Jumanne, 11 Agosti 2015

NGUVU YA MTANDAO



NGUVU YA MTANDAO


 Mwanzo 11:1-6
“Bwana akasema,tazama,watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja ………………..wala sasa hawatazuiliwa neno wanalolikusudia.”

Sote tunajua pindi mtandao ukiwa vizuri basi mawasiliano yanakuwa mazuri na hata huduma zingine uweza kufanyika kwasababu mtandao umekaa vizuri! Na pindi mtandao unapokuwa chini au unaposumbua basi yako matatizo yanaweza kutokea kama ucheleweshaji wa taarifa au kutofika kabisa na pengine uweza kukosa huduma uliyokuwa unahitaka.

Ili mtando ufanye kazi lazima pawepo na mjumuhisho wa vitu vingi ili viwezeshe mtandao kuweza kutenda kazi katika ufanisi wake na pindi kifaa au kitu kimoja kinaposhindwa kufanya kazi yake basi uweza kusababisha ufanisi wa mtandao kuwa chini au kuwa duni.

Katika utendaji ulio na tija na ulio na uwezekano wa kufanya vizuri lazima wafanye kazi katika mfumo wa kimtandao au kishirikiana kitim( team work) ufanyaji kazi au utendaji wa shirika.

Ni wazi ili kufanya kazi au jambo katika ushirika wa kimtandao hatuna budi kila mtu kutambua nafasi yake na kila mtu lazima haiheshimu nafasi ya mwezake kuona kuwa naye anawajibika katika nafasi hivyo pasipo na hali ya kuzalauliana au kutoaminiana bali kila mtu awajibike akatika nafasi yake tena katika ufanisi huku akijua kwa yeye katika kuwajibika atapunguza mazigo kwa mwingine katika kuwajibika na hivyo kuwa na mchango wa uboreshaji wa kimtandao na sio kuzolotesha mtandao.

Kufanya kazi katika hali ya kimtandao kunatoa asilimia kubwa ya kushinda kuliko kushindwa, lakini kufanya kazi isiyo ya kimtandao kunakuwa na asilimia kubwa ya kushindwa kuliko kushinda na katika swala zima la kimtandao sumu kubwa ni kutenda jambo katika hali ya ubinafsi na sio shirika.

Ni kweli hulka ya kibinadamu inaweza kusema mimi naweza hata nikiwa peke yangu ukweli ni ngumu sana hasa kwa jambo la muda mrefu kwakua katika kufanya jambo kimtandao kunaleta wepesi na uharaka……….pamoja na hilo pia kama jambo mnafanya kitim lakini hakuna kushikamana basi bila wasi jambo hilo litakuwa kubwa badala ya kuwa dogo na litachukua muda mrefu sana badala ya kuchukua muda mfupi.

Jambo hili limekuwa ni shida kubwa katika utendaji kazi wa watu wengi wako walionza katika ushirika huu lakini baadae ukagawanyika na wako wanaondelea na ushirika lakini kila siku unapungua ubora wake na kutoa kiashirio kibaya…….sababu kubwa watu wameshindwa kwenda sawa na tofauti zao hivyo badala ya kujuana zaidi kukazalisha utengani wa mioyo na baada utakuja wa mwili.

Niseme mambo mengi yanashindwa kufika mbali kutokana na vitu viwili yaani mfumo usioeleweka(unstructure) na hatua yakufanikisha jambo hilo(strategies) hivi ni vitu vidogo sana lakini vina maana kubwa na uwezeshaji mkubwa katika utendaji wake.

Ni muhimu kama mmeweka utaratibu basi kila mtu aufuate huo utaratibu na kuhakikisha unatekelezeka na kamwe hakuna mtu aliyejuu ya huo utaratibu ili kuusaidia huo utaratibu unadumu na kufuatwa kikamilifu.

Na ni muhimu kujali vitu vyote viwili kwa pamoja yaani jambo linalo fanyika na wanaofanyakazi hiyo kwakua vyote ni muhimu katika uzalishaji.

Ilikuwa na mtandao wenye nguvu ni muhimu kuzingatia yafuatayo: UWAZI,UWAJIBIKAJI NA USAWA!

Imeandaliwa na ;

Cothey Nelson……………………………………………………………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni