Ijumaa, 30 Desemba 2022

UKO KATIKA MIKONO YA NANI?

 



Kuna wakati unaweza kumlaumu Mungu kama sio majira ya dunia kwakuwa umekosa wa kumlaumu!

Mathalani katika majira ya mvua yanapofika kutokana na maeneo unayoyaishi maji yanakuwa ni kikwazo kwako hivyo japo unaipenda mvua lakini ukifikiri mazingira yako na mateso unayoyapata unakuwa katika wakati mgumu hivyo wakati watu wanaomba mvua inyeshe wewe unafikiri adhabu utakayoipata baada ya mvua kunyesha,

Lakini kwa mtu yule ambaye anaishi mahali ambapo mvua inyeshe kwa namna yoyote yeye anakuwa katika mikono salama kama sio sehemu salama maana kwake huyo pindi watu wanapo omba mvua inyeshe yeye atakuwa anamshukuru Mungu kwakuwa anajua joto litapungua!

Asante……………………………………karibu sana!

Naam mambo mazuri yanakupata yasikupumbaze na wala mambo mabaya yanapokupata yasikufanye kuwa mnyonge.

Usione watu wengi wanacheka basi nawe ukajiunga nao ukafikiri wanapenda kucheka na pindi unapowaona watu wanalia usifikiri wana huzuni ukawapa pole wakati mwingine kile kinachoonekana kinaweza kisiwe uhalisia uliopo.

Uwa mtu mwenye akili afurahi tu kuwa ana nyumba nzuri bali ni pale atapoona misingi ya hiyo nyumba nzuri itamfanya awe salama na endelevu kwakua  hiyo misingi inafanya hiyo nyumba idumu katika mazingira yoyote.

Naam kuna kipindi katika maisha ya mwanadamu unaweza pitia maisha yatakayo fanya moyo wako kuwa chini napengine ata kujuta kwanini umezaliwa duniani, kwa kifupi hali hiyo inapelekea radha ya kuishi hapa dunia inapotea kabisa, pasipo kujua katika siku kuna mchana na usiku na bora zaidi ni kujua namna ya kuishi mchana ni tofauti kabisa na kuishi usiku na kikubwa ni kujua huko katika bustani gani na ni bustani yenye ubichi au yenye ukame?

Mathalani maisha yanayo fanana na nyasi nayapenda sana maana pindi upepo mkali unapovuma zinalala na baada ya kitambo kidogo baada ya upepo kukata hizo nyasi zinarudi kama awali na maisha yake yanaendelea mpaka kikomo chake.

Pia napenda sana maisha ya mlinzi hasa wa usiku anapokuwa lindoni akivumilia baridi kali nap engine hata mbu wakimuuma lakini uku akiacha familia nyumbani kwake wakiwa wameshakula na kupumzika japokuwa yeye anakabiliana na usiku akijua asubuhi itakuja na hili baridi au mbu wakali atawasahau.

Mbali na hiyo mifano pia napenda maisha ya mkulima pindi anapoamua kupanda mbegu zake hata kama hana akiba ya kutosha na anaweza kupitia kipindi kigumu akiwa anasubiri mavuno yake; anajua njaa haitadumu katika maisha ya familia yake bali anajua muda si mrefu kitakuwepo chakula cha kutosha katika maisha yake.

Yesu alisema “ roho yangu naiweka mikononi mwako”

Akiamini na kujua kwamba  katika mikononi mwa Mungu uhai wake utafichwa naam maisha yataendelea na ushindi utapatikana.

Hayo maneno aliyasema ikiwa analikamilisha kusudi lake la kuja duniani katika kuleta ukombozi wa wanadamu.

Na ni kweli maisha yameratibishwa katika ramani ya Mungu lakini bado ni uchaguzi wako kuyaweka hayo maisha mikononi mwa Mungu au sehemu nyingine ambayo wewe binafsi utaona inafaa kwako.

Ni kweli unauchaguzi wa wapi uyaweke maisha yako lakini hauna uchaguzi kuyakataa matokeo ya uchaguzi ulioufanya ni kama vile mwanafunzi asiposoma akifeli atashangaa labda awe “ hamnazo “

Usifurahi kwa sababu unakula hama unapata unachokitaka pasipo kujali maisha yako yamebebwa na mikono ya nani? Hii ni hatari sana.

Kwani wako watu walifurahi kuwa na vitu baadae wakalia pale vitu vilipoondoka hama kuanza kuwatesa!

Ni vizuri maisha yako uyaweke katika mikono salama  ( Mungu ) ni sawa na kupanda mti katika chemichemi isiyokauka jua liwake liwakavyo bado utaendelea kuyafurahia maisha yako na Mungu siku zote.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………….…………..0764 018535

 

Ijumaa, 16 Desemba 2022

UJACHELEWA,



Kuna wakati macho yetu na maneno ya watu yanaweza kutudanganya na kuona tumechelewa kumbe sio hivyo!

Na moja ya kitu kinachoweza kutufanya kuona tumechelewa au tunachelewa ni matarajio tuliyonayo kwa jambo husika kukawia,

Naam mathalani mnawezafanya kazi kwa miaka 10 lakini ukijilinganisha na wafanya kazi wenzako japo inawezekana mnalipwa kiasi sawa lakini unaweza kuona kuwa wamekuacha mbali sana na hali hiyo ikapelekea kujiona mnyonge kama sio mpweke nakujiona kama ndege mtoto aliyekosa kumbatio la mama yake wakati analihitaji ukabaki kujilaumu na kutafuta dhambi yako.

Wakati mwingi matarajio yetu yanakuwa ndio kifungo chetu hasa yanayo ambatana na tamaa zetu binafsi mathalani unaweza kuwa katika mahusiano ukawa na furaha nyingi na hata ukaweka matarajio kuwa Mungu akipenda kipindi kijacho nitaanzisha familia yangu, lakini unaweza kukuta mwenza wako hayuko tayari au kuna mambo hayajakuwa sawa wakati mwingine hali hii inapozidi unaweza kujikuta unavunja mahusiano matukio haya yakijirudia unaweza kujihisi kuwa unanuksi kama sio mikosi hama wewe ni fungo la kukosa.

Siku zote kila matarajio uwa yanabebwa na mfumo fulani inawezekana unajua au ujui  unaweza kuwa ni mfumo wa mbingu au duniani na wala sio matarajio yetu tu, hivyo ukishindwa kuelewa  mfumo unaotawala jambo lako  ni wazi mtapishana na matokeo au yale unayoyatarajia.

Unaweza kuona uhitaji wako unachelewa maana kila jambo lina maandalizi yake, endapo usipo jua kiwango cha maandalizi yake unaweza kutaka jambo lisilo la wakati huo na mwisho likakutesa badala la kulifurahia.

Naam inawezekana ukawa na sifa zote za kupata hilo jambo na kila mtu akakupa matumaini yote lakini ukiwa nje ya mfumo unaweza kukuta nafasi hiyo sio yako.

Jifunze kutazama mambo kwa jicho la Mungu wakati mwingine unaweza kuwa na sifa za dunia lakini ukawa hunasifa za mbingu hivyo ukakosa hiyo nafasi kutokana na mtazamo wako na wa Mungu kupishana.

Kwa asilimia kubwa watu wengi pale walipo sasa awakutegemea kuwa hapo lakini wakajikuta wako hapo na pengine yamezidi matarajio yao.

Hivyo tukubaliane kuwa sio kila matarajio uliyonayo ukafikiri kuwa ni sahihi na kutojua labda kuna makubwa zaidi unayo weza kuyafikia.

Pia mbali na hapo kikubwa sio kuwa na matarajio tu bali ni kuwa nyezo ya kukusaidia kukamilisha hayo matarajio na moja wapo ni afya njema itakayo kuwezesha kukamilisha ndoto yako maana nje ya afya njema kuna magonjwa yanawezapelekea kupoteza uhai na matarajio yako yakakoma hapo.

Kikubwa usikate tamaa wala usitoe nafasi ya kumlaumu mtu maana asili ya ubinadamu ni ubinafsi kila kitu kizuri mtu upenda  kianze naye lakini Mungu ndiye msimamizi wa kweli atakupa kile unachopaswa kupewa kwa majira yake.

Usishikilie matarajio uliyonayo tu kana kwamba bila hayo uwezi kuishi, kuna kipindi matarajio yako yanawezapishana na mawazo ya Mungu, hivyo Mungu anapoanza kulidhihirisha kusudi lake hautakiwi kupingana naye maana yeye anakujua vizuri kuliko wewe unavyojijua  na yeye ndio hitimisho la maisha yako.

Hivyo usiwe mnyonge pindi unapohisi kuwa matarajio yako yanachelewa ila elewa mfumo ulioambatana na matarajio yako wala hauna haja ya kukata tamaa

“ uhai ni bora kuliko matarajio yako”

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson………………………………………………………………….0764 018535

 

 

Ijumaa, 2 Desemba 2022

SAHAU, ATAKUKUMBUSHA;



Usipende kutumia nguvu nyingi katika kupata kitu ambacho yeye Mungu anajua unahitaji hicho kitu.

Ø  SAHAU, ATAKUKUMBUSHA ( omba, utapewa )

Mathayo 7:7 Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;

Wakati mwingi tunapoenda mbele za Mungu tunapenda atuelewe vile tunavyojielewa ili aweze kutupa haja/ yale matakwa tunayotaka sio mbaya lakini sio ukamilifu wa kupata haja yako.

Unahitaji kujua kuwa Mungu ni Mungu wa kanuni na anafanya mambo katika mawanda ya utaratibu wake sawa na uradhi wa mapenzi yake.

Mungu ahitaji umwelekeze sana ili ajue kweli unahaja na hilo jambo bali anahitaji moyo wako ujimimine kwa bwana ukieleza sifa zake katika maisha yako.

Mikakati tunayojiwekea katika mambo mbalimbali katika maisha yetu ili kufanikisha/kukamilisha malengo yetu ndivyo wakati mwingine yanakuwa kongwa au kikwazo kikubwa cha kumuona Mungu, mathalani mtu anahitaji kazi hivyo anaandaa mikakati yake ya kumshawishi bosi ili apate hiyo ajira/kazi wakati mwingine hata kutoa rushwa/kuonga ili mradi tu afanikishe lengo lake kupata kazi.

Ahuhitaji jitihada zako nyingi ili kumuonyesha Mungu kuwa wewe ni mwihitaji bali hali ya moyo wako inaongea vizuri mbele za Mungu naye anajua kuwa wewe kweli ni mwihitaji au sio mwihitaji au tamaa zako.

Karibu katika somo!

SAHAU, ATAKUKUMBUSHA…………………………………………………….

Unapoomba jambo usipende kulitafiti kwa akili zako na kulikamia bali amini limeshafanyika fanya shughuli zingine, “ tukiomba yeye atasikia “

1 yohana 5:14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia

Unapoomba jambo alafu ukalitazama kama lilivyo wakati mwingine kukata tamaa, mathalani unapomuombea mtu mwenye tatizo la tumbo alafu ghafla tumbo likazidi hatimaye mtu akapoteza fahamu hali hiyo inapotokea  na kama hauna mwingiliano (network) nzuri katika ulimwengu wa roho unaweza kutafuta njia na kusepa! ( imani yako kwa Mungu inapotea ).

Naam kuliamini jambo litakalotokea sio lazima ulikazie sana macho bali ni hali moyo wako kukubaliana na kile ulichokisema.

Yesu alisema “ mti uliokosa matunda akaulaani usitoe matunda tena”

Mathayo 21:19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. Mtini ukanyauka mara.

Yesu akuukazia sana ule mti ili kuhakikisha unakauka palepale bali aliposema akaondoka kesho alipopita akushangaa kuona mti umekauka baada ya wanafunzi kumwambia ila wanafunzi walishangaa sana.

Wakati mwingine unapoenda kwa Mungu katika uhitaji wako lazima akili yako iwe kwa Mungu na wala sio kwa watu unaona kuwa wanaweza kutatua shida yako ndo mana kuna neno linasema SAHAU.

Maana Mungu anajua haja yako hata kabla ujafungua kinywa chako kumuomba tayari ameshakupa ni wewe kujua namna gani ya kukichukua  na ni wakati gani?

“ mkiomba amini yameshakuwa nayo yatakuwa yako”

Yohana 14:13 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.

Ukisha mletea Mungu au kumuomba kisha ukaamini katika kile ulichomuomba pasipo shaka yoyote hiyo hali inamfanya Mungu ashughulikie hilo jambo lako kwakuwa kwake hicho ni kigezo kikubwa kuwa una mwamini na unamtegemea na hauna mbadala wowote ila ni yeye tu.

Mungu anapotaka kufanya jambo ahitaji akili yako imwelewe sana bali anataka kuishangaza akili yako ili uzidi kumwamini.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………………..0764 018535

 

Ijumaa, 18 Novemba 2022

KUMTEGEMEA MUNGU

 



Haya maisha ya kumtegemea Mungu na yafananisha na maisha ya mtu aliye kipofu anayetembea usiku pasipo usaidizi wa mtu ila anakuwa ana matumaini kuwa safari yake anayoiendea atafika hata ikitokea amejikwaa mara zote lakini ana amini kufika kupo tu!

Ni rahisi kusema au kujishuhudia kuwa unamtegemea Mungu lakini ni kitu kingine Mungu mwenyewe kukushuhudia kuwa unamtegemea.

Naam ni fahari ya mzazi kuona watoto waliochini ya uangalizi wake wanamtegemea yeye! Na sio jirani zake.

Hivyo linakuwa ni jukumu lake kuhakikisha hao watoto wako salama na wanafurahia maisha yao hasa katika uwepo wake.

Katika kumtegemea Mungu uwa hatusemi kuwa sisi tunamtegemea Mungu! basi inatosha, bali zaidi sana maisha yenyewe yanajieleza kuwa yanamtegemea Mungu au la!

Kumtegemea Mungu ni siri iliyojificha ndani ya mtu binafsi na sio kitendo cha kujivika majukumu ili uonekani kwamba uko kanisani na unamtegemea Mungu.

Kumtegemea Mungu ni kuishi au kutembea na moyo wa Mungu, unatembea uku ukisababisha shangwe katika moyo wa Mungu.

Mtu anapoishi maisha ya kumtegemea Mungu hayo ndio maisha yanaitwa maisha ya uchaji/ moyo wa ibada.

Hakuna jambo utakalo lifanya mbele za Mungu naye Mungu akakufurahia nje ya maisha ya kumtegemea yeye pasipo kujali watu wanasisimka kwa kiasi gani hama changamko lao.

Kabla ujazama katika kutumika zaidi ni vizuri ujikite sana kumtegemea Mungu maana swala hili limekuwa ni mtihani mkubwa, mtu anakuwa bora zaidi kutumika katika vipawa kuliko kukua na kuzidi katika kumtegemea Mungu pasipo kujua kutumika pasipo kudumu katika kumtegemea Mungu inakuwa sawa na nahodha wa meli anayeendesha kwa bidii uku akikosa dira sahihi ya kule anakoelekea.

Kama ikatokea fursa ya kusoma na ukawa na masomo mengi mathalani kujifunza kuimba , kuponya wagonjwa, kuubiri hata kutoa unabii na likawepo pia somo la kumtegemea Mungu basi mimi ningekushauri acha kwanza masomo yote na ujikite katika kujifunza kwanza kumtegemea Mungu na ndivyo masomo yote yatakuwa mepesi na hata kuwezekana.

Unapotaka kumuona mtu mwenye nguvu za rohoni na mwenye akili kubwa ni mtu anayemtegemea Mungu wakatiwengine watu wanataka upite huku ili wakupate lakini watashangaa umepita njiia wasioijua na kufika mahali ambapo awakutegemea utafika na kuketi pale wasipo penda.

Mtu anayemtegemea Mungu uwa anaona mahali ambapo wengine hawaoni na anatembea mahali ambapo watu kwa kawaida wa akili za kinadamu awezi kutembea hapo naam anakaa mahali kwa akili timamu hauwezi kukaa hapo.

Ø  Danielkatika tundu la samba

Daniel 6:23 Basi mfalme akafurahi sana, akaamuru wamtoe Danieli katika lile tundu. Ndipo Danieli akatolewa katika lile tundu, wala dhara lo lote halikuonekana mwilini mwake, kwa sababu alikuwa anamtumaini Mungu wake.

Daniel 6:24 Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki Danieli, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na wale simba wakawashinda wakaivunja mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika chini ya tundu.

Ø  Shedrack, Meshack na Abenego katika tanuru la moto

Daniel 3:19 Ndipo Nebukadreza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraka, na Meshaki, na Abednego, basi akatoa amri watie moto ile tanuru mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto..

Daniel 3:26 Kisha Nebukadreza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. Akanena, akasema, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye juu, tokeni, mje huku. Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakatoka katika ule moto

Ukifanikiwa kujua namna ya kumtegemea Mungu kuna maisha hauwezi kupitia  mathalani maisha ya kukata tama, kuwa na chuki, kisirani na hata magomvi kwakuwa uyaweka maisha yake ndani yako.

Kwakuwa mtu anayemtegemea Mungu uwa kila jambo linalotokea katika maisha yake yeye anamuona Mungu tu haoni kingine kwa kuwa anajua jambo ambalo lililoanzishwa na Mungu yeye atalikamilisha kwa wakati wake hivyo furaha kwake ni kama pumzi katika maisha yake siku zote.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………………..0764 018535