Ni kawaida tu, kuwa kitu kinachoshawishi lazima kiwavute wengi kwake! kwa kuwa kinasifa ya kuvutia, “ PESA “ wengine wanasema ni jibu la maisha au heshima ya mtaa!
Tukiachana na PESA kwanza!
Neno USHAWISHI limekuwa ni msingi mkubwa katika dunia ya leo.
Kila bidhaa ni lazima iwe na ushawishi ili iweze kumvutia mhitaji ( mteja ).
Mtu anaweza kuwa na bidhaa nzuri sana lakini bado akafanya vitu vingi ili watu washawishike! Na watu wanafanya hivyo, ili kujaribu kuleta mvuto unaombatana na uelewa kwa watu pengine watampendezwa na kutokea kukipenda hatimaye kukinunua/kukichukia.
Na ni wazi ushawishi wowote usio na matokeo mazuri basi hali hiyo ya ushawishi uweza kukoma kabisa kama sio kupungua.
Ni kweli mahali popote penye ushawishi watu wengi ukimbilia hapo, japo hapo ukweli wakati mwingine ubora unaweza usiwepo.
Kwa kiasi kikubwa dunia ya sasa vitu vingi vinabebwa na ushawishi mathalani ili mtu akupende ni lazima umshawishi au aone sababu ya kukupenda hama atakapo kupenda nini atafaidika au kitaongezeka.
Na hii dhana imeingia hata upande wa ajira imepelekea ili mtu akupe kazi yake au akuajiri lazima umshawishi kuwa unaweza hiyo kazi na uko tayari kufanya hiyo kazi.
Na hata katika uwanja wa kukopa imekuwa ngumu ili mtu akukopeshe tu, ili mtu akukopeshe ni lazima umshawishi ili aone sababu ya kutoa pesa yake yaani umuhimu wa hitaji ulionalo, pia uhakika wa kurudi fedha yake pamoja riba yake.
Ushawishi umekuwa ni msingi wa mambo mengi kwenda pasipo kujali huko yanapokupeleka kuna usalama au la!
Wako watu walio hatarisha afya zao na hata maisha yao ili kutaka kumshawishi mtu akubali kufanya jambo fulani lenye maslahi kwake mathalani wako watu walikubali kufanya ngono na mabosi wao ili kupata ajira hama kupata nafasi za juu.
Ni kweli usiopingika ushawishi unaweza kuzaliwa katika muonekano wa nje au nguvu inayozaliwa ndani yako.
Ni muhimu utambue ushawishi ulioambatana na muonekano uwa unakuwa na mwisho lakini ushawishi unaotoka ndani yako uwa hauna kikomo ni kama bahari isivyo kuwa na mwanzo wala mwisho.
Kila ushawishi unaambatana/unaendana na matokeo pamoja na majira, pia ukijiona umefika ujue wapo waliofika kabla yako.
Kuwa na muonekano unaovutia ni kitu kizuri sana lakini kitu pekee kitachoweza wavutia watu na Mungu pia ni pale utakapo jali UTU WA MTU.
Muonekano wako usikupumbaze kuona watu vile watu wanakusifia ukafikiri mbinguni wanakupigia makofi namna ulivyovaa au namna unavyotabasamu.
Tambua Mungu ndiye ametia hiyo akili katika kichwa ( ubunifu ) ila akumaanisha ukishajiona umetokeleza duniani basi ujione umetokelezea hadi mbinguni.
Katika yote lazima utambue wewe ni asili ya Mungu na Mungu kwa thamani mtu aliutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
“ unapokunywa chai ya maziwa usione wajinga wanaokunywa chai ya rangi”
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………………….0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni