Ijumaa, 3 Januari 2020

AMANI YANGU INATUNZWA NA YEYE!




Yohana 14:27
“Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga”.

Moja ya bidhaa/kitu adimu katika ulimwengu wa sasa ni AMANI, maana palipo amani ndipo radha ya kitu unachokifanya unakiona,mtu uliye naye au mahali uliopo upafurahie na siku zote uona sababu au umuhimu wa kuwa hapo.

Moja ya kitu ambacho mtu angetamani awe nacho siku zote za maisha yake ni Amani ya kudumu ndani ya maisha yake, na kizuri zaidi amani ikiwepo udhihirisho wake utaonekana ila amani inapotoweka viashirio vyake utaviona na hapo unyonge na ukiwa pamoja na hali ya kutoendelea uweza kujitokeza na hata kupelekea kupoteza mwelekeo.

Tatizo sio kuwa na kitu bali ni namna utakavyo kitunza ili kiendelee kuwepo “ uki kitunza kitadumu “
Namna unavyokaa nacho kinaweza kuzidi kukita mizizi yake au kupoteza utawala wake.

Wako watu amani yao inatunzwa na kazi nzuri aliyonayo, rafiki mwenye uwezo wa kumsaidia apatapo shida, mchumba au mali alizonazo n.k , inapotokea vitu hivyo vikipotea/kuondoka uwa vinaondoka na amani yake kwakuwa vitu hivyo ndivyo vilivyo shikilia amani yake hama ndicho chanzo cha amani yake ( hivyo vinaondoka na amani yake ).

Sio rahisi kujua msingi wa amani wa kila mtu unayemuona ( hasa jamii ya waaminio/ waendao kanisani ) uwa wengi upenda kusema “ amani yangu ina Mungu” huna haja ya kubishana nao, subiri vile vitu halisi/ hasa vinavyoshikilia amani yake pindi vitakavyopata mtikisiko utoshangaa hata ratiba za kanisani zitaanza kupungua na kuanza kambi za ghafla ghafla pamoja na maombi yasio kuwa na mpangilio maalum bali yanasukumwa na hisia pamoja na msongo wa mawazo.

Kujua kuwa “ amani yako inatunzwa na Mungu “ na kuifanya “ amani yako itunzwe na Mungu “ hivi ni vitu viwili tofauti ni sawa sawa na mbingu na nchi, uwezi kuirahisisha kimawazo ukasema mbingu na nchi vinafanana ukaachana na uhalisia uliopo!

Natambua kuna vionjo vya mwili vinavyobebwa na matukio mazuri yanayomtokea mtu mathalani kuifikia/kuikamilisha ndoto yake, moyo uweza kuchangamka na kusababisha tabasamu kwenye uso.

Hatua ya kwanza ili uwe na amani iliyozaidi ya amani zote jambo muhimu lazima umpate Mungu kwanza ili akupe amani yake hiyo AMANI hainaga mbadala, uwezi kutamani amani ya mtu wakati mtu mwenyewe umtaki! Lazima umpate mtu hapo ndipo utaanza kuiona amani yake.

“ palipo na yeye amani yake ipo”.

Usikubali “ kujitekenya na kucheka mwenyewe ” huku ni kupoteza muda unapoamua kuwa na amani ya Mungu basi hakikisha unampata Mungu kwa ukamilifu wake.

Hii itafanya/kuzidisha mng’ao wako kuzidi wala usififie maana uko katika amani inayonawirisha.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………………………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni