Ijumaa, 17 Januari 2020

BAADA YA DHIHAKA KUNA HESHIMA!




1 petro 1: 11……..Wakatafuta ni wakati upi, na wakati wa namna gani ulioonywa na Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo, na utukufu utakaokuwako baada ya hayo.

Uwa tunaifurahi leo kwasababu tumeipita jana na tunaitumaini kesho kwakuwa tunaishi leo,
Mathayo 17: ( 24-27 )…… 24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

                                         25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
                                         26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;
                                          27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Tuna tambua katika machafuko hapo uimara wa mtu uonekana, na ni katika msingi ulioshikiliwa na neno lazima uwe salama katika dhoruba yoyote.

Moja ya kitu kinachopiganiwa sana na watu ni kuwa na heshima “ kuheshimika” maana itazidi kumjengea nafasi katika jamii aliyekuwepo.

Japo ni mtego mkubwa kwakuwa watu wengi wako tayari kupata heshima lakini awako tayari kudhihakiwa pasipo kujua wakati mwingine dhihaka uweza kukupeleka kwenye heshima. Ndomana wengine uweza kusema baada ya taabu/dhiki faraja!

Inakuwa sawa na mtu anataka kuvuna pasipo kujigharimu katika kupanda!

Imekuwa ni rahisi mtu kuikabili dhiki/changamoto baada ya kuona kuna neema mbele yake lakini sio kitu rahisi kuikabili dhiki/changamoto kama hataona neema itakayozaliwa baada ya hapo.

Unapoamua kuishi na Mungu hayo majira uwezi kuyakwepa kwakuwa yapo ili kuhakikisha heshima yako inadumu na sio kushuka ni sawa mjenzi wa ghorofa lazima haende chini sana ili apate uwezo wa kwenda juu sana.

Kila mtu upenda heshima lakini ni muhimu kutambua heshima inatengenezwa unaweza jua au kutojua lakini ukitembea kwenye kanuni basi matunda yake yatadhihirika tu.

Unapotambua baada ya dhiki kuna heshima haupaswi kuishi maisha ya unyonge au ya ukiwa bali ni kipindi cha kuimarisha roho+akili+mwili wako tayari kuingia katika hatua nyingine ya maisha yako iliyobeba heshima yako.
Kipindi cha dhihaka kinakuwa kigumu sana kwa mtu asiyejua namna gani ya kuishi katika kipindi hicho, unaweza kukuta mtu katika kipindi hiki amejawa na lawama, huzuni na teso lisilokoma, na hali hii inaweza pelekea kushindwa kuifikia heshima yake.

Unapaswa kujua heshima inakuja, katika kujibu maswali yaliyo jikita katika fahamu zako na hata kuondoa pumziko la roho yako na sio kuwa kikwazo kwa wenzako.

Na heshima ya kudumu haiji tu kwasababu imetokea tu bali kwasababu unastahili, hivyo ni lazima ustahili kwanza ili heshima iweze kuja kwakuwa kila jambo linatokea katika mazingira yake na kama si mazingira yake ni vigumu kutokea.

Ni muhimu kuzingatia katika dhiki uko na nani ili heshima ije!

Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. ” zaburi 23:4

Usije ukaishi maisha ya kufuata mwili ukategemea heshima ya Mungu ikuambate/kukufunika kwa kuwa heshima yake haichanganywi .

Unapopita katika dhiki pamoja na Mungu basi hapo tegemea heshima ya Mungu kukuinua.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………….0764 018535


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni