Ijumaa, 10 Juni 2022

USILIE! ANAJIVUNIA WEWE

 



 

Ni kawaida ya binadamu kuwa kila jambo analolifanya uwa nyuma yake linakuwa na sababu yake, pindi unapomuona mtu anacheka uwa anakuwa na sababu ya kucheka vilevile pindi unapomuona mtu analia uwa anakuwa na sababu ya kulia japo sio lazima uelewe kama anavyoelewa yeye maana ni kama maumivu ayapatayo mtu anayetumbuliwa jipu na sio anayetumbua jipu.

Unaweza kukuta mtu analia na ikatokea ukajua sababu yake ya kulia, pindi unapojua \unaweza kushindwa kujua uzito wa kumpeleka mtu kuwa katika hali hiyo lakini ukweli moyo ni kificho, maumivu ya mtu anayajua mtu mwenyewe na zaidi sana kile unachokiona ni sehemu ndogo katika kile kinachomfanya alie.

Japo linapotokea unaweza usijue kwanini limetokea, muda mwingi tunaona kama uonevu na wala sio majigambo ya Mungu katika uwanda wake!

Muda mwingine inakuwa ni maamuzi yaliyofanyika katika ulimwengu wa roho ila matokeo yanaonekana katika ulimwengu wa mwili.

Ni muhimu unapopita katika kipindi kigumu ni sawa na mwanafunzi akiwa katika chumba cha mtihani jicho la msimamizi likiwa juu yake………ni zaidi pindi unapopita katika kipindi kigumu uwa mbingu inatulia kukuangalia kuona misuli yako ya rohoni kiwango chako! Ni sawa bondia aliye ulingoni wakati anaendelea na pambano anaweza sema sasa naweza/ninasababu  ya kuinua mikono lakini zinaweza kuja nguvu akiwa katika maumivu ya mwili na akipata fursa na hatimaye akatangazwa kuwa ni bingwa.

Wakati Mungu anajivunia wewe ni wazi maumivu yanaweza kuandamana na wewe!

“ Tazama mwanakondoo azichukue dhambi za ulimwengu”

Ni maneno mazuri lakini yaliyobeba dimbwi la mateso ili liweze kutimia ni lazima jasho la damu liwe limeshatoka.

Ili Mungu aendelee kujivunia ni muhimu tu, uweze kuruhusu afanye apendavyo na sio utakavyo yaani na uwe wewe kwa uhalisia wako, na sio mtu anaishi katika maisha ya wengine bali ishi katika wewe ( ishi maisha yako).

Watu wengi wanapopita katika kipindi kigumu uwa awapendi kuonyesha wanapitia kipindi hicho hivyo kuishi sio maisha yao(japo sio muhimu watu wajue kuliko Mungu anavyopaswa kujua), kucheka wakati ndani analia, kwani kipindi hiki watu wengi awapendi wajue yale wanayo yapitia watu wasije wakawadharau katika hali hiyo utazidisha kipindi kigumu kiwe zaidi kuliko kinavyotakiwa ni sawa na mwanafunzi anapofanya mtihani na kushindwa/kupata matokeo sio mazuri itamlazimu arudie  huo mtihani mpaka atakapo faulu au amue kuacha shule.

Ni muhimu kukubali watu wakuone vile ulivyo ili neema inapokujilia wajue sasa Mungu amekuinua na wala sio jitihada zako.

Hivyo unapokuwa chini wacha ieleweke hivyo labda Mungu mwenyewe aamue kukufunika tu lakini sio wewe ujifunike.

Na pia ni muhimu utambue kila kipindi ambacho unapitia kina maana kubwa katika ustawi wako pia lipo kusudi jema ambalo Mungu analo katika hilo, hivyo ondoa mashaka.

Na utambue kuwa ni Mungu pekee mwenye uchungu wa kweli kuliko mtu/kitu chochote katika maisha yako hivyo anavyoruhusu haya yaje kwako hana lengo la kukuweka katika hatari ambayo haina utatuzi wa kukutoa hapo salama kama aliweza kukutunza tumboni mwa mama yako japo kipindi hicho mimba nyingi ziliharibika lakini wewe ulikuwa salama maana hakuna mtu mwingine awezaye kukutunza unapokuwa tumboni hivyo awezi kushindwa kukutunza sasa.

Uwa wazo jema la Mungu kwa mtu wake aliwezi badilika ila mtu husika anaweza badilika lakini sio ahadi ya Mungu. AKISEMA ANAISIMAMIA MWENYEWE!

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………..……0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni