Moja ya kitu kinachosababisha majuto katika maisha ya mtu ni
kufanya maamuzi akiwa katika hali ya kukosa utulivu, wakati mwingine hali hii
ya kukosa utulivu inaweza sababishwa na hasira pamoja na jazba. Mathalani mtu
mmoja pindi atakapoamua kumchoma kisu mwenzi wake kwasababu ya jambo baya
alilolifanya au kwakuhisi tu……….baadae, hicho kitendo alichokifanya kinaweza
kumgharimu maisha yake hata kujuta kwanini amefanya hilo jambo hata kujikuta
yuko jela au uraiani katika maisha ya mateso.
Niseme wazi katika hali yoyote iliyo ndani ya moyo wa
mwanadamu uwa inatoa majibu inawezekana katika hali ya utulivu au kukosa
utulivu bado kutakuwa na majibu, japo sio kila kila jibu unalolitoa linaweza
kuwa sahihi katika swali ambalo unalopaswa kulijibu ndomana ata katika mitaala
ya elimu unapopewa mtihani na kuamua kujibu unaweza kupata au kukosa!
Inaaminika majibu sahihi au mazuri yanategemea sana ulimwengu
wa utulivu, maana hapo panakutafakari maisha yatakayoendelea mara baada ya
kutoa maamuzi au majibu katika jambo husika.
Kwani moja ya sifa ya majibu yatokanayo na hali ya utulivu ni
majibu yaliyojaa usalama ndani yake na wala sio kisasi wala kukomoa.
Ni muhimu kutokukubali kusema kwakuwa watu wanakujaza
upepo wa kusema hama kuona nisiposema
heshima yangu itashuka hama wazfa wangu utakosa nguvu.
Ni muhimu huo utulivu ubebwe na Mungu mwenyewe na wala sio
akili zako, maana akili zako zinaangalia maslahi yako lakini Mungu anaangalia
maslahi ya ufalme wake, kwakuwa kwa kiasi kikubwa maslahi yako yanawezaleta uharibifu
katika ufalme wa Mungu lakini ufalme wa Mungu utaimarisha maisha yako.
Utulivu katika Mungu ni jambo jema sana na wala sio kitu cha
kuzoelea bali ni kitu cha kuwa makini nacho ili kikurahisishie kufikia hatma
yako, ni afadhali ukose vyote lakini uwe na utulivu wa kutosha na Mungu maana
kupitia hali hiyo inakuwa rahisi kutembea katika mwelekeo na Mungu utakaokupa
mwanga katika maisha yako.
Ni muhimu uhakikishe jibu lako linajenga ufalme wa Mungu na
wala sio kustawisha nafasi/heshima yako
maana nafasi yako inakipindi tu cha muda fulani na wala sio cha milele ndomana
wanasema “ cheo ni dhamana “.
Unahitaji kujua thamani uliyonayo mbele za Mungu ndio
hiyohiyo aliyonayo mtu mwingine, hivyo tambua hakuna mwenye nafasi zaidi ya
mwingine hivyo jibu lako lijengwe katika upendo wa kristo. ( mpende jirani yako
kama nafsi yako ).
Unahitaji kuona kama Mungu anavyoona ili uweze jibu kama
Mungu angelikuwepo angelijibu.
“ majibu yako ya leo ndio mstakabali wako wa kesho”
INAITWA SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson…………………………………………………………………………….0764
018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni