Uhitaji ni swala lisiloweza kuachwa nyuma katika hali yoyote, tukikubaliana wote kuwa ili maisha yaweze kuendelea hatuna budi kutimiza uhitaji wa kitu husika mathalani binadamu ili aendelee kuishi hana budi kutimiza uhitaji wa mwili na moja la hitaji ni chakula, mbali na hilo hata gari ili liweze kwenda linahitaji vitu vingi pamoja na vyote moja ya kitu muhimu ni mafuta ( petrol au diesel) , kama mafuta yakiwa yamekwisha hata ukiwa mtaalamu kiasi gani hama dereva unayesifiwa kijiji kizima bado utashindwa kuliondoa gari hapo kwa kuliendesha.
Ukiangalia mmea ili ukue unahitaji vitu vya msingi kama vile mwanga, hewa, maji na udongo kwa kupata mahitaji hayo itarahisisha katika ukuaji wake vilevile katika mwili wa binadamu una mahitaji mengi lakini kimojawapo ambacho ni muhimu ni MAJI, tukiachana na hilo wataalam wanasema binadamu ana mahitaji makuu matatu: chakula, maradhi na mavazi.
Hivyo uhitaji ni kitu kisichoweza kukwepeka!
Karibu……………………………………………..
Hakuna kitu kizuri kama unapo kuwa na uhitaji wa kitu uka kipata kwa wakati muhafaka maana najua kuna raha inazaliwa pindi unapo kipata kitu unachokipenda, mathalani unapokuwa na kiu ya maji utapenda upate maji ili kiu kiondoke na kawaida uhitaji ndo uzaa matamanio na hapo jitiada na mikakati uweza kuzaliwa.
Na ni kipindi hiki ambacho unaweza usimuelewe mtu pindi mtu anapo sumbuka katika kukizi uhitaji wake mathalani wanandoa wanaotaka kufunga ndoa na siku zimeisha na mambo ya msingi hayaja kaa vizuri unaweza usishangae kukutana nae kila eneo utakalopita mjini, barabarani na hata maeneo mengine, sio kwamba anapenda kurukaruka ila uhitaji wa kitu unamsukuma kufanya hivyo japo jambo hili sio hitaji la msingi ( kwa maana hauwezi kuishi bila kufunga ndoa) ila ni matwaka yaliyo ambatana na taratibu za jamii fulani.
Unahitaji neema ya Mungu na sio watu ili kukamilisha uhitaji wako!
Watu sio kwamba hauta wahitaji bali watapatikana ndani ya neema ya Mungu, maana Mungu atakupa watu wakukamilisha uhitaji wako, uwa katika picha ya haraka haraka sio rahisi kuona umuhimu wa neema ya Mungu hasa jambo unaona linawezekana kufanyika katika hali ya kawaida ,
Ila mara nyingi tunaona umuhimu wa neema jambo linapoanza kuwa gumu hama kuwa na picha ya kushindikana hapo utaanza kuona umuhimu wa neema ya Mungu, ni muhimu kutambua kila jambo linalokutokea linahitaji neema kwa kiwango kikubwa hama kwa lugha nyepesi unahitaji neema ya Mungu kwa asilimia zote.
Kikubwa kutambua watu wanaweza kukuacha hama kukusahau lakini sio neema ya Mungu ikikuambata haita kuacha kamwe kwa kifupi neema ya Mungu ni hitaji la dunia ukiikubali utaona utofauti wake uki kutofautisha katika utendaji wako.
Ni muhimu kuruhusu utawala wa kweli ya Mungu katika maisha yako ili neema yake uzidi kuiona ikiongoza akili yako na kukupa wepesi katika utendaji wako.
INAITWA SIKU! BARIKIWA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni