Ijumaa, 29 Mei 2020

MUNGU HAKOSEI




Kitu ambacho MAJAMBAZI, MAFISADI, MAJANGIRI NA HATA WANASIASA…… hawawezi sahau kusema “KAZI YA MUNGU HAINA MAKOSA” hasa wanapokuwa wamepewa nafasi kuongea katika hali ngumu iliyo wakuta watu fulani au jamii kwa ujumla wake.

Naam unaweza kuwa binadamu wa kwanza pindi utakapoinuka na kusema Mungu anamakosa au anakosea! Kwasababu katika hali ya kawaida watu wengi wanamuogopa Mungu kuliko kumuheshimu.

Na utakuwa binadamu wa kawaida kama sio mwenye busara utakaposema MUNGU HAKOSEI! Japo hili neno sio wakati wote linakuwa na maana sana kwa mtu anayelisikia au kulitamka kutokana na mateso au maumivu yaliyo ndani ya moyo wa mtu husika.

Japo wakati mwingine mazingira na uhalisia wa mambo yanayoonekana na kile anachokisema Mungu ina onekana kuwa haiwezekani tena hata kama yeye anasema! Kwa kuwa dhoruba inapokua kali na moyo uweza kupoteza matumaini yake.

Ahadi ya kuingia nchi ya kanani!
Yoshua 1:6 Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa.
Imani uweza kufifia pindi unapowaona watu kama majitu!

Hesabu 13:33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.
Pindi unapotambua/ kusikia ahadi ya Mungu juu ya maisha yako, usifikiri tu kwasababu amesema basi itakuwa tu hata kama niki lala au kuisubiria tu itakuwa au itakuja tu sio kitu chepesi kama utakavyo fikiria.

Uwa ahadi ya Mungu inapoachiliwa ndivyo vita vinainuka kuizima hiyo ahadi isi dhihirike katika mwili au isitimie.

Hata yesu alipotaka kuzaliwa na hata alipozaliwa vita dhidi yake ikaibuka………..hata malaika akamtokea yusufu na kumwambia aondoke!

Luka 2:9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu.
          10 Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;
          11 maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
Kwa hivyo ni muhimu kutambua kuwa kitu kipya kinapotaka kuzaliwa hapa anga linatambua na hata kuweka kizuizi dhidi ya hicho kitu.

Mathayo 2:13 Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.

Hali ya kutambua kuwa Mungu hana kawaida ya kukosea, hali hiyo lazima idumu katika maisha yako mpaka ahadi hiyo itimie, uwa Mungu anaposema anakuwa ameshamaliza ahitaji nyongeza tena zaidi ya kuona imetimia.

Ni muhimu kutambua ni kweli Mungu hakosei ( maana ajawai kukosea ) ila wewe unaweza ukakosea ukasababisha ukose ahadi ambayo Mungu aliiandaa kwa ajili yako.

Ahadi ya Mungu hipo na inapotoka uwa imetoka inategemea mazingira yake ili kutendeka zaidi ya asili ya neno lenyewe lisiloshindwa, lenyewe liko zaidi ya mazingira yote na linajitosheleza alihitaji usaidizi wowote, maana neno la Mungu ndio asili ya vyote hata vile unavyo viogopa vinaweza kumezwa hama kusimamishwa na neno.

Na ni muhimu akili yako ijue kwamba kabla ya wewe ujazaliwa naam hata dunia kabla haijaumbwa mpaka leo Mungu ajawai kukosea japo wakati mwingine kutokana na akili zetu zilizo na mipaka unaweza kuhisi hama kuwaza kwamba Mungu anakosea kutokana na muono wako lakini sio sahihi, kwakuwa hiyo ni akili yetu sio akili yake.

Na ukumbukwe hakuna mtu/kitu kinachoweza kumrekebisha Mungu maana vyote vilifanywa naye zaidi sana Mungu kuachilia siri yake katika akili zetu mathalani ukuaji wa vitu: mimea, wanyama na viumbe vingine lakini sio kuviboresha zaidi ya kujifunza kwanini iko hivyo/ inakuwa hivi.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………….0764 018535


Ijumaa, 15 Mei 2020

MEMA YA MACHO vs MEMA YA MUNGU




Moja ya kazi ya macho ni kuona na akili kutafsiri kile ulichokiona,hivyo ni muhimu uone ili uweze kujua kuwa haya mema au si mema! 

Utakapo amua kuishi katika macho ya nyama utaona mema mengi yanayokuvutia na hata kukushawishi kuyapata hivyo hivyo ukiishi katika Mungu utaona mema ya Mungu japo wakati mwingine yanaweza yasivutie.

Ni jambo la kawaida binadamu kupenda mema au kutendewa mema na pindi anapokosa kuyapata hayo mema uweza kujikuta kuishi maisha ya ukiwa.

Ni kweli sio kila mema unayoyaona yanaweza kukupeleka pema hasa yanayotokana na macho ya nyama, kwakuwa chochote ili kikupate ni lazima kiwe katika hali ya kukuvutia ( muonekano wa nje kama kuna mema ). Na ndomana ata Eva ili ale tunda kwanza alivutiwa nalo na pia alishawishika na hali ya kujua mema na mabaya.

Usitegemee kuona mema nje ya kile kilichoko ndani yako, dunia ikiwa na nguvu ndani yako basi hapo tegemea macho ya nyama kuwa na nguvu basi hapo inakuwa ngumu kuona kwa jicho la Mungu.

Japo wakati mwingine unaweza kuwa na Mungu lakini usiyaone mema ya Mungu kwasababu akili imekataa kukubaliana na macho ya Mungu.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya mema ya macho na mema ya Mungu!

Ni tarajio la Mungu tuone mema kupitia yeye ( Ruth & Ibrahim ) maana katika yeye mema yanapatikana lakini sio mema yanayozaliwa na macho nyama, uharibifu unaweza kuzaliwa au kupatikana.

Mema ya macho yana mwisho, haijalishi hayo mema unayatazama vipi au yana mng’ao upi jua kuna mahala itafika mwisho haijalishi uliutegemea au haukutegemea…kwa kuwa chochote kinachoonekana kwa macho, mara nyingi kinakuwa kimetengenezwa au kimejitengeneza na uwa vitu vilivyo na sifa hizi uwa vinakuwa na mwisho kwakuwa vimetoka kwenye mikono ya wanadamu lakini mema yanayoonwa kwa macho ya Mungu, kwakuwa yanatengenezwa na Mungu na kwakuwa Mungu hana mwanzo wala mwisho naam ndivyo yatakavyokuwa mambo yake ( kwakuwa vile alivyo ndivyo mambo yake yatakavyokuwa).

Ni dhana isiyo sahihi kuwa tunaweza pata mambo ya Mungu kwakuwa watulivu/ wakimya, bali mpaka tumpate Mungu ili tuweze kuona kama anavyoona, lazima uyaone ili uyapate maana hauwezi kukipata kitu usichokiona.

Wakati mwingine kuna gharama kubwa katika kuyapata mema ya Mungu kwakuwa wakati mwingine tunayapata mema yake baada ya kukosea sana hivyo neema ya Mungu inaturudisha katika njia yake au jambo lake.

Ni muhimu kujua kuwa ustawi wako uko mikononi mwake Mungu na ili uupate ni vyema uone kama yeye anavyoona nje ya hapo mbwembe zote zitakupeleka shimoni tu.

Hauhitaji mambo mengi, bali unahitaji mema ya Mungu ili uwe salama na ndipo utaanza kufurahia wokovu wako na maisha yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………..0764 018535

Ijumaa, 1 Mei 2020

MAJIBU YALIYO NDANI YA UTULIVU




Moja ya kitu kinachosababisha majuto katika maisha ya mtu ni kufanya maamuzi akiwa katika hali ya kukosa utulivu, wakati mwingine hali hii ya kukosa utulivu inaweza sababishwa na hasira pamoja na jazba. Mathalani mtu mmoja pindi atakapoamua kumchoma kisu mwenzi wake kwasababu ya jambo baya alilolifanya au kwakuhisi tu……….baadae, hicho kitendo alichokifanya kinaweza kumgharimu maisha yake hata kujuta kwanini amefanya hilo jambo hata kujikuta yuko jela au uraiani katika maisha ya mateso.

Niseme wazi katika hali yoyote iliyo ndani ya moyo wa mwanadamu uwa inatoa majibu inawezekana katika hali ya utulivu au kukosa utulivu bado kutakuwa na majibu, japo sio kila kila jibu unalolitoa linaweza kuwa sahihi katika swali ambalo unalopaswa kulijibu ndomana ata katika mitaala ya elimu unapopewa mtihani na kuamua kujibu unaweza kupata au kukosa!

Inaaminika majibu sahihi au mazuri yanategemea sana ulimwengu wa utulivu, maana hapo panakutafakari maisha yatakayoendelea mara baada ya kutoa maamuzi au majibu katika jambo husika.

Kwani moja ya sifa ya majibu yatokanayo na hali ya utulivu ni majibu yaliyojaa usalama ndani yake na wala sio kisasi wala kukomoa.

Ni muhimu kutokukubali kusema kwakuwa watu wanakujaza upepo  wa kusema hama kuona nisiposema heshima yangu itashuka hama wazfa wangu utakosa nguvu.

Ni muhimu huo utulivu ubebwe na Mungu mwenyewe na wala sio akili zako, maana akili zako zinaangalia maslahi yako lakini Mungu anaangalia maslahi ya ufalme wake, kwakuwa kwa kiasi kikubwa maslahi yako yanawezaleta uharibifu katika ufalme wa Mungu lakini ufalme wa Mungu utaimarisha maisha yako.

Utulivu katika Mungu ni jambo jema sana na wala sio kitu cha kuzoelea bali ni kitu cha kuwa makini nacho ili kikurahisishie kufikia hatma yako, ni afadhali ukose vyote lakini uwe na utulivu wa kutosha na Mungu maana kupitia hali hiyo inakuwa rahisi kutembea katika mwelekeo na Mungu utakaokupa mwanga katika maisha yako.

Ni muhimu uhakikishe jibu lako linajenga ufalme wa Mungu na wala sio kustawisha nafasi/heshima  yako maana nafasi yako inakipindi tu cha muda fulani na wala sio cha milele ndomana wanasema “ cheo ni dhamana “.

Unahitaji kujua thamani uliyonayo mbele za Mungu ndio hiyohiyo aliyonayo mtu mwingine, hivyo tambua hakuna mwenye nafasi zaidi ya mwingine hivyo jibu lako lijengwe katika upendo wa kristo. ( mpende jirani yako kama nafsi yako ).

Unahitaji kuona kama Mungu anavyoona ili uweze jibu kama Mungu angelikuwepo angelijibu.

“ majibu yako ya leo ndio mstakabali wako wa kesho”
INAITWA SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey  Nelson…………………………………………………………………………….0764 018535