Jumanne, 31 Machi 2015

UPOFU WA AKILI



UPOFU WA AKILI



Tunakubaliana sote kwa pamoja kuwa tofauti kubwa ya mwanadamu na mwanadamu na tofauti ya tofauti ya mwanadamu na wanyama sio Akili tu bali matumizi ya AKILI, hivyo hapa kuna vitu viwili kuwa na akili na matumizi ya akili na pia katika matumizi ya akili kuna matumizi sahihi na matumizi yasiyosahihi….matumizi ya akili yanazalisha majina kama haya mjanja,mjinga,mzembe,mvivu,goigoi,mwelevu na hata kuitwa usiyejitambua.

Naamini katika maneno makali ambayo binadamu apendwi kuambiwa ni neno kuwa HUNA AKILI hii ni lugha yenye ukali yanayoathiri mfumo mzima wa maisha ya mtu katika mwenendo wake mzima.japo wako watu wanakataa kuambiwa kuwa wanamatumizi mabaya ya akili zao au kwa lugha rahisi anaitwa mjinga ambalo ni neno lilojaa mauzi kebei na kwa hakika alivutii katika masikioni mwa mtu.

Ninapozungumzia upofu wa akili sina maana kuwa akili iliyokosa mwelekeo au akili iliyokosa njia sahihi yanamna kutatua majukumu yanayo mzunguka,…………..bali hali ya kujua uaribifu wa maisha yako na kwenda katika njia hiyo pasipo kujali kitakachotokea, mtu wa namna hii ataashauriwe na mtu wa namna gani? Bali ushikilia kile alichokiamua/alichokiamini mathalani kuwa katika maamuzi ya kuchukua kuingia katika UJAMBAZI,UCHAWI na hata UKAHABA, mtu wa namna hii sio kitu rahisi kumtoa mtu katika maazimio yake hayo labda mpaka aone madhara yake na anaweza kuona anahitaji msaada na asiupate huo msaada kwani jamii inawakata au inawanyanyapaa na hata kuwatenga kuishi na watu hawa katika hali ya kujiami.

Sikatai wako watu wanajiingiza katika mfumo huo usio rasmi wakiwa na mawazo tofauti wako watu watasema mimi nitafanya kwa muda tu alafu nitaacha na pindi atakapoacha anaamini atakuwa anaweza kujishughulisha katika shughuli nyingine ambayo itampatia kipato katika kuendesha maisha yake….lakini katika mawazo hayo ni wachache sana wanao uwezo kuyatimiza hayo mawzo…zaidi sana wanachokiongea sio kile wanachokifanya inawezekana katika ushawishi binafsi au ushawishi wa wenzao.

Naamini kama akili yako ikiwa njema haiwezekani tu ukaingia katika mfumo huo ambao utahatarisha maisha yako na niseme wazi maamuzi ya jinsi hii aichagui MSOMI au ASIYESOMA  au MASIKINI au TAJIRI wote akili zao zinaweza patwa na upofu wakafanya mambo ambayo yakaongeza giza katika maisha yao badala ya kuongeza nuru….ni wazi kuwa kazi hii hauwezi fanya milele ila sio rahisi kutimiza lile lengo ambalo umelipanga kuwa nitatimiza.

Watu wanaofanya shughuli hizi wengi wanasema wafanya hili sio kwa kupenda bali kunashinikizo ambalo linamsukumo katika kuyafikia maamuzi hayo inawezakuwa maisha, msuko wa mwili wake na hata  katika mtazamo wake au ushawishi watu……….tunaamini kunashughuli nzito kamaukiingia sio rahisi sana kutoka huko mathalani mtumiaji madawa ya kulevya na msambazaji wa madawa ya kulevya anaweza asitoke kutokana na manufaa anayo yapata au kutokana na kuathirika katika mwili wake.

Japo ziko taasisi zilizoazishwa katika kuwasaidia jamii kuondoka na tatizo hili lakini tatizo limekuwa likupungua tu lakini ukweli tatizo limeendelea kuwepo wakati wote na jamii imekuwa ikizidi kuathirika na janga hili pasipo kujua nini cha kufanya.

 Ushauri wangu kwa watu wa jinsi hii……kwanza nitoe shukrani zangu kwa kila taasisi ambazo kiukweli zimejitolea kuhakikisha jamii inaondokana na janga hili na kuwa jamii isiyo na watu wenye akili zilizotiwa giza ambazo kwa muonekano zimekosa njia sahihi, zimekosa mwelekeo na hata kukosa kuthamini kesho yao………lakini kubwa katika yote Mungu anaweza kuyafanya yale ambayo kwa uhalisi yalikuwa ni magumu sana kama mzazi au mlezi na hata ndugu mwamini yesu katika maisha yako awe dira katika maisha yako yote na yeye ataleta nuru kwa wale waliofikia hatima mbaya ambayo jamii haiwaelewi tena……na kwa mtu aliyeathirika katika utendaji niseme sana wewe ni mtu wa maana sana kwani katika biblia yesu aliwapenda waliokataliwa na jamii husika  mathalani wenye ukoma, makahaba na hata watoza ushuru Mungu ni zaidi ya baba anayejua kulea,kujali na kukupa kile kitu ambacho hakuna mtu anaweza kukupa mkabidhi yesu maisha yako na kuamua kwenda kanisani kwa waliokoka na kufundisha neno sahihi la Mungu!

Imeandaliwa na;
Cothey  Nelson………………………….0764 018535

Ijumaa, 13 Machi 2015

UZURI USIO HARIBIKA



UZURI USIO HARIBIKA


Uzuri ni kitu au jambo au ni hali? Yote haya ni maswali ambayo mtu anajiuliza pindi anaposikia neno hili……..wako wanazuoni na wataalamu mbalimbali wanajaribu kutoa maana ya neno hili UZURI wengine wa kimaanisha ubora au hali ya kung’aa au hali ya kustahimili au kushamiri katika yote… haya bado kuna maswali ya watu na utofauti wao katika kunyambua hili neno………na sijui wewe msomaji wangu pindi unaposikia neno hili sijui akili yako inapata picha gani? Au dhana ipi lakini yote nakuachia wewe!

 Ki kawaida hili ni neno zuri ambalo pindi unapolisikia mtu anakwambia basi moyo wako unakuwa na changamko la furaha mathalani mtu akikwambia wewe ni mzuri au umefanya jambo Fulani ukaambiwa umefanya vizuri! Ni wazi moyo wako utajawa na furaha sana….na sijajua neno hili mzuri uambiwa wanawake tu au hata wanaume na kama wanaume wanaambiwa katika muktaza upi au kwa dhana iliyo sawa na mwanamke katika muonekano ulio bora na wenye kung’aa.

Ni wazi kila mtu anapojitazama ujiona kuwa yeye ni mzuri japo naamini kuna watu wakijiangalia kwenye kioo wanaweza kusema wao ni wabaya inawezekana kwakukosa maboresho au vile anavyojiona au vile alivyoambiwa, na amini hata Yule mwenye kujiona sio mzuri sana huwa apendi kuambiwa kuwa yeye ni mbaya……..vilevile kwa mtu asiyejitambua kunakipindi anaweza kuambiwa yeye ni mzuri akakubaliana na hali hiyo kwa asilimia zote na pia kunakipindi anaweza kuambiwa kuwa yeye ni mbaya bado akakubaliana na hali hiyo kwakuamini kuwa mwanzo alikuwa mzuri na sasa amekuwa mbaya akakubaliana kuwa kuna mabadiliko.

Pia katika haya yote tukumbuke kuwa kuna uzuri wa ndani na uzuri wa nje yaani upo uzuri usio onekana na uzuri unaoonekana, lakini ningependa sana kuuzungumzia uzuri usio onekana kama ndio matokeo ya kunawirisha uzuri unaonekana, na ni wazi unapo ujali uzuri wa ndani basi uzuri wa nje utakuwa unaujali sana japo inawezekana kwa kujua hama kutokujua.

Na uzuri wa Mungu unanawilishwa na ufalme wa Mungu ukaao ndani yako katika kufanya maboresho na ushamiri wa makazi ya ki Mungu katika himaya yako ya ndani katika kutoa muungozo wa uzuri wako wa nje, kwakusema hivyo uwa si maanishi watu wa sijigharamie katika mapambo yao ya nje ila fanya yote kuustawi wa muonekano wako kuwa vyema.

Ila niseme kitu kuwa muonekano wako wa nje utegemea sana na muonekano wako wa ndani kwakua tunaona watu mambo yanapo wachanganya hata muonekano wa nje ubadilika kabisa na hali ya kutojijali uanzia hapo.

Lakini ukiutunza uzuri wako wa ndani kwa kuhakikisha maamuzi yako yote yanamleta Mungu kuzidi kujengeka katika utu wa ndani bila shaka Mungu atawezesha kuyamudu mazingira yote ya nje yasiweze kuharibu uzuri wa ndani na wanje.

Imeandaliwa na;
Cothey  Nelson……………………………………..0764 018535

Jumatatu, 9 Machi 2015

JIFUNZE KUSAHAU



JIFUNZE KUSAHAU na sio kupotezea!



KUSAHAU NI ZAIDI YA KUSAMEHE

Uwa hakuna ulazima wa kujifunza kitu ambacho sio kigumu au kinaeleweka kwa wote au kwa urahisi pasipo usaidizi wa mtu mwingine,na ni wazi pindi unapojifunza kitu uwa kinakuwa sio kigumu tena…….mathalani mtu anayejifunza kuendesha inawezekana hapo awali aliona kuwa ni kitu kigumu sana japo nae alikuwa anatamani ndani yake lakini baada ya kujifunza uweza kuona uwezekano wa kujua zaidi na mwisho uona kuwa ni kawaida sana.

Hili ni jambo ambalo watu wengi utamani kuwa nalo, japo naamini yapo ambayo binadamu yeyote ambayo apendi kuyasahau na yapo ambayo uweza kuyasahau……….lakini twende mbele na kurudi nyuma tambua kusahau kutokana na uwezo wa ubongo mtu husika sio kitu rahisi labda awe na shida katika ubongo wa mtu husika.

Ningependa kusema kuwa kusahau ni chanzo kimoja wapo katika kufanya mambo kiufanisi zaidi na uwanja mzuri katika kujenga kitu chema katika akili yako(ubongo) wako watu wanapita katika kipindi kigumu sana kwa sababu hawataki kusahau bali utaka kubaki katika kumbukumbu katika ufahamu wao na ni wazi inakuwa teso baada ya kuwa Baraka………..ninge penda ujue kwamba yako mambo ukiyakumbuka au kusahau hayaletishida katika akili yako ila yako mambo ambayo pindi unapoyakumbuka yana haribu hata utendaji wako wa kazi na kufanya kazi kuwa ngumu hata kama ilikuwa nyepesi.

Kulia kila siku hii ni ishara kubwa sana ya mtu kutotaka kusahau au kutoona umuhimu wa kusahau au kutojua kwanini nisahau, siwezi kukataa baadhi ya matendo yaliyo athiri yanaweza baki katika mwili wako na kuweka alama ambayo kila ukiyakumbuka yanarudisha nyuma kukupeleka katika lile tukio ambalo likasababisha jambo hilo litokee….na jua katika mazingira haya kusahau inakuwa ni ngumu tu kwani ukiangalia yale uliyokuwa ukiyafanya hauwezi kuyafanya tena mathalani ulemavu.

Wako waliofanikiwa katika maisha yao kwa kukubali kusahau na kujikubali na hali waliyonayo na kuanza kufanya jambo ambalo mwisho wake likawa Baraka katika maisha yao, kwa mtu huyu ana fikiria katika yale yanayomkabili kuliko yale yaliyomkabili………..najua kuna wakati unaweza kupitia jambo ambalo kwa kiasi kikubwa likachanganya akili yako kwa kiasi kikubwa sana lakini ujajua hatima yako inaweza kuwa kubwa kuliko ilo jambo linalo kukabili au lililo kukabili.

Lazima utambue ikiwa kweli unamtumikia Mungu na wala ndani yako hakuna unafiki jua mazingira ,teso shida na hata hadha sio Mungu japo yeye anaweza kuyaruhusu kufanya jambo likawa Baraka katika maisha yako kuliko vile unavyofikiria.

Imeandaliwa na;

        Cothey Nelson…………………………………………..0764 018535