimu utambue dunia inapotoa uwa inalenga kwa faida yake hata kama baadae utapata maumivu, dunia yenyewe haijali ili mradi imetimiza lengo lake lakini Mungu anapotoa inakuwa kwa ajili ya ustawi wako wa leo, kesho na milele mathalani na mzazi mwenye akili njema anapokubali kunyima ili mwanae asome.

Ni muhimu iwe dhahiri pindi Mungu anapofanya basi iwe ni kweli Mungu amefanya na dunia inapofanya basi ijulikane tu ili ushuhuda wako uweze kudumu.

Ikumbukwe unaweza kuwadanganya wote lakini sio nafsi yako wala Mungu/dunia mathalani mtu anapotafuta muujiza dunia inaweza fanya maajabu yake na Mungu anaweza fanya muujiza hivyo sio kila muujiza chanzo chake ni Mungu.

Ili uweze kuvipata vitu vya Mungu lazima ukubali kutulia na kukubaliana na dhoruba na vitisho vya dunia maana dunia upenda kukuonyesha jinsi gani uwezi kutoka ulipo bila kumsikiliza au kufuata njia zake.

Kwa harakaharaka dunia inatoa vitu vyake haraka na kwa muonekano mwepesi “ easy come easy go” na kukunawirisha kwa kitambo baadae ukuacha kwa kuwa ilishatimiza haja yake.

Lakini Mungu “ Alfa na Omega” akianza na wewe hauwezi kukuacha labda wewe ndio umuache lakini ujue ukimwacha ni kwa hasara yako.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey  Nelson…………………………………………………………0764 018535