Uhitaji moja ya ishara
ya kuwa kiumbe hai, japo kunatofauti ya uhitaji lakini hali ni ileile tu, UHITAJI.
Naam ili kupata kitu
lazima mchakato upitie katika usaidizi wa Mungu au Dunia kufanikisha jambo
unalolihitaji.
Hivyo ili upate kitu ni
lazima dunia ikupe au Mungu akupe.
Luka 4:3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa
ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.
4 Yesu
akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu.
5
Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.
6 Ibilisi
akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi
mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.
7 Basi, wewe
ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.
8 Yesu
akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke
yake.
Japo
dunia au mbingu imepanga kukupa lakini kila utawala unapokupa kitu chake
unakuwa una matakwa yake ni muhimu utambue matakwa ya kila utawala kabla
ujaingia mahali ambapo utajuta kwa nini upo hapo!
Ili mradi
tu unahitaji basi jua dunia na mbingu ziko mbele yako zikisubiria maamuzi yako.
Kumbukumbu
la Torati 30:15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na
mauti na mabaya;
Maamuzi
yako ndio ukombozi wako! Basi utaamua nini ndivyo itaamua hatma yako na sio
unavyotaka.
Kila
kitu alichonacho au alichonacho mtu kina pande mbili Mungu ametoa au dunia
imetoa, na tunapozungumzia dunia sio lazima utumie nguvu za giza bali yenyewe
kutokana na kanuni zake iliyo asili yake.
Mathalani
ibrahimu, Ishmael mwanae ambaye dunia ilitoa na isaka naye ni mwanae lakini
Mungu ndiye alitoa………………..japo wote ni watoto lakini ni mfumo miwili tofauti!
Hivyo
sio kuwa na kitu tu bali iko kitu umepokea kutoka katika mikono ya dunia au
mbingu hilo lina maana sana hasa katika ustawi na mstakabali wako.
Na
umuhimu utambue kila kitu kitoe au kikupe kina utaratibu wake kinategemea sana
akili yako na namna yako ili kukufuata.
Usipokuwa
mwangalifu dunia inaweza kukupa ukafikiri Mungu amekupa ukamshukuru yule
asiyestahili na aliyekupa akigundua anaweza kukichukua.
Siri
kubwa ya kukipata kitu chochote ni umakini wa kusikiliza, kitu gani umekipa
uzito wa ndani wa kumsikiliza hivyo ukamsikiliza vizuri Mungu basi utavipata
vyake hivyohivyo ukiisikiliza vizuri dunia na kuifuata basi utavipata vile
vilivyo vyake.
Na
muhimu utambue dunia inapotoa uwa inalenga kwa faida yake hata kama baadae
utapata maumivu, dunia yenyewe haijali ili mradi imetimiza lengo lake lakini
Mungu anapotoa inakuwa kwa ajili ya ustawi wako wa leo, kesho na milele
mathalani na mzazi mwenye akili njema anapokubali kunyima ili mwanae asome.
Ni
muhimu iwe dhahiri pindi Mungu anapofanya basi iwe ni kweli Mungu amefanya na
dunia inapofanya basi ijulikane tu ili ushuhuda wako uweze kudumu.
Ikumbukwe
unaweza kuwadanganya wote lakini sio nafsi yako wala Mungu/dunia mathalani mtu
anapotafuta muujiza dunia inaweza fanya maajabu yake na Mungu anaweza fanya
muujiza hivyo sio kila muujiza chanzo chake ni Mungu.
Ili
uweze kuvipata vitu vya Mungu lazima ukubali kutulia na kukubaliana na dhoruba
na vitisho vya dunia maana dunia upenda kukuonyesha jinsi gani uwezi kutoka
ulipo bila kumsikiliza au kufuata njia zake.
Kwa
harakaharaka dunia inatoa vitu vyake haraka na kwa muonekano mwepesi “ easy
come easy go” na kukunawirisha kwa kitambo baadae ukuacha kwa kuwa ilishatimiza
haja yake.
Lakini
Mungu “ Alfa na Omega” akianza na wewe hauwezi kukuacha labda wewe ndio umuache
lakini ujue ukimwacha ni kwa hasara yako.
INAITWA
SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa
na:
Cothey Nelson…………………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni