Jumanne, 25 Agosti 2015

UPANDE ULIO BEBA USALAMA WAKO



UPANDE ULIO BEBA USALAMA WAKO



Moja ya vitu vinavyopendwa na watu wengi ni usalama!

Kwakua katika usalama kuna utendaji katika uhuru na nafasi ya kufanya jambo lenye ubora wake.tuna fahamu kuwa moja ya kazi ya vyombo vya ulinzi ni kulinda mipaka ya nchi ( kuhakikisha usalama wa nchi wakati wote)

Na hichi ndicho kitu ambacho watu wengi ukitamani sana…..usalama wao pamoja na mali zao, kwakua wanajua katika usalama basi mambo mengi uwa rahisi kufanyika pasipo na ugumu usiokuwa na lazima.

Shida kubwa moja ya watu wengi wanapenda sana kuwa na usalama lakini namna wanavyoenenda wanaufukuzia mbali usalama wao na vitu vyao……….sawasawa mtu anayetumia dawa(dozi) katika hali mbaya lakini bado mtu anatumia kilevi kikali lakini katika hali hiyo bado anaamini Mungu atamsaidia.

Niseme wazi siku inapande mbili yaani usiku na mchana……..na hata dunia inapande mbili yaani uliosalama na usio salama, na hakuna ambaye apendi usalama lakini ugumu uko katika  kudhihirisha kuwa wewe unapenda usalama katika maneno tu au pia katika mfumo mzima wa maisha yako.

Kibinadamu yako mambo mengine mtu anafanya akiwa ametiwa giza akiamini anaona kumbe haoni sawasawa na mtu kuamini anajua kumbe ajui! Ndani ya dunia kuna mtindo ukiishi ambao utaondoa usalama wa maisha yako na kusababisha mambo mengine yazidi kukukabili.

Unahitaji kujua kwamba binadamu wewe ni sahihi kwamba uhuru ulionao unapaswa usifanane na wanyama katika utendaji wako na katika kutimiza hisia zako inakupasa ujue kuwa viumbe vyote vya dunia vinapaswa vijifunze kupitia wewe na sio wewe ujifunze kwao unaweza kukataa kabisa lakini ukweli ni kwamba mambo mengi tunayoyafanya yanafanana na wanyama kwa asilimia kubwa mathalani kupigana hadharani na matendo mengine yanayofanana na hayo.

Kuna maisha ya mengine mtu anaishi unaona mwisho wake wa maisha yake umebebwa na maumivu, kukataliwa na hata kutengwa lakini bado mtu anakuwa anakaza mwendo kuendelea, na ukiwasikiliza wanasababu nyingi wengi wakisema maisha magumu, nilikataliwa na wengine wanasema nimetendwa vibaya hivyo staili ya maisha haya ndio niliyoichagua hivyo na ishi maisha haya sio kama napenda bali inanilazimu.

Niseme kwamba kwa namana yoyote ulivyo, jua yuko mmoja tu ambaye atakupenda vile ulivyo na kutopenda aibu yako iendelee kwakua kwa yeye ulitoka na kwake utarejea, hivyo niseme wazi katika maisha yoyote unayoishi bado Mungu aliyenipenda mimi basi anakupenda nawe tena upendo uleule hakika ni baba mwema.

Niseme maadamu unaishi tu haijarishi uko katika hali gani nini kimeathiri mwili wako, akili yako na kuona kuwa umeharibu mstakabali wa maisha yako napenda ujue kuwa bado unayo nafasi kubwa kwa Mungu aliyekuumba anaweza akainawilisha tena ngozi yako na kuwa zaidi ya ulivyokuwa jana! Huna haja ya kulia na kusononeka sana bali yuko Mungu ambaye kwake yeye kila kitu kina nawilishwa na kuzidi kwa bora.

Mungu anasubiri maamuzi yako tu katika kurejea kwake naye akufanye kuwa mtu wa maana katika viwango vyake. Mungu awezi kukurahumu wala kukuchoka bali anajua kuwa kwa wewe unaweza kuwa mtu mwingine kupitia yeye.

Hivyo Mungu anasubiri umpatie maumivu yako,teso lako na dhihaka yako ili yeye achukue na kukuacha ukiwa huru mbali na mateso…………maana salama yako ndio furaha yake.

Giza katika dunia japo ni sehemu ambayo watu wengi upenda kufanya mambo yao kwasababu kuna maficho yao lakini hawapendi kujua kuwa ndani ya giza kuna upofu uharibifu na mateso yaliyobebwa na huzuni isiyokoma.

Nuru ya Mungu katika dunia hii……… hapo ni sehemu salama japo watu wengi hawapendi kwenda katika njia hiyo kwani haina mvuto lakini niseme kwamba katika nuru kuna nguvu na uimara uliobeba stara ya mwanadamu.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………0764 018535

Jumanne, 18 Agosti 2015

MVUTANO KATIKA KUISHI



NAISHI KWA RIDHAA YA NANI?



Hakuna kitu kizuri kama kuishi hasa kuishi katika maisha unayoyataka, kwani kila binadamu ana uhuru wake na matakwa yake………….ni jambo lililowazi kuwa binadamu yeyote ili aishi anahitaji kutambua mambo matatu yanayoonyesha/dhihirisha utashi wa kuishi kwake;

a)kuishi kwa matakwa ya nafsi

b)kuishi kwa matakwa ya dunia

c)kuishi kutokan na utu wako

hivi ni vitu vitatu ambavyo ukiangalia kwa jicho la haraka haraka utaona kama kunakuingiliana au kushabiliana lakini ukweli kwamba uko utofauti mkubwa katika kila kitengo na utendaji wake.

Katika utendaji au maamuzi ya mwanadamu yeyote yanaathiriwa na vitu hivi vitatu au kushawishiwa na na vitu hivi…………..unaweza usiwe tayar i(utu) lakini nafsi yako ikakushawishi na unaweza usipende lakini nguvu ya dunia ikakushinda  na hatimae ukaamua au kutenda pasipo kupenda au pasipo utayari ulio kamilifu.

Watu wengi wanakuwa na shauku katika kutenda jambo ambalo litakalo furahisha moyo wake au kuleta fahari katika maisha ya mtu husika lakini nguvu ya dunia inaweza kupindua maamuzi yake au lile kusudio lake.

Hii ni moja ya shida inayoikabili dunia kwa sasa kwani nguvu ya dunia imekuwa na uweza hata kuliko maamuzi ya mtu husika au nafsi ya mtu mwenyewe, hii ni vita imekuwa ikila muda mwingi na kuchosha watu wengi kutokana na mwenendo wake ni tofauti kabisa na hali ilivyo au vile anavyotaka.

Wako watu walijitahidi kuwa wakarimu,wenye upendo lakini hali hii haikudumu bali nguvu ya dunia ikawa vaa na kujikuta katika kuwa na tabia sawa na dunia ilivyowaweka ndani yao kuwa na kisilani,chuki na malipizo yasiyo na akili au yasiyoangalia mwendelezo wenye maana.

Watu wengi wamekuwa wakijifunza mara baada tu yakuona yaliyotokea kwa wengine hasa upande wa hasara na wengine wanajifunza mara baada ya jambo jema kutokea kwa mtu lakini walio wengi wamekuwa wakishindwa kuweza kuenenda sawa na walivyojifunza kwa wengine wakajikuta kudumbukia mara ambapo dunia ikawazamisha

Matahalani mtu amejifunza au kuona mtu alivyoathirika na ukimwi na mateso aliyoyapata lakini kutokana na ushawishi wa dunia basi nae akajikuta anazidiwa na ile nguvu ya dunia na hatimae naye kujikuta kaingia katika mateso hayohayo.

Ni vitu viwili tofauti kati ya kujifunza na kutendea kazi hivi vitu havilingani kwani watu wengi wanayojifunza sio yale wanayoyatenda………..mtu anaweza kujifunza kuwa sumu ya panya inaua lakini mtu kwakujua kuwa kuwa ni kinywa sumu ya panya nitakufa lakini bado anakunywa na huku akiwa tayari kufa bila shaka inakuwa nguvu ya dunia imemzidi.

Ni lazima ujue kwamba kuishi uku ukienda kinyume au kutoenda sawa na nguvu ya dunia unahitaji Nguvu kubwa, maarifa ya kutumia hayo nguvu na kuwa mwepesi kwenda sawa na wimbi la mbingu!

Vijana wengi wanapotea,wazee wengi wanapotea kwasababu na kushindwa kuimiri nguvu ya dunia na hatimae kuwazamisha katika maji yenye kina kirefu na kushindwa kumudu.

Kujifunza mambo ya dunia haitoshi ni lazima ujifunze habari sahihi za mbingu! *Kwani dunia inakamilika kunapokuwa mbingu na nchi.

“mjue sana Mungu ili uwe na amani ndipo mema yatakapokujilia” ayubu 22:21

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson………………………………..0764 018535

Jumanne, 11 Agosti 2015

NGUVU YA MTANDAO



NGUVU YA MTANDAO


 Mwanzo 11:1-6
“Bwana akasema,tazama,watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja ………………..wala sasa hawatazuiliwa neno wanalolikusudia.”

Sote tunajua pindi mtandao ukiwa vizuri basi mawasiliano yanakuwa mazuri na hata huduma zingine uweza kufanyika kwasababu mtandao umekaa vizuri! Na pindi mtandao unapokuwa chini au unaposumbua basi yako matatizo yanaweza kutokea kama ucheleweshaji wa taarifa au kutofika kabisa na pengine uweza kukosa huduma uliyokuwa unahitaka.

Ili mtando ufanye kazi lazima pawepo na mjumuhisho wa vitu vingi ili viwezeshe mtandao kuweza kutenda kazi katika ufanisi wake na pindi kifaa au kitu kimoja kinaposhindwa kufanya kazi yake basi uweza kusababisha ufanisi wa mtandao kuwa chini au kuwa duni.

Katika utendaji ulio na tija na ulio na uwezekano wa kufanya vizuri lazima wafanye kazi katika mfumo wa kimtandao au kishirikiana kitim( team work) ufanyaji kazi au utendaji wa shirika.

Ni wazi ili kufanya kazi au jambo katika ushirika wa kimtandao hatuna budi kila mtu kutambua nafasi yake na kila mtu lazima haiheshimu nafasi ya mwezake kuona kuwa naye anawajibika katika nafasi hivyo pasipo na hali ya kuzalauliana au kutoaminiana bali kila mtu awajibike akatika nafasi yake tena katika ufanisi huku akijua kwa yeye katika kuwajibika atapunguza mazigo kwa mwingine katika kuwajibika na hivyo kuwa na mchango wa uboreshaji wa kimtandao na sio kuzolotesha mtandao.

Kufanya kazi katika hali ya kimtandao kunatoa asilimia kubwa ya kushinda kuliko kushindwa, lakini kufanya kazi isiyo ya kimtandao kunakuwa na asilimia kubwa ya kushindwa kuliko kushinda na katika swala zima la kimtandao sumu kubwa ni kutenda jambo katika hali ya ubinafsi na sio shirika.

Ni kweli hulka ya kibinadamu inaweza kusema mimi naweza hata nikiwa peke yangu ukweli ni ngumu sana hasa kwa jambo la muda mrefu kwakua katika kufanya jambo kimtandao kunaleta wepesi na uharaka……….pamoja na hilo pia kama jambo mnafanya kitim lakini hakuna kushikamana basi bila wasi jambo hilo litakuwa kubwa badala ya kuwa dogo na litachukua muda mrefu sana badala ya kuchukua muda mfupi.

Jambo hili limekuwa ni shida kubwa katika utendaji kazi wa watu wengi wako walionza katika ushirika huu lakini baadae ukagawanyika na wako wanaondelea na ushirika lakini kila siku unapungua ubora wake na kutoa kiashirio kibaya…….sababu kubwa watu wameshindwa kwenda sawa na tofauti zao hivyo badala ya kujuana zaidi kukazalisha utengani wa mioyo na baada utakuja wa mwili.

Niseme mambo mengi yanashindwa kufika mbali kutokana na vitu viwili yaani mfumo usioeleweka(unstructure) na hatua yakufanikisha jambo hilo(strategies) hivi ni vitu vidogo sana lakini vina maana kubwa na uwezeshaji mkubwa katika utendaji wake.

Ni muhimu kama mmeweka utaratibu basi kila mtu aufuate huo utaratibu na kuhakikisha unatekelezeka na kamwe hakuna mtu aliyejuu ya huo utaratibu ili kuusaidia huo utaratibu unadumu na kufuatwa kikamilifu.

Na ni muhimu kujali vitu vyote viwili kwa pamoja yaani jambo linalo fanyika na wanaofanyakazi hiyo kwakua vyote ni muhimu katika uzalishaji.

Ilikuwa na mtandao wenye nguvu ni muhimu kuzingatia yafuatayo: UWAZI,UWAJIBIKAJI NA USAWA!

Imeandaliwa na ;

Cothey Nelson……………………………………………………………0764 018535