UTUMWA WA HIARI
Katika hali ambayo watu
wengi hawapendi kuishi wala kusikia ni hali hii inaitwa UTUMWA kwani ndani ya
hali hii inaambata na mateso ya nafsi na wakati mwingi ina ambatana na mateso
ya mwili, kiukweli unapozungumzia utumwa lazima uendane sambamba kufanya jambo
nje ya hiari binafsi (matakwa binafsi) lakini katika dunia ya sasa kuna utumwa wa kupenda au utumwa wa hiari
binafsi na wakati mwingine utumwa uendana sana na majonzi hasa katika moyo.
Hili neno UTUMWA alina
rafiki katika dunia, na kama ukiamua kuanzisha maandamano ya kuondokana na
utumwa wa nafsi basi bila shaka utapata wafuasi wengi na hasa tabaka la chini.
Kwa jinsi watu
wanavyolichukia hili neno watu wangekuwa na uwezo wa kuliondoa neno hili katika
kamusi basi wangeliondoa maana neno linachefua moyo! Kwakua alipendezi kutamkwa
wala maana yake bali linaonekana kama JANGA.
Adui mkuwa wa utumwa ni
uhuru, kwani palipo na uhuru basi hapo hakuna utumwa na palipo na utumwa basi
hapo hakuna uhuru hawa ni maadui ambao hawawezi kukaa sehemu moja na kuamua
jambo hilo kwa kushirikiana kama timu.
Kuna mambo mengine mtu
anaweza akaona ni ya kawaida kwakuwa watu wengi wanafanya na kwa mtazamo wa
kawaida unaweza kuona kama yanafaida katika maisha ya watu wanavyoishi kutokana
na hali ya kuzoelea kwa watu wafanyao mambo hayo au kutokana na tafsiri
inayotolewa na macho yako.
Utumwa wa hiari ni hali
ya mtu kujikuta kufanya jambo yeye binafsi kutokana kushindwa kufanya tofauti
na hali iliyopo na akili yake ikiona kuwa hakuna njia ila inabidi nikubaliane
na hali hii kwa maana wakati mwingine unaweza kujikuta katika hali mbaya zaidi
kwa kushindwa kufanya jambo unalopaswa kufanya.
Huu ni utumwa ambao
unajikuta wewe binafsi unatengeneza nafasi katika kukamilisha swala au jambo
unalolifanya kila siku au kila wakati, na huu ni utekwa katika upande wa akili
na mwili unakuta unafanya kwakujua lakini hauna njia mbadala nyingine ya
kufanya tofauti na vile unavyopaswa kufanya. Wakati mwingine utumwa huu unaweza
kufanya hata bila ya kusimamiwa na mtu na wakati mwingine unaweza kufanya kwa
shinikizo au kusimamiwa na mtu ila katika hali ya kupenda.
Huu ni utumwa ambao
wewe binafsi ndio unajua kwanini nafanya hivi na sio mtu aliye karibu yako au
mwenye nafasi yeyote katika maisha yako, kwakua kile unachokiamini wewe na
namna unavyopenda uwezi kuamini kama kuna mtu mwingine anaweza kukuelewa kama unavyoelewa/unavyoamini.
Huu ni utumwa ambao
hauwezi kuchoka katika kuenenda katika mtindo maisha ambao umeuchagua pasipo
kukata tamaa bali ni katika kuridhisha akili yako na mwili wako, wakati
mwingine unawezajua kuwa kitu hiki au jambo hili mwisho linaweza kuniweka
katika hali ngumu lakini bado utakuwa ukiendelea kufanya hivyo maana katika
kufanya hivyo ndio uleta burudiko la nafsi yako.
Kwakua huu ni utumwa
unaohusisha hiari yako hivyo inakuwa sio kitu rahisi tu kwa wewe kuwaza tofauti
na hasa katika hali unayostahili kuwa nayo, wakati mwingi unakuwa katika giza
japo unajikuta una hali ya kupenda pasipo kujua hasa maana yake nini na kujua
faida yake au matokeo yake katika jambo ambalo unalolitaka kulifanya.
Na ukumbuke kuwa utumwa
wa hiari unazaliwa pale tu akili inapokosa kutawala jambo Fulani katika
mwenendo mzima wa maisha yako, jambo hilo linaweza kuwa la siri au wazi lakini
linakuwa lina nguvu hata kushindwa kuzuiwa na akili au mwili wako, utumwa huu
unakupa nguvu hasa unapotambua hakuna mtu anayekuona hivyo unakuwa huru kutumia
uhuru wako.
Hakuna nguvu ya kweli
inayoweza kuzaliwa hapa ikiwa tu tayari utumwa wa hiari utakuwa ukisababisha
giza kuzidi kuchukua nafasi katika maisha yako, na mwisho utakapojitokeza
unaweza ukaweka wazi yale yote yaliyo uteka mwili wako na akili yako.
Imeandaliwa
na:
Cothey
Nelson…………………………………………………………0764 018535
UTUMWA NI TESO LA NAFSI
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni