Jumatatu, 20 Julai 2015

HARD DECISION IS MY LIFE



MAAMUZI MAGUMU NI MAISHA YANGU


Maamuzi magumu kwa maana nyepesi ni uchaguzi wa kujigharim!

Uwa hakuna furaha katika maamuzi magumu katika kila hatua ya awali ya mwanadamu anayoipiga ila matokeo yake yanaweza yakazalisha furaha, naamini kila binadamu anatawaliwa na maamuzi katika utendaji wake ya sasa na hata ya baadae yanabebwa na maamuzi.

Kwa sababu unaishi basi swala la maamuzi uwezi kuliepuka, yapo Maamuzi tunayo yafanya kila siku tunayaita kuwa haya ni maamuzi ya kawaida ambayo baadhi unajigharim kidogo na hata mengine haujigharim kabisa………kwa maana yako mengine unakuwa na wasiwasi sana na mengine unakuwa huna wasiwasi kabisa.

Tuna amini katika maamuzi magumu tunaweza kufanya jambo kuwa kubwa tena kwa wepesi zaidi katika muonekane wake, ni jambo la kawaida sana kwa wale walifanya mambo ambayo yamekuwa msaada sana katika maisha yetu mathalani waliotengeneza ndege,meli na mengine mengi sio ajabu wengine walitumia muda wao mkubwa katika shughuli hizo kuliko hata na familia zao,ndugu zao na pia hata marafiki zaohatimae wakafanikisha ile ndoto yao.

Niseme kuwa katika maamuzi haya magumu hapa ndipo tunaweza kufanya mambo katika mafanikio makubwa japo wako watu wanafanya maamuzi madogo huku wakitegemea kupata mafanikio makubwa…..sio kila jambo rahisi kama hivyo bali tambua kuwa kazi kubwa katika maamuzi yako ndio yanaleta matokeo makubwa.hivyo utakiwi kuogopa sana katika maamuzi magumu hasa yakiwana tija katika maisha yako na mbele za Mungu.

Ukweli hatua yako ya mbele inategemea sana maamuzi yako kwani maamuzi yenye kujigharim kidogo basi hiyo ni hatua ndogo lakini maamuzi yenye kujigharim sana basi hiyo ni hatua kubwa katika maisha yako.

Katika maisha tuliyonayo uwa hatuwezi kufika katika maamuzi yasiyo na kina mathalani serikali yetu na mambo mengine yafananayo na hilo mengi sana yamekubwa na mfumo ambao kwa kiasi kikubwa hauja beba haki au usawa bali katika kila jambo jambo walitendao limejaa udhalimu na ubadhilifu wa mali ya umma katika hili ni seme tu wazi tunahitaji mapinduzi magumu yanayobebwa na dhamira ya dhati katika kuleta mabadiliko chanya.

Tukianza na maisha binafsi hatuna budi kuhakikisha kuwa maamuzi sahihi yaliyojaa kujigharim ndio chachu nzuri ya maendeleo mathalani wako watu wanaanza na pa dogo lakini mwisho wao wanategemea kufika mbali sana lakini kama ukiangalia mwanzo wao unaweza usione mwisho wenye maana sana.

Lakini watu wengi wanaogopa kuingia katika maamuzi magumu kwani wanaona kama wataonekana wanaanza moja, na hivyo wataonekana kama wajinga hawajui wanachofanya na kuona kwamba hawata kaa wafike japo haya ni mawazo au ni maneno ya kawaida sana lakini yanaweza yakabadilisha  mfumo wa maamuzi wako badala ya kwenda kulia ukaanza kwenda kushoto.

Hivyo imekuwa ngumu sana kwa watu katika kuamua maamuzi magumu na wengi wamekuwa wakiendeleza hata kwa yale wanaona wanaelekea sio salama lakini wamekuwa wakijikaza kisabuni maadamu siku zinaenda na maisha yanadumu basi wanavumilia wakiamaini ipo siku mambo yatabadilika.

Asikudanganye mtu uwa mambo mengi hayajibadilishi bali yanabadilishwa na mtu husika au mfumo husika hivyo kusubiri maji yabadilike ni sawa kusubiri maji ya bahari chumvi ya badilike  alafu maji yawe kama ya mto…………unaweza ukasubiri sana! Lakini matokeo yake yameshatokea na kamwe haya wezi kubadika.

Unaaja kumcheka kinyonga kwa sababu ya mwendo wake bali angalia wewe unapo lala yeye anakuwa wapi lengo lake ni muhimu sana kuliko chochote uwa anajiangalia mwenyewe na kujikubali yeye kama yeye na hatimae anatimiza malengo yake.


Hakuna anayeweza kubadilisha maisha yako ila ni wewe mwenyewe!

Imeandaliwa na;

Cothey nelson…………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni