Jumanne, 7 Julai 2015

USTAWI ULIOBEBWA NA UTII



USTAWI WA KIMUNGU


Kutoka 19:5
Hakuna kitu hatari sana kama UTII kwakua ndani ya utii mtu uweza kufungua hazina yake ambayo aliiweka kwa muda mwingi……. akitafuta mtu ambaye atamwamini na kuachia mambo yote ndani yake.

Mshikamano, ushirikiano, kuimarika katika yote unabebwa na utii na ni utii pekee ndio wenye kuashiria kuwa wewe una nafasi gani kwa mtu yaani nama unavyo mtii ndiyo ishara kuwa kwake kuwa unamthamini kwa kiasi gani?

Unapaswa kujua kuwa yote unaweza kumfanyia mtu hata Mungu akaweza kukupa neema yake lakini sio kutokutii…….ni ishara kubwa sana kuwa hauko na yeye na uko mbali nae! Tunajua tatizo la watu sio kutokutii tu bali ni namna ya kutii na mambo ya kutii watu wengi wanatii katika baadhi ya mambo tu hivyo kupelekea kushindwa kuonyesha utii uliobeba moyo wote.

Niseme kuwa pasipo utii hakuna mwendo ulio wa maana wa wewe na Mungu, hata na mtu yeyote kwakua ndicho kiunganishi kikubwa katika kufanya mambo ya weze kuwa katika hali yake stahili…kwa hiyo kama hakuna utii hakuna kwenda!

Japokuwa watu wengi wanatamani sana kumtii Mungu ili wafike peponi wakiwa wana maana waweze kuwepo mahali ambapo yeye yuko yaani mahali salama mbali na jehanamu, unahitaji kujua kuwa katika mwendo huo ni vigumu sana katika mwendo wako wa kumtii Mungu katika hali ya kupenda na sio msingi utakao kuweka imara!

Kumtii Mungu hiyo ni ishara ya pekee kuwa wewe ni wake, kwani kile unacho kipenda kweli ni wazi hauwezi kukitii kinafiki kwakua kwakua unakipenda au unampenda Mungu anataka umtii kwakua unampenda na unamthamini na kuona yeye ni wa pekee katika maisha yako, kwakua Mungu anataka nafasi ya kutosha ndani ya maisha yako.

Ni seme tu hakuna maana ya kujipaka au kujiweka utakatifu kama hauna utii wa kweli mbele za Mungu, hakuna jambo litakuwa na kibali kwa Mungu endapo tu hutajua thamani ya utii mbele za Mungu.

Udhihirisho wa utii!!!

i.kifo cha matumani ya mwili
kama ibrahimu ilibidi mwili ufe ili aweze kumpata isaka na sio ishamaeli, siku zote mtu yote ana mtii Mungu uwa anapoteza matumaini ya mwili wake kuwa hapo ndipo mtu anakuwa awazi nitavaa nini? 

Nitakula nini? Nitalala wapi? Haya ni maamuzi yanafichwa na mtu ambaye aliye mbeba Mungu kweli kweli na anaye weza kufanya mambo ambayo kwa hakika watu wengi wanaomtazama hawataona maana ya yeye kufanya hivyo.

Hapa mtu anaweza Mungu tu katika staa ya maisha yake hana jambo jingine na wala haiogopi kesho bali kesho inamuogopa yeye.

Ni mtu ambaye anakwenda kinyume na mfumo ulioko katika hali ya dunia bali yeye amebebwa na uweza wa Kimungu unaompa kuona katika hali ya kimbingu na kusimama mahali pasipo simamika kwa mtu mwenye akili timamu.

ii.mateso ya akili

uwa hakuna akili itazalisha jibu katika mazingira ya mtu anayemtii Mungu alikubali kwenda na mbingu, hakika kila siku mazingira hayafanyiki tu bali katika uwepo wake hapo ndipo kunazaliwa vitu vitu vyote vinavyotakiwa kuwepo.

Wakolosai 3:10
mtu huyu hauwezi kukaa nae ukapata/ukauelewa ufahamu wake kwakua ufahamu wake umefichwa ndani ya kristo na kinachoonekana na kristo mwenyewe katika kuyafanya mambo ambayo hayawezekanai kabisa.
Nikweli hauwezi kumpendeza Mungu katika mazingira ya kuonekana ya kawaida ya kila siku na mtazamo wa akili ya kawaida………unahitai kuwa na akili nyingine!

AKILI INAYOANZISHA SIO AKILI INAYOFUATA!!!

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson………………………………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni