Alhamisi, 2 Oktoba 2014

ZAWADI ILIYOJIFICHA



ZAWADI ILIYOJIFICHA;


Hakuna mtu ambaye apendi kupewa zawadi na mtu anayempenda, kwakua wakati mwingine utumika kama mwendelezo mwema wa mausiano. Lakini inakuwa tatizo pale tu usipoielewa au kutoiona, wakati mwingi haina ya zawadi itakuwa inaashiria mustakabali wa mausiano yenu.

Kwa Yule aliyekupa zawadi kwa dhamiri iliyo njema uona fahari sana kama utaitumia vizuri kwakua ana amini hiyo zawadi itakusaidia kwakua mpaka amekupa anaamini ni njema na inakufaha, tatizo inakuja pale tu ile zawadi usipoijua ni ya kwako na matumizi yake yaliyo sahihi.

Ni jambo la kawaida sana endapo usipoielewa namna ya kuitumia haita fanyika Baraka bali itakuwa ni mzigo badala ya kuwa burudiko ambayo ndio hasa kusudi la zawadi.

Kila mwanadamu ndani yake kapewa zawadi na Mungu ili imsaidie katika maisha yake duniani iwe Baraka kwake na kwa wale watakao mzunguka. Kwakua chochote ambacho Mungu anakupa wewe ni kwa ajili ya kufaidiana ili muishi kama familia moja yenye upendo na mshirikiano wa kweli.

Huwezi ukaitambua zawadi aliyokupa Mungu halafu ukawa namna ambayo Mungu ajaikudia iwe katika maisha yako, lakini wanadamu wengi wanapata tabu sana ni kwa vile hawajajua hadhina iliyo ndani yao na namna ya kuitumia.

Ukiona mtumishi wa Mungu kafanikiwa kihuduma sana katika kuimarisha roho zatu kujenga misingi imara ya kumpenda Mungu isiyotingishwa ujue amitambua zawadi/hadhina ambayo Mungu amempa na kuitendea kazi katika hali stahiki.

Ni wazi kuwa hauwezi kufika tu kwa njia nyingine ila ni kwa kuitambua zawadi ambayo Mungu amekupa na kuifungua na kuanza kuitumia.

Baadhi ya vikwazo vya watu kutoitumia zawadi aliyowapa Mungu!

Ni wazi tu usipotambua wapi umeanguka uwezi kusimama katika hali stahiki isiyotoa taswira ya kuanguka tena. Kujua tatizo ndio hatua ya kwanza ya kuondoka mahali ulipo pasipo kijua basi utakuwa unazunguka hapohapo siku zote pasipo mafanikio ya kutoka mahali ulipo.


i.watu hawajipendi

watu wanapenda wafanane na mtu mwingine na sio watu wao wafanane na yeye japo yote yanawezekana watu wakaitambua nafasi yako na hata kujifunza kupitia wewe.

Watu wamekuwa hawishi maisha yao bali upenda kuishi maisha yaw engine ambao hawajui chimbuko lao wapi limetoka na ustahimilivu wake umejengwa na nini nay eye kufika pale ili mgharimu nini na nani aliyekuwa karibu yake.

Hauwezi ukawe wewe kama tu mfumo wa maisha umebeba ramani ya watu wengine mwelekeo wako umebebwa na maisha ya watu wengi.


ii.mafanikio yasiyo ambatana na usahihi wake
kufanikiwa sio tatizo bali unafanikiwaje na katika misingi hipi ilichimbuko ndani ya moyo wako au ilichumbuko kutoka kwa watu wengine.

Mafanikio haya kulupukiwi bali ni mikakati na maongozi sahih neon lake Mungu. Na katika mafanikio utakiwi uchoke au uone kuwa haustahili kwa mapungufu yeyote yaliyo ndani yako.

Usione kitu kizuri basi ukawaka tama na ndipo ukaanza mikakati ya kupata yale uliyoyaona ka kutumia utundu wa akili tu bali lazima ujue vitu vya muhimu ni vipi! Na nawezaje kuvipata! Na je! Kwa wakati gani ni sahihi wa mimi kuvipata.


Imeandaliwa na ;
                           Cothey Nelson, 0764018535, cotheyn@yahoo.com


NIKUTAKIE KILA LA KHERI NDUGU!!!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni