Ijumaa, 21 Oktoba 2022

NDANI YA UWEPO WAKE!

 



Kila kitu  kinakuwa ni rahisi kukipata endapo ukijua kinapatikana wapi na namna ya kukipata! Endapo utakosea wapi pa kuvipata ni ngumu kuvipata, mathalani mtu mwenye akili akihitaji kumuona mamba awezi kwenda baharini na kutegemea kumuona mamba maana mamba apatikani baharini.

Pia unaweza kuta hiyo bidhaa inapatikana maeneo yanafanana lakini unaweza kukuta wote wanaweza kuuza bidhaa moja lakini inaweza kutofautiana katika ubora na hata baadhi ya bidhaa ikajulikana ni original na fake, hivyo dhana ya kupatikana pekee yake sio jibu kamili bali ubora wa hiyo bidha inaweza kuchochea katika kukamilisha maana ya upatikanaji wake maana inakuwa na tija katika matumizi yake hata kwa upande wa afya.

Karibu katika somo;

Ndani ya uwepo wa Mungu uwa kuna vitu vinazaliwa hapo:

Ø  Ushindi unatokana na uwepo wake

Ø  Nguvu inayotokana katika uwepo wake

Ø  Amani inayotokana na uwepo wake.

Ø  Ujasiri unatokana na uwepo wake

Naam yako machipuo yanatokana ndani ya uwepo wa Mungu, japo yako machipuo yanayotokana nje ya uwepo wa Mungu kufanana au hata kupelekea kutojua utofauti wake.

Ni kweli kuna uwezekano wa kuzaliwa kwa ujasiri ulio nje ya uwepo wa Mungu lakini ukweli ujasiri wowote ulio nje ya uwepo wake sio wa kudumu na ndani yake furaha ya kweli inakuwa haipo.

Unaweza kukuta mtu anajenga nyumba ya kifahari sana hama kupata kazi ambayo wewe binafsi ukiisikia unaweza kutetemeka na hata kushindwa kuamini lakini pindi hivyo vitu vikizaliwa nje ya uwepo wa Mungu bila shaka ukamilifu wa furaha ya kweli hautakuwepo.

Kwa asilimia kubwa watu wengi wanapenda kuwa na vitu vitakavyowapa furaha hata pasipo kujali hivyo vitu nitavipata nikiwa ndani ya uwepo wa Mungu au nje ya uwepo wake bali yeye furaha yake ni kuvipata tu.

Vitu vingine utakavyo vipata nje ya uwepo wa Mungu muda mwingi vinaweza visiambatane na njia iliyo sawa/sahihi hivyo ujasiri na kujiamini sio uhakika sana.

Kuwa na vitu vyenye viwango vya juu ( standard ) kwa mtu aliye ndani ya Mungu ni haki yako na wala sio vinyonge na vizuri ujue kuwa Mungu ni kama baba mwenye busara hata akiwa anamiliki/utajiri kiasi gani hata kuwa na fahari nyingi nyumba na magari ya kutosha hawezi  kumpa mtoto wake ambaye akili yake haijakomaa kumiliki nyumba akampa akae peke yake hata kama anampenda kiasi gani; kwakuwa anajua hapo sio kumsaidia bali kumwangamiza.

Ni kweli ndani ya uwepo wake viko vitu vyenye viwango: mathalani mfalme Daudi alikuwa analalia kitanda kilicho na dhahabu tupu; ila kikubwa lazima ujue akupi ufanya tambo katika jamii yako bali watu wamuone Mungu kupitia maisha yako.

Uwepo wake unatoa vyake endapo utaamua kutulia na kusubiri utoe matunda yake yatakayo dumu siku zote.

Naam kama kweli wewe ni mkristo na unatambua nafasi ya Mungu basi hakikisha unakuwa ndani ya uwepo wake ili naye akupe hazina yake.

“ uso wangu utaenda pamoja nawe nami nitakupa raha “

kutoka 33:14 Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.

Ni kusudi la Mungu endapo utakubali kuishi katika maongozi yake atakupa raha yake, yeye awezi kuviachilia vitu anajua vitaleta uharibifu katika maisha yako.

Tunajua thamani katika dunia ya leo inapimwa kile unachokimiliki, hivyo kiwango cha mali unazo miliki ndivyo thamani utakayopata kutokana watu walioibeba dunia hivyo itakavyokuwa humiliki mali yoyote basi usitegemee heshima yoyote.

Ni kweli kila mtu anatakiwa aheshimike lakini uwezi kulazimisha watu wakuheshimu na pia usilazimishe kuwa na mali ili upate heshima inayozaliwa na mali na heshima ya mali haina nguvu sana kama kumuheshimu mtu katika UTU, kwakuwa mali zinaweza kuja na kupotea.

Usipende kufanana na maisha ya wengi kuwa thamani yao ubebwa na vitu wanavyoviona anafahari nyingi bali muheshimu na kumthamini vile alivyo lakini sio kutokana na mali zake.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………………..…….0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni