Na moja ya kitu kinacholeta furaha kwa mtu ni pale anapotambua ANASIKILIZWA hapo ndipo kiu inaweza kukatika bila maji, njaa inaweza poteza nguvu yake bila ya chakula.
Endapo utafanikiwa kujua namna ya kumsikiliza Mungu nawe ukawa mwaminifu kumsikiliza, basi hapo utauteka moyo wake! Utaupendeza moyo wake.
Japo kuna vitu vinataka kusikilizwa na wewe na vinajiona vinasababu ya kusikilizwa na wewe! Hivyo unahitaji kujidhatiti katika kuitumikia sauti ya Mungu.
Kuna vitu vingine ukivipa sikio lako unaweza usitoke salama lakini sio kutoa moyo wako katika kusikia sauti ya Mungu ni hakika utakuwa salama milele.
Ukitaka kuifikia hatma ya wanadamu basi endelea kuwapa sikio lako ila endapo ukitaka kuifikia hatma ya Mungu juu ya maisha yako basi mpe sikio lako lote! Uchaguzi ni wako.
Ukweli katika uwanja wa kusikiliza unavipingamizi vingi: kujisikiliza, kuisikiliza dunia na kumsikiliza Mungu.
Kumsikiliza Mungu kwa njia nyingine tunaweza sema ni kupata ustawi unaotokana na Mungu kwa namna yake unaozaliwa ndani ya sauti yake.
Kiukweli Mungu kwako ahitaji vitu vingine maana vyote ni vyake na akihitaji anavipata bali kitu anachokitaka kutoka kwa ni kuona moyo wako unamsikiliza yeye.
Kama kweli unataka kuwa kipenzi cha Mungu basi jifunze sana namna ya kumsikiliza.
“ mtu atayekayefanya mapenzi yangu” Matendo 13:22
Yohana 4:34 Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.
“ chakula changu ndicho hichi ni yatende nikamalize”
Unaweza ukatembea na manabii na ukaishi kwenye sauti zao lakini unaweza usiwe nabii lakini uwezi kutembea kwenye sauti ya Mungu usipate maatamio ya kiMungu.
Na muhimu utambue Mungu anaifurahia dunia kwa uwepo wako na uwepo wako unakuwa na thamani zaidi kwakuwa unaishi katika sauti ya Mungu.
Moja ya kitu kitakachoweza fanya ili watu waweze kukusikiliza ni muhimu sana ujifunze kumsikiliza Mungu ili yeye akuanganishe na watu wako.
Kuna wakati mwingine unakuwa katika hali ngumu unaweza tamani hata kusikia neno la mtu ili liweze kuchangamsha moyo wako angalau upate faraja kwa kipindi lakini hapo ujue unahitaji kuisikia sauti ya Mungu ili ikupe mwelekeo wa kutoka hapo ulipo.
Naam moja ya sauti isiyochosha kusikia wala kukinai ni kusikia sauti ya Mungu maana kila wakati usikiapo katika masikioni inakupa uwanja mwingine wa ushindi.
Nani vizuri utambue ushindi wa Mungu katika maisha yako unazaliwa ni baada ya kusikia sauti yake hapo neema ya uwezesho uachiliwa katika kufanikisha jambo husika.
Na ishara ya kumpenda Mungu uwa inaoneka au dhihirika pale utakapo amua kumsikia.
Na Mungu anataka apate uhakika wa kuwa utasikia kisha achilie Baraka zake kwako!
“ msikilize akusikilize”
INAITWA SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson…………………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni