Miwani kama kifaa kinachowekwa machoni ili kutoa usaidizi wa macho ili kuweza kuona vizuri, na inawezekana ukavaa miwani kwa kupenda au kutopenda na kwa asilimia kubwa wanaovaa miwani uwa wanakuwa na matatizo ya nguvu katika kuona,
Japo matatizo ya macho yamegawanyika katika sehemu kuu mbili:
i. Kushindwa kuona mbali
ii. Kushindwa kuona karibu
Pamoja na matatizo hayo lakini chanzo chake kinaweza kutofautiana mtu na mtu, wako waliopata na matatizo ya macho kwa kurithi, vyakula, mtindo wa maisha na wako waliokuwa wanavaa miwani kama kutafuta muonekano mzuri pasipo kujua hiyo miwani ni tiba kwa mgonjwa wa macho waka kuta wanakumbwa na matatizo ya macho.
Pia wako watu wanamatatizo ya macho wamefikia hatua ya kuvaa ya miwani lakini awavai ( kutopendelea ) au uvaa kwa tukio maalum au majira fulani tu.
Vilevile wako watu wasio na matatizo ya macho lakini upendelea kuvaa miwani inawezekana katika kutengeneza muonekano wa kuvutia zaidi.
Karibu!
Ningependelea kuangalia miwani katika uwanda wa uhuru wa kuvaa au kutovaa,
Ni kweli unaweza vaa miwani pengine pasipo kujua hiyo miwani ni tiba ya macho, lakini wewe ukaamua kuvaa ili mradi uimarisha umaridadi pasipo kujua kwa kuendelea kuvaa miwani kutapelekea kuathirika kwa macho yako.
Sio vizuri kuona rafiki yako anavaa miwani basi ukaona na wewe uingie mkondo huu wa kuvaa miwani pasipo kujua kwanini rafiki yako anavaa miwani.
Kuna vingine vya leo vinaathari kubwa kesho.
Unapoishi katika jamii unapata kujua/kuona mienendo mbalimbali inayoendelea katika jamii,sio uone mtu anavaa nguo za gharama, anakaa katika makazi mazuri hama anaendesha magari ya kifahari, ukasema maisha ndio haya pasipo kujua gharama katika kupata na kutunza.
Na pengine unaweza usijue uharibifu gani unakula nafsi yake chinichini,
Sio kila unachokiona unataka kukichukua ( kuvaa miwani ) kumbe unaweza kukiacha na bado ukawa salama sana.
Ni kweli unaweza uvae ukisasa lakini angalia yasije yakakupata ya kisasa! Au ukapoteza maana katika wengi maana kila nafsi itapata maumivu yake.
Ni vizuri kutembea katika njia ambayo inakupa mwanga kuliko kung’ang’ania njia ukijua unamfurahisha mtu uku unajua unaangamia wewe binafsi.
Using’ang’ania miwani ambayo ina umiza macho yako hata kama maumivu sio makali hata kama watu watakusifia sana au kukuona umekuwa wa kisasa ni bora uache au rudi kwa daktari akuibadilishie akupe itakayo kufaa.
Usipende kufuata kila upepo unapoenda/ usipende upepo maadam unakupuliza maana kuna upepo mwingine unaongeza joto na sio ubaridi.
Kumbuka tunaishi mara moja hapa duniani ipende nafsi yako ishi katika ustawi wako na itunze nafsi yako.
Ni vizuri na ni muhimu kumuheshimu mtu aliye kuzidi umri,elimu, hekima n.k lakini sio kila neno anenalo mtu huyu ukalichukua ( ukalivaa ) lipe nafasi kujua je! Hilo neno au ushauri nafsi yako itakuwa salama.
INAITWA SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………….……………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni