Ijumaa, 29 Desemba 2023

UKISASA UNA GHARAMA



Wanasema kizuri kina gharama au kina gharamikiwa!

Inasemekana ukisasa ni mzuri na sikatai ila unagharama yake.

Kwenda na wakati ni jambo jema sana kwakuwa lina mazuri yake mengi lakini vilevile usipouelewa vizuri unaweza kufanyika kuwa teso kwako hata ukawa mtumwa wake badala wewe kufaidika nao.

Mabadiliko katika mambo mengi uwa ni jambo la heri, kwa maana kwa kiasi kikubwa mabadiliko mengi uchochea maendeleo kwa jamii au taifa kwa ujumla wake.

Tatizo linakuja katika jamii tuliyo nayo, ni jamii kubwa imekuwa ikiteseka sana na ukisasa tulionao kuliko kufaidika nao watu upenda kujaribu kila kitu hatimaye kupelekea matatizo mengi; katika upande wa afya, watu wamekuwa wakitengeneza miili yao au kutumia vitu hata kwa namna ambayo haiongezi tija kwao zaidi ya matokeo yake kudhoofisha afya zao mathalani watu wengine uona fahari kuvuta sigara muda wote lakini mwisho wake uweza kusababisha kansa ya mapafu na magonjwa mengine mengi.

Naam watu wengine wametumia ukisasa katika kuharibu jamii badala ya kuwa saidia: mathalani sasa tunaongezeko la mashoga, watu kujiunga na makundi mabaya ( kigaidi, ujangiri n,k), watu kutekwa hasa watoto na wanawake.

Ukisasa umetoa njia rahisi ya kuwafikia watu hao na kufanikisha matendo yasiyofaa kufanyika katika jamii zao.

Na watu wengi kuingia uingia katika ulimbukeni katika mitandao na kukuta wanatumia muda mwingi katika mitandao kuliko shughuli zao au watu wawapendao/wanaowategemea familia na watu wengine.

Viko vitu vingi vipya vinavyotambulishwa katika ulimwengu wa sasa kila siku baadhi yao vikiwa na lengo la kuwa na msaada katika jamii husika ziko dawa zimekuwa zikisemekana zina nguvu ya kuongeza nguvu ya kiume na kwasasa soko lake limekuwa kubwa pia yako madawa mengine yanasemekana yanaweza kupunguza unene/matumbo, miguu na hata maziwa kuwa makubwa na hivyo jamii imejiingiza katika maisha hayo wakiamini ukisasa unalipa,

Na hali hiyo kupelekea kuharibiwa zaidi kuliko kusaidika! Wakati mwingine mtu anagundua kuwa alikosea akiwa katika madhara makubwa, na wakati mwingine inakuwa ni ngumu kutoka hapo.

Na kutokana na ulimbukeni wa wengi imepelekea watu wengi kuamini hata taarifa zisizo kuwa sahihi au za kweli na baadhi ya watu wamepoteza maisha yao kwa kuamini taarifa zisizo sahihi na kuacha pengo katika jamii au familia husika.

Ukweli ukisasa ni kitu kizuri hata kupelekea mambo yote kupatikana  kwa urahisi hasa yale yaliyo ya kweli na kusaidia jamii husika, wako watu wamejifunza mambo mbalimbali mitandaoni na kuwa na matokeo chanya mathalani mkimbiaji mmoja toka aliweza kujifunza namna ya kurusha mkuki kwa kasi kupitia mtandao na hatimaye hata kupelekea kuiletea medali ya dhahabu nchi yake kutokana na ushindi alioupata kutokana na mashindano hayo.

Na wengine imepelekea kujifunza mambo mbalimbali na kufaidika na maarifa wanayoyapata kutokana na mitandao mathalani wako watu wamejifunza namna nzuri ya upishi kupitia mitandao na wengine kupata masomo yao kupitia mitandao na mengine mengi.

Ni kweli kabisa maadamu unaishi katika jamii ya kileo uwezi kujitenga na usasa ambao dunia inaenda nao maana kuna baadhi ya watu wanajiingizia fedha nyingi kupitia mitandao kwa halali kabisa,

Ukisasa ( teknolojia) katika dunia ya sasa uwezi kuukwepa ili uyafikie mambo mengi kwa haraka unahitaji kuwa na maarifa sahihi ya hicho kitu ili kikusaidie kuongeza maarifa kwa yale unayoyajua na hata usiyoyajua ili ikusaidie kufanya jambo lilelile katika ubora zaidi wenye tija kwako na jamii kwa ujumla.

Ukisasa umepelekea familia kusambalatika, ndugu kutoelewana kutokana kupenyeza taarifa zisizo sahihi katika fahamu za watu mathalani itikadi kali na imani potofu hata kusababisha kila mtu aamue vile anavyoona sawa pasipo kujilizisha kwa umakini yeye anaamini na kukiishi kile anachoambiwa.

Mahusiano mengi yamekuwa ya kidumu kwa muda wa kitambo na mengine yamekuwa yakivunjika hata kabla ya ndoa na mengine yamevunja baada ya ndoa kutoka na mmoja au wote kutaka kuenenda kama ukisasa  unavyotaka ufanye mathalani kutaka kufanya mapenzi kinyume na maumbilena mengine mengi.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………………..0764 018535

 

Ijumaa, 8 Desemba 2023

NI LAZIMA UPITE ILI PAWEPO NA NJIA;



Uwa njia inatengenezwa na mtu au watu na wala haijitengenezi yenyewe! Ni lazima awepo mtu na aamue pawepo njia ndipo njia utokea,

Na katika utendaji wa Mungu tunaona kuwa ni tabia ya Mungu kufanya njia pasipo na njia! Kwakuwa uweza wake hauna kikomo/hauzuiliki.

Kutoka 14:10 Hata Farao alipokaribia, wana wa Israeli wakainua macho yao, na tazama, Wamisri wanakuja nyuma yao; wakaogopa sana; wana wa Israeli wakamlilia Bwana.

13 Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.

-          Ni maneno ya musa akiwaambia Israel yakionyesha kuamini neno la Mungu na uweza wake!

Kama binadamu unayeishi katika dunia hii kuna majira unafika unaweza kuona kukumbana na mazingira ambayo sio rafiki/kandamizi unaweza kuona nyuma maadui na mbele bahari ya shamu hapo ni lazima patokee njia ili uweze kupita la sivyo unaweza kuangamia,

Ni kweli watu upenda kupita njia ambayo ipo tayari inatumika pasipo kujua hiyo njia mpaka imekuwa njia kuna mtu ili mgharimu kuifanya ili wengine wafaidike kwa kuitumia, waswahili wanasema “mwanzo ni mgumu”,

Unapopita katika njia ambayo wengine imewagharimu hata ikawepo basi hapo jua nawe unadeni katika kutengeneza njia ili wengine wapite.

Usiogope kuandaa njia kwa ajili ya wengine ili wapite lakini tambua kama na wenzako wangeamua kuogopa wewe leo usingeijua njia unayoipita leo.

Na tambua kupita katika hali ngeni (experirnce) mpya iliyo katika changamoto kwakuwa uwezi kujua hasa matokeo yake yatakuaje! Na hata kama ni jambo ambalo wengine wamepitia na wako salama lakini swali litakuwa kwako ni kweli matokeo aliyoyapata mwingine nawe utayapata au itakuwa tofauti na ikiwa tofauti utakuwa katika hali gani? Mathalani unaweza kuwa muathirika wa ukimwi na ni kweli unaweza kuwa na shuhuda za watu waliopona  ukimwi lakini ikija upande wako ni kweli utapona au utakufa? ( maana tunajua sisi tuna amini lakini muamuzi ni Mungu ).

Ni kweli unapopita mahali akili yako inapo kosa mwanga au matumaini basi machozi hapo yanakuwa ni fungu lako.

Niseme tu inaweza ukalia baada ya kujitambua kuwa umekosa au kupoteza matumaini kwani hata yesu mwenyewe alilia hata akatokwa na machozi ya damu lakini lile chozi alikumfanya ashindwe kukamilisha kusudi lake alilopewa na Mungu hapa duniani.

Tatizo sio kulia bali nikuendelea kulia katika hali ya kukosa muelekeo matumaini tena,

Ni muhimu kuwa na fikra pana na usione katika dunia ni wewe pekee ndio mambo yanakusonga kana kwamba jicho la Mungu liko mashariki nawe uko magharibi kwahiyo Mungu haoni kile kinachoendelea katika maisha yako.

Usilie kwa sababu ya kutoa uchungu moyoni kwani baada ya kulia na kama hali haijabadilika basi hapo kilio kitaendelea pasipo kukoma lakini itakuwa tofauti tu mara tumaini jipya litakapo chipuka ndani yako.

Mruhusu Roho mtakatifu alete mwanga au tumaini katika akili yako iliyo na giza maana ni yeye tu awezaye kuifanya njia nawe ukaiona kisha ukachukua maamuzi ya kupita, na lazima uione kutokea ndani yako! Maana ni yeye anayekuonesha njia ambayo wengine hawawezi kuiona mpaka pale umepita ndipo wengine waione njia wapite kwasababu wewe umepita.

Kuna raha sana baada ya wewe kupita na wengine wakaona njia nao wakaanza kupita unakuwa kama mtu aliyejigharimu kujenga nyumba nzuri japo aliteseka lakini furaha yake inakuwa pale atakapoona watu wengine wanakaa humo na kupafurahia yeye uwa furaha yake inazidi hasa akikumbuka namna alivyokosa usingizi na kujinyima ili akamilishe jambo hilo japo anaweza jua kuwa ile gharama aliyoingia kuna mtu anafurahia.

Ni kama yesu furaha yake uwa inaongezeka japo ili mgharimu kufa na kufufuka, ila anapoona kuna watu wanaokolewa yaani wanaifuata njia ambayo yeye aliitengeneza.

Ni sawa na mama mjamzito uwa furaha yake inakuwa nyingi pindi anapo mpakata mtoto wake katika mikono yake japo inawezekana alipita katika hatua ngumu tangu ujauzito hadi kujifungua!

 

ISHI ILI WENGINE WAISHI!

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey  Nelson………………………………………………………0764 018535

 

Ijumaa, 24 Novemba 2023

NI KWASABABU YAKO:

 



Ø  Kufanya kitu sio tatizo maana hayo ndio maisha lakini endapo ukaamua kufanya kitu kwa ajili ya mtu mwingine hilo linakuwa ni jambo lingine na lenye mtazamo mwingine likiambatana na mguso mwingine.

Ø  Figo inaposhindwa kufanya katika viwango vyake na unapoenda hospitali kupata matibabu yake hilo ni jambo linalotarajiwa na watu wengi lakini endapo utaenda hospitali kwa ajili ya kutoa figo kwa ajili ya mtu mwingine ili aweze kuishi hilo ni jambo lingine lenye kuonyesha upendo wa namna yake. ( unahatarisha maisha yako kwa ajili ya mtu mwingine )!

Ø  Naam…….Kitendo cha kulia kinawezekana kuwa ni jambo la kawaida kutokana na majira na matukio fulani yanayo mkumba mtu lakini inapotokea unalia kwa ajili ya mtu mwingine linakuwa ni swala lingine lenye mtazamo mwingine wenye thamani nyingine,

-          Mathalani kumuona mtu analia unaweza kumpita tu au kutoa kauli ya pole kisha kuendelea na shughuli zako lakini pindi utakapojua kuwa analia kwa ajili yako hapo unaweza kuvuta subira na kutaka kuwa naye karibu hasa endapo kama hauta tambua kwanini anakulilia, kwakua utataka kujua kwanini ameamua kulia kwa ajili yako na wala sio mtu mwingine.

Ø  Pia………Ni jambo la kawaida kumuona mtu ameshika jembe na kuelekea shambani hasa katika mazingira ya vijijini, wakati mwingine ana kwenda asubuhi sana akiwa amebeba kidumu cha maji na jembe pamoja na panga, anakwenda shambani huku akijua amemuacha mke na watoto wake hivyo amebeba majukumu mabegani mwake akiwa anawaza tu kule aendako na familia aliyoaicha nyumbani na wakati mwingine hata bila kujijali yeye mwenyewe bali wale wanao muhusu tu ( familia ) na wakati mwingine anarudi jioni sana akiwa amechoka sana akili, hisia na kimawazo pamoja na mwili lakini bado atawaza kesho kwenda tena.

Ø  Vilevile unaweza kukuta mtu asubuhi na mapema tayari yuko barabarani akigombania magari/mabasi ya kwenda kwenye shughuli zake ( hasa maeneo ya mjini ) uwaacha jamii inayomzunguka na kumtegemea/kumuhitaji anaenda kutafuta kwa ajili yao, mvua na jua vyote vinaishia katika mwili wake lakini anakubali hali zote ili mtu mmoja awe salama hama jamii yake kwa ujumla iweze kukaa katika hali njema.

Naam!

-          Hakuna raha unayoipata kama ukisikia au kujua kuwa haya yote mtu anayafanya ni kwa ajili yako tu na wala sio kwa mtu mwingine hama jamii yeyote, na wala sio kwa ajili yake! Amekubali adhalilike au aibike au pengine hata mwili wake kupata shida ili wewe uwe katika namna njema.

-          Bila shaka hakuna mtu asiyependa kuwa na mtu wa namna hii, mtu mwenye kuhakikisha furaha yako haipungui/ huzuni inapita mbali na maisha yako bali utulivu na raha unakuwa matuo ndani yako.

-          Naamini kama ungetambua mtu wa namna hiyo yupo duniani hata kama anaishi pembeni mwa dunia amini ungejipanga kwenda kukutana naye hata kama sio leo au kesho hama wakati muafaka ili siku ukikutana naye maisha yako uyaweke mikononi mwake kwa kuwa utajua maisha yako yatakuwa salama katika matunzo mema.

-          Na ukweli huo ndio mtihani unawakumba wanadamu katika dunia ya leo….anapoona hapa ndipo barafu anashangaa moto umeanza kumchoma na anapofikiri hapa ni sehemu salama ya kupumzika anakuta majani yameanza kumuwasha mpaka inampelekea machafuko kutokea, mauaji na hata chuki iliyokithiri inakuwa katika mioyo ya watu, watu wanatembea huku mioyo yao inavuja damu kwa sababu uliye muamini hakuweza kudumu katika kuaminika.

-          Uzuri ni kwamba yuko Mungu anayekujua na alishakujua kabla ujaja duniani na anajua kuwa ni nani yuko tayari kuibeba aibu yako na kukustili katika hali yoyote utakayo kuwa nayo.

-          Kiukweli una muhitaji Mungu kwanza yeye ndiye anaweza kukutanisha na yeye aliyemkusudia ambaye atakuwa kimvuli salama kwako na sio jangwa.

-          Bidii utakayoitumia katika kumtambua yeye naye atakutambulisha katika mtu atakayekamilisha ndoto yako na sio kuhiharibu.

 

INAITWA KESHO! BARIKIWA SANA.

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………………………..0764 018535

Jumamosi, 11 Novemba 2023

KUMPENDA MUNGU KAMA NJIA YA UKOMBOZI:



Zaburi 107:20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.

-          Neno la Mungu lina uwezo kukutoa katika maangamizo yote endapo utalikubali na kulipa nafasi.

Kuna maisha uwa yanaanza pale mtu anapokombolewa, maisha ya kwenye vifungo hayana uhuru na amani timilifu.

Naam ukombozi ni jambo muhimu na baadhi ya wakristo wanaamini kufunguliwa kunakotokana na maombezi ( kwa kiasi kikubwa ) watu uamini hapo nami kwa kiasi kikubwa na kubaliana nao japo na amini ukombozi huu unaweza usiwe wa kudumu.

Lakini napenda kusema kufunguliwa kunakotokana na kumpenda Mungu uwa ni wakudumu kwa asilimia kubwa labda ukengeuke au kuiacha imani.

Uponyaji unaozaliwa katika kumpenda Mungu huu ni uponyaji unaoanza ndani yako ukiruhusiwa na ufahamu wako uliokubali mabadiliko hayo.

Huu uponyaji uwa unajijenga kwa ndani vizuri kabla ujaanza kudhihirika kwa nje na uwa ukipona unapona jumla ( sio ugonjwa wa kujirudiarudia ).

Kama ilivyokuwa uhitaji mkubwa kwa wanadamu ni kupendwa ndivyo ilivyo kwa Mungu haja yake kupendwa!

Na kama watu wanapopendana sana, uweza kupelekea kuishi pamoja, ndivyo hivyo ukimpenda Mungu uwa unaacha vyote na kuamia kwako jumla vile alivyo na vyote alivyonavyo anakuja na kukakaa kwako milele.

Kama unahitaji ufunguzi wa kweli na wakudumu unahitaji kumpenda Mungu kwelikweli, kwa kiwango kile unachompenda ndicho kiwango utaona mema yake katika maisha yako.

Unapompenda kwa kweli unafanya yeye kuwa jukumu la kuhakikisha maisha yako yako salama wakati wote.

Ni kama vile mtu anapougua utegemea dawa/ maelekezo ya daktari yanaseamje: wengine wataambiwa wameze dawa, na wengine kujichua n.k, pindi mgonjwa atakapopewa maelekezo ya kumeza dawa naye akaanza kutumia na baadae akaanza kuona unafuu katika mwili wake basi hizo dawa zimefanikiwa katika lile lengo lililokusudiwa endpo huo unafuu utakamilisha uzima mkamilifu.

Ndivyo ilivyo katika kusudi la Mungu kupitia neno lake unapolimeza/kulisoma linakwenda kupambana na vitu visivyosahihi kukaa ndani yako ikiwemo magonjwa ya kutupiwa/ya kawaida au tabia ngumu katika uwezo uliondani ya neno hakuna kitu kitabaki salama labda neno likose ushirikiano na wewe.

“ ukinipenda utalishika neno langu”

Yohana 14:23 Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.

Unapoamua kulishika neno lake naye Mungu anashika maisha yako na kukufanya vile apendavyo yeye.

Kulishika neno kwa lugha nyepesi tunasema ni kulisikiliza vile linavyotaka na kuamua kufanya sawasawa na lilivyokukuagiza.

Ukiisha katika agizo lake hapo utaona utajiri wa neno ulizaidi ya duniani hata mbinguni.

Unahitaji kumpenda Mungu ili afanyike uzima na nguvu dhidi ya maradhi na uvamizi wowote wa giza.

“UKIMPENDA  ATAKUPENDA”

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson……………………………………………………………………0764 018535