Ijumaa, 17 Julai 2020

NAFSI YANGU!




“ ukombozi wa nafsi ndio uhuru wa roho “

Nafsi ya mwanadamu inaweza kuwa katika hali mbili tofauti inaweza kuwa huru au utumwani na hali hizi utokana na kile kilichobebwa ndani ya nafsi.

Nafsi inapobeba mambo mengi yenye huzuni na mateso basi machozi ndio fungu lake.
Bora mtu afungwe jela miaka mia kuliko kuishi ndani ya kifungo cha nafsi.

Japo wako watu waliofungwa nafsi na hata kukosa dira nzuri ya maisha yake lakini akakuta ameyazoelea hayo maisha pasipo kujua yuko shimoni na anatakiwa kutoka na mbaya akili yake iliyotiwa giza akaona hayo ndio maisha aliyokusudiwa kuishi hii ni zaidi ya hatari.

Na pia nafsi inapokuwa kifungoni uwa magonjwa yanaweza kuwa fungu lako!

Nafsi ni nini?

-Ni hali kamili iliyondani ya mwili wa binadamu inayo mwezesha mtu kujitambua!
Hivyo huwezi kuigusa kama unavyogusa mwili wa binadamu japo hiyo nafsi ina umuhimu mkubwa kuliko mwili wa mtu husika.

Nafsi ni rahisi kugandamana na jambo linaloendelea katika maisha ya mtu husika linaweza kubeba kisirani/mauzi na mateso katika utendaji wa mtu husika.

Nafsi ni kama mtu asiyevaa nguo na pindi anapovaa nguo kama ni safi na size ikaendana na umbo lake basi bila shaka itatoa muoneka unaovutia kama si kupendeza sana na hapo huo muonekana ukaathiri katika maisha yake na hata kupelekea kuyafurahia maisha yake.

Lakini pindi nafsi ikiwa imevaa nguo chafu basi hapo uwezekano wa kujichukia ni mkubwa na kila tendo atakalofanyiwa liwe zuri au baya linaweza kuondoa thamani yako katika jamii, hali hiyo uwa fungu lake.

Na ni ukweli usiopingika uwezi kuwa na muonekano tofauti na nafsi yako ilivyo mathalani mtu aliyejeruhiwa katika nafsi yake ni wazi sura yake itaonyesha basi kama nafsi yako ilivyo ndivyo utakavyoonekana katika jamii husika.

Nafsi yako ikivaa ukatiri na ukaanza kutoa udhihirisho wake katika matendo basi hapo jamii itapata sura au namna ilivyo nafsi kupitia matendo ya ukatiri yanayotoka ndani yako.

Na ili nje uweze kupata badiliko la kweli  hilo badiliko ni muhimu ni lazima lianzie ndani ya nafsi yako ndo maana kuna uwezekano usio na mashaka ndani yake kama nafsi yako ikipona basi hapo kuyafurahia maisha ni swala lisilopingika.

Ukatiri wa simba haupo kwenye muonekano wan je bali upo ndani yake uliambata na asili yake na uwezi kuubadilisha kwa kukata manyoya yake.

Ni muhimu ujue unahitaji kuwa na nafsi iliyo na utoshelevu wa Mungu yaani kama vile kama anavyotaka au alivyoikusudia na sio kitu kingine mathalani kama jamii ilivyokutengeneza katika uharibifu wake au wewe mwenyewe ulivyoitengeneza tofauti na mpango wa Mungu.

Ni hatari sana kukutana mtu aliyejeruhiwa nafsi alafu hiyo nafsi ikashindwa kutawaliwa na akili yake kwa kuwa tendo atakalolifanya linaweza tikisa jamii nzima na kutoamini binadamu gani huyu aliyefanya tukio hili utoshangaa mtu huyo akila nyama ya mtu mchana kweupe bila uwoga!

Kufurahia maisha yako inategemea hali njema ya nafsi yako!

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni