Ijumaa, 15 Mei 2020

MEMA YA MACHO vs MEMA YA MUNGU




Moja ya kazi ya macho ni kuona na akili kutafsiri kile ulichokiona,hivyo ni muhimu uone ili uweze kujua kuwa haya mema au si mema! 

Utakapo amua kuishi katika macho ya nyama utaona mema mengi yanayokuvutia na hata kukushawishi kuyapata hivyo hivyo ukiishi katika Mungu utaona mema ya Mungu japo wakati mwingine yanaweza yasivutie.

Ni jambo la kawaida binadamu kupenda mema au kutendewa mema na pindi anapokosa kuyapata hayo mema uweza kujikuta kuishi maisha ya ukiwa.

Ni kweli sio kila mema unayoyaona yanaweza kukupeleka pema hasa yanayotokana na macho ya nyama, kwakuwa chochote ili kikupate ni lazima kiwe katika hali ya kukuvutia ( muonekano wa nje kama kuna mema ). Na ndomana ata Eva ili ale tunda kwanza alivutiwa nalo na pia alishawishika na hali ya kujua mema na mabaya.

Usitegemee kuona mema nje ya kile kilichoko ndani yako, dunia ikiwa na nguvu ndani yako basi hapo tegemea macho ya nyama kuwa na nguvu basi hapo inakuwa ngumu kuona kwa jicho la Mungu.

Japo wakati mwingine unaweza kuwa na Mungu lakini usiyaone mema ya Mungu kwasababu akili imekataa kukubaliana na macho ya Mungu.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya mema ya macho na mema ya Mungu!

Ni tarajio la Mungu tuone mema kupitia yeye ( Ruth & Ibrahim ) maana katika yeye mema yanapatikana lakini sio mema yanayozaliwa na macho nyama, uharibifu unaweza kuzaliwa au kupatikana.

Mema ya macho yana mwisho, haijalishi hayo mema unayatazama vipi au yana mng’ao upi jua kuna mahala itafika mwisho haijalishi uliutegemea au haukutegemea…kwa kuwa chochote kinachoonekana kwa macho, mara nyingi kinakuwa kimetengenezwa au kimejitengeneza na uwa vitu vilivyo na sifa hizi uwa vinakuwa na mwisho kwakuwa vimetoka kwenye mikono ya wanadamu lakini mema yanayoonwa kwa macho ya Mungu, kwakuwa yanatengenezwa na Mungu na kwakuwa Mungu hana mwanzo wala mwisho naam ndivyo yatakavyokuwa mambo yake ( kwakuwa vile alivyo ndivyo mambo yake yatakavyokuwa).

Ni dhana isiyo sahihi kuwa tunaweza pata mambo ya Mungu kwakuwa watulivu/ wakimya, bali mpaka tumpate Mungu ili tuweze kuona kama anavyoona, lazima uyaone ili uyapate maana hauwezi kukipata kitu usichokiona.

Wakati mwingine kuna gharama kubwa katika kuyapata mema ya Mungu kwakuwa wakati mwingine tunayapata mema yake baada ya kukosea sana hivyo neema ya Mungu inaturudisha katika njia yake au jambo lake.

Ni muhimu kujua kuwa ustawi wako uko mikononi mwake Mungu na ili uupate ni vyema uone kama yeye anavyoona nje ya hapo mbwembe zote zitakupeleka shimoni tu.

Hauhitaji mambo mengi, bali unahitaji mema ya Mungu ili uwe salama na ndipo utaanza kufurahia wokovu wako na maisha yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni