Ijumaa, 27 Machi 2020

LA MSINGI!




Tunasema ni siku nyingine kwakuwa kulikuwa na siku kabla ya leo………………….!

Karibu…………….!

Unaweza kukaa na mtu kwa muda mwingi ukicheka naye na hata kutaniana naye na hata ikiwezekana kula pamoja naye, ukawa mvumilivu kwa huyo mtu na hata ukaacha baadhi ya shughuli zako kwa ajili ya kutoa umakini wako wote ukitaka kujua ujio wa huyo mtu ulikuwa na lengo gani hasa?

Kwa kiasi kikubwa ujio wa mtu kwako unaweza kuubashiri katika muonekano wa sura pamoja na tone ya sauti yake ( huzuni au furaha ) uweza kubashiri kitu na kuanza kuandaa moyo wako kupokea kitu kitakachosemwa na mtu husika.

Na inakuwa mchanganyo kidogo kama sio sana pindi utakapo bashiri kitu ambacho mtu atasema na wewe lakini ikiwa tofauti kabisa na kile anachosema, mathalani unaweza ukawa na changamoto ya kifedha ghafla mgeni akakutembelea na kwa muonekano wa kawaida ukajua kuwa huyu mtu yuko vema nawe ukafikiri hapa ndipo mahali pa kuponea ili siku hiyo isipite bure lakini ukashangaa mtu huyo anakwambia “ biashara zangu zimekwama kidogo ningepata kiasi fulani cha fedha kingenisaidia katika kipindi hiki “

Bila shaka ukiwa na moyo mdogo unaweza kujikuta kimoyomoyo unaomba aondoke tu maana hana faida kwako kwa wakati huo na ikitokea anaendelea na mazungumzo mengine unaweza kujibambikizia shughuli ya kufanya hapohapo tu ili mradi tu aondoke au ukaunda safari ya ghafla ili mradi uepukane naye.

Ni jambo la kawaida tu unapomuhitaji mtu kuongea naye ukweli vinywaji na chakula vinaweza visiwe vya msingi kwake bali kile kiini/lengo kuu la kikao hicho ndicho kitakuwa cha maana kwake.
Hutakosa kusikia mtu katika hali ya kujuta baada ya kutopendezewa na jambo la msingi lililoendelea katika mazungumzo hayo……………..hizi ni baadhi ya kauli zake:

“ mi nilifikiri ameniitia jambo la maaaaana sana kumbe hakuna kitu “

“ tangia siku hile ya kile kikao na alichoniambia thamani yake nimeishusha kabisa kwangu mimi nilifikiri ataniambia jambo la msingi kumbe ujinga mtupu “

NOTE: Ni jambo la msingi wakati mwingine mkanganyo mkubwa utokea katika jambo husika lakini linaweza lisiwe la msingi kwa sasa lakini likawa la msingi katika hatua inayofuata katika maisha yako.

Karibu katika somo……………………………………………!!!

Katika jambo lolote linalo muhusisha Mungu jua katika utendaji mzima wa hilo jambo linamuhitaji Mungu kuliko kitu chochote, na ni muhimu zaidi kuliko oxgen katika maisha ya mwanadamu maana ukikosa oxgen unaweza kufa kimwili ila ukimkosa Mungu utaangamia roho na mwili pia.

Na hata katika mambo ya kushirikiana katika shughuli za kibiashara la muhimu nguvu ya uchumi na wazo lililobora ulilokuwa nalo.

Ni kweli kabisa katika kufanikisha mambo mengi, watu na mtaji ni muhimu lakini sio muhimu kuliko Mungu, kwakuwa vyote vya tokana na Mungu.

Na ni muhimu kujua ili ufanikishe mambo ya kimungu katika hali yoyote ni muhimu sauti ya Mungu iwe nguvu katika moyo wako kuliko jambo lolote, sauti zisizo ambatana kweli ya Mungu zisiwe na nguvu kwako kwakuwa watu uliwakuta na utawaacha lakini Mungu ulikuwa naye kabla ujatokea katika ulimwengu wa nyama na hata hitimisho lako limebebwa na yeye.

Sizungumzii kuwa watu sio wa muhimu la hasha! Bali hekima inahitajika katika utendaji maana hakuna aliyezaidi ya mwingine wala aliye chini ya mwingine! Ila katika yote Mungu anabaki kuwa Mungu.

Ukimfanya Mungu kama kiongozi wako na ikiwa jambo LA MSINGI katika maisha yako hauwezi kupoteza na kufika kwenye hatima yako ni jambo lisilopingika.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………..................…………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni