NAISHI KWA RIDHAA YA NANI?
Hakuna kitu kizuri kama
kuishi hasa kuishi katika maisha unayoyataka, kwani kila binadamu ana uhuru
wake na matakwa yake………….ni jambo lililowazi kuwa binadamu yeyote ili aishi
anahitaji kutambua mambo matatu yanayoonyesha/dhihirisha utashi wa kuishi
kwake;
a)kuishi kwa matakwa ya
nafsi
b)kuishi kwa matakwa ya
dunia
c)kuishi kutokan na utu wako
hivi ni vitu vitatu ambavyo
ukiangalia kwa jicho la haraka haraka utaona kama kunakuingiliana au
kushabiliana lakini ukweli kwamba uko utofauti mkubwa katika kila kitengo na
utendaji wake.
Katika utendaji au maamuzi
ya mwanadamu yeyote yanaathiriwa na vitu hivi vitatu au kushawishiwa na na vitu
hivi…………..unaweza usiwe tayar i(utu) lakini nafsi yako ikakushawishi na unaweza
usipende lakini nguvu ya dunia ikakushinda na hatimae ukaamua au kutenda pasipo kupenda
au pasipo utayari ulio kamilifu.
Watu wengi wanakuwa na
shauku katika kutenda jambo ambalo litakalo furahisha moyo wake au kuleta
fahari katika maisha ya mtu husika lakini nguvu ya dunia inaweza kupindua
maamuzi yake au lile kusudio lake.
Hii ni moja ya shida
inayoikabili dunia kwa sasa kwani nguvu ya dunia imekuwa na uweza hata kuliko
maamuzi ya mtu husika au nafsi ya mtu mwenyewe, hii ni vita imekuwa ikila muda
mwingi na kuchosha watu wengi kutokana na mwenendo wake ni tofauti kabisa na
hali ilivyo au vile anavyotaka.
Wako watu walijitahidi kuwa
wakarimu,wenye upendo lakini hali hii haikudumu bali nguvu ya dunia ikawa vaa
na kujikuta katika kuwa na tabia sawa na dunia ilivyowaweka ndani yao kuwa na
kisilani,chuki na malipizo yasiyo na akili au yasiyoangalia mwendelezo wenye
maana.
Watu wengi wamekuwa
wakijifunza mara baada tu yakuona yaliyotokea kwa wengine hasa upande wa hasara
na wengine wanajifunza mara baada ya jambo jema kutokea kwa mtu lakini walio
wengi wamekuwa wakishindwa kuweza kuenenda sawa na walivyojifunza kwa wengine
wakajikuta kudumbukia mara ambapo dunia ikawazamisha
Matahalani mtu amejifunza au
kuona mtu alivyoathirika na ukimwi na mateso aliyoyapata lakini kutokana na
ushawishi wa dunia basi nae akajikuta anazidiwa na ile nguvu ya dunia na
hatimae naye kujikuta kaingia katika mateso hayohayo.
Ni vitu viwili tofauti kati
ya kujifunza na kutendea kazi hivi vitu havilingani kwani watu wengi
wanayojifunza sio yale wanayoyatenda………..mtu anaweza kujifunza kuwa sumu ya
panya inaua lakini mtu kwakujua kuwa kuwa ni kinywa sumu ya panya nitakufa
lakini bado anakunywa na huku akiwa tayari kufa bila shaka inakuwa nguvu ya dunia
imemzidi.
Ni lazima ujue kwamba kuishi
uku ukienda kinyume au kutoenda sawa na nguvu ya dunia unahitaji Nguvu kubwa,
maarifa ya kutumia hayo nguvu na kuwa mwepesi kwenda sawa na wimbi la mbingu!
Vijana wengi wanapotea,wazee
wengi wanapotea kwasababu na kushindwa kuimiri nguvu ya dunia na hatimae
kuwazamisha katika maji yenye kina kirefu na kushindwa kumudu.
►Kujifunza mambo ya dunia haitoshi ni
lazima ujifunze habari sahihi za mbingu! *Kwani
dunia inakamilika kunapokuwa mbingu na nchi.
“mjue
sana Mungu ili uwe na amani ndipo mema yatakapokujilia” ayubu 22:21
Imeandaliwa
na;
Cothey
Nelson………………………………..0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni