Ijumaa, 17 Aprili 2020

MAISHA YAKE NDANI YANGU!




Ni kauli au msemo ulio na hali ya ugumu au kutowezekana pindi utakapo amua kuutafakari kwa kina “maisha yake ndani yangu” !!!

Ni ngumu tu kuishi ndani ya maisha ya mwingine! Kwakuwa yeye anayo ya kwake (anayoyapenda/ matakwa yake) na wewe unayo ya kwako (ubinafsi) na kila mtu ujisikia vizuri kuishi maisha anayoyataka, maisha ya uhuru binafsi ndiyo yanayopelekea furaha ya kweli…!

Japo inawezekana kwakuwa endapo utaishi katika hali hii itafanya wepesi kuyapata mambo ya mwingine pindi utakapoishi huku ukiufurahisha moyo wake, hapo utayajua kwa mapana zaidi yanayoendelea moyoni mwake na kufaidika matunda yake.

Kuna kutamani kuishi maisha ndani ya mtu na kuna kuthubutu na kudumu katika maisha ya mwingine!

Ni furaha ya mzazi kuona mtoto wake anafanana naye katika muonekano lakini inakuwa na maana zaidi kwake kama mwenendo wake utafanya wengine wabarikiwe/wapendezwe nao.

Unapokuwa ujui njia ni vigumu tu kuwa kiongozi wa hiyo safari, maana hamtofika mnapotakiwa kwenda na hata ikatokea bahati umefika unaweza usijue kama umefika maana huna mwelekeo sahihi wa wapi unatakiwa kwenda au kuwa.

Kuyaishi maisha ya mwingine lazima uweze kuyasahau maisha yako, kiwango cha kuyasahau maisha yako ndicho kiwango cha kuyaishi maisha ya mwingine.

Moja ya kitu kinachoweza kuleta mshikamano zaidi/kuongezeka kwa upendo ni namna ya kila mtu mmoja kujisahau na kuanza kuishi kwa ajili ya mwenzake tu.

1 petro 4:8zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.

“ Maisha yake ndani yangu” hama! Ni kauli iliyojaa lugha ya kufikirika sana kama sio ya picha na hali ya kutowezekana kwa mtu kuishi ndani ya maisha ya mwingine kwa kuwa kila mtu anaishi maisha yake na zaidi sana matakwa hayafanani na hata ya kifanana sio kwa asilimia zote.

Kuna mambo mengi utayapata endapo utakubali kuishi ndani ya mtu na kuna mambo utayakosa endapo utaishi nje ya mfumo huo hata kama utaonyesha utayari kiasi gani kwa huyo mtu?

Ni kusudi la Mungu kuona tunaishi katika maisha yake ili kuyafikia yale yaliyo mipango yake.

Ufike hatua ya kuonyesha ni kweli unaishi lakini sio maisha yako bali wewe unaifuata njia ambayo wengine awaioni au awaielewi.

Yohana 8:29……Naye aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.

Raha ya kitu ni pale utakapoamua kukipendeza kwa asilimia mia nacho kitafanya au kudhihirika na kupata faida.

Bidii yako ya kuishi nje yako ndio neema ya yule unayeishi kwa ajili yake inaongezeka katika maisha yako.

 “ Nje yake hakuna vitu vyake bali ndani yake kuna mambo yake”

Usitegemee kupata vya kwake kama ukiamua kuishi nje yake maana nje yake hakuna neema yake.

Usipoteze muda kufikiria maisha yake ndio maisha yako wakati namna sahihi ya kufanya ili yeye aishi kupitia wewe hipo.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni