Ijumaa, 28 Juni 2024

INGIA NDANI

 



Kuna tofauti kubwa kati ya mtu anayeongea mambo akiwa ndani na mtu anayeongea mambo akiwa nje! Ni sawa na mtu anaongea mambo anayojua na mwingine hasiye yajua hawa ni watu wawili tofauti na hata ujasiri wao ni tofauti kabisa.

Kitu chochote ili uwe na uhalali/ujasiri wa kukiongelea au kukisema ni lazima ukijue au uwe ndani ya hicho kitu….ndomana waswahili wanasema “ ukitaka kujua uondo wa ngoma uingie ndani na ucheze “

Kwa asilimia kubwa inaaminika mtu aliye ndani ya jambo anakuwa na ushawishi mkubwa wa kusikilizwa mathalani mtu aliyeko kwenye ndoa mwenye umri zaidi ya miaka 50 ndani ya ndoa na ndoa yake ikiwa bado imebeba ubichi/ ustawi mtu huyu anakuwa na nguvu kubwa ya kusikilizwa na watu wengi walio katika ndoa hata wale ambao bado hawajaingia ndani ya ndoa hata kama ataongea sio vitu vya msingi sana lakini yale maisha yake katika ndoa yata mbeba na kumpa ushawishi kwa maana mtu anaongea kitu anachokiishi.

Pia mtu aliye ndani ya huduma kwa muda mrefu na kustawi anakuwa na ujasiri pamoja na ushawishi katika kueleza hali ya huduma ilivyo sawasawa na Mungu alivyompitisha.

Ni muhimu uwe ndani ili uwe miongoni mwa wale unaowasema au kuwawazia yaliyo ndani yako.

Bila shaka hata fahari ya Mungu utaanza kuiona pale utakapokuwa ndani yake, kwakuwa Mungu hawezi kujifunua ukiwa nje yake bali ukiwa ndani yake japo ni Mungu asiye na mipaka.

-          Maana hata utendaji wa Mungu unaanza kuona tokea ndani yako ndipo udhihirike kwa nje.

Naam unapokuwa ndani ya mfumo na uka uelewa mfumo kuna namna sahihi utaongea mambo yanayo husu huo mfumo na hata mapengo yake utaanza kuyaona kwa uhalisia wake na kuweza kuyaziba.

Na unapokuwa ndani uwa utaongea kile unachopaswa kuongea na sio kile unachojisikia kuongea.

Na makosa mengi unaweza kuyaona/kufanya pale unapokuwa nje ya mfumo na pengine hata kuwaza kuona walitakiwa kufanya hili au lile basi mambo yangeenda vizuri.

Bila shaka unapokuwa ndani ya Mungu hapo unaweza kumtambua Mungu kwa mapana yake na yeye kukutambulisha kuwa wewe ni nani?

 Ni kama unaweza kuwa mchoraji au mcheza mpira usiojifahamu lakini watu wanaokuona wakaanza kuona uwezo wako pale unapokuwa uwanjani au katika kuchora na kuanza kukupa njia ya namna ya kufika mbali zaidi.

Jambo lolote utakalojiweka ndani yake ni wazi utalifanya katika usahihi na ufanisi mkubwa na hata kama utatoa hukumu bila shaka utatoa hukumu kama wewe ndo unahukumiwa.

Pindi utakapotokea kufanya jambo na wewe ukawa ndani yake ni vigumu tu kukata tama maana ukiwa ndani ya mazingira hayo kuna hali yako binafsi katika kutaka kufanikiwa kwa gharama yoyote hata pasipo kuvipa nafasi vipaumbele vipingamizi dhidi ya ndoto yako.

Ni muhimu sana jambo lolote unalolifanya uwe ndani yake ili uweze kupata matokeo unayopaswa kuyapata iwe ni kazi ulioajiriwa au uliojiajiri ili uweze kutumia uwezo wako wote na nguvu zako zote katika kuleta matokeo unayopaswa kuyaleta katika shughuli husika.

Mungu anapenda uwe ndani yake ili uweze kupata uwezesho wa kufanya yake na kuwa kile kitu ambacho Mungu anatazamia.

Kufanya jambo ukiwa nje yake kuwa na mwenedelezo uliobora ni ngumu kwa kuwa uifanyi kuwa ni maisha yako/haipo mizizi ya kuimili kishindo cha dhoruba  na mafuriko yanayotaka kukuondoa hapo.

Unapokuwa nje sio rahisi kuwa na mtazamo sahihi!

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………………………………………………..0764 018535

 

Ijumaa, 14 Juni 2024

HAUNA MIPAKA

 

Neno mipaka katika upande mmoja ni neno nzuri na ni kiashilio chema katika mazingira fulani na maisha ya mwanadamu kwa ujumla wake, maana ina aminika kuwa mwisho wa mpaka wako ndio mwanzo wa mpaka wa mwingine hivyo unavyoishi katika mipaka yako ina maana unaheshimu mipaka ya mwingine.

Kuna mipaka katika vitu vingi mathalani mipaka ya maeneo na maneno, lengo la mipaka ni kutoa muongozo wa nini cha kusema na cha kufanya naam wewe kama binadamu uwa hupaswi kuongea chochote tu bali katika kila jambo kuna mipaka yake mathalani unapoongea na mtu aliyekuzidi umri kuna namna ya kuongea naye na pia kuna maneno ya kuongea naye na unapozingatia mipaka ina maana unamuheshimu yule unayeongea naye hata bila kumwambia shikamoo.

Kama hautazingatia mipaka yako usitegemee wengine wakaiheshimu/kuizingatia, mara nyingi vile unavyoiheshimu mipaka yako ndivyo hivyo wengine watafuata.

Katika maisha tunayoishi kuna hali mbili zinazodhihirika katika maisha ya watu, kuna hali ya kujiwekea mwenyewe mipaka na kuna hali ya kuwekewa mipaka nje ya ridhaa yako, unaweza kuwa unapenda au haupendi hama unajua au haujui lakini unakuwa kifungoni katika maisha usiyoyapenda.

Pia kuna mipaka uliowekewa katika ulimwengu wa roho ambayo inadhihirika katika ulimwengu wa mwili. ( kwa asilimia kubwa mipaka mingi wanadamu wanayotembea nayo huwa imeanzia rohoni ).

Moja ya athari kubwa ya kuishi katika mipaka uliyowekewa ni kuishi katika maisha uliyoamriwa na sio yale unayotaka au kukusudia.

-          Hakuna jambo utapanga likaenda, vikwazo vitakuwa ni maisha yako!

Bila shaka unapoishi nje ya wewe basi utakuwa unaishi kwa kujitahidi sana ni sawa sawa na kutaka kuku  aishi kama bata au nguruwe aishi kama mbuzi.

-          Unaweza kuwa nyima uhuru kuishi katika asili yao lakini baadae watarudi katika asili yao pindi watakapotoka kifungoni.

Kuna mipaka inayotawala maisha yetu:

-          Inayotokana na;

a)      Wazazi wako

-          Kazi gani ufanye?

-          Nani umuoe/ uolewe naye?

 

b)      Ukoo

-          Yapi yasiyofanyika katika ukoo wako? -Hutayafanya hata kama ni mazuri kiasi gani?

-          Yapi yanayofanyika katika maisha yako? -Utayafanya hata kama yanagharimu maisha yako.

 

c)      Binafsi

-          Ni kile ulichokikubali na kukifanya kuwa ni maisha yako.

Haya yote yanaweza kukusaidia katika kujifungia geti na kujiwekea kufuri na kuona kuwa ni sawa tu na ndivyo hivyo unapaswa kuishi.

Wakati mwingine mtu h upenda kuishi humo katika simulizi na kuamini kuwa hiyo ndio njia sahihi ya kuishi na wakati mwingine huo mtindo wa maisha unaweza kumweka katika mazingira magumu hata kupelekea kutofurahia maisha yake.

Pia kuna mipaka iliyojitokeza katika maisha yako kutokana na matokeo ya hofu, ulivyofanyiwa na matendo uliyofanya au uliyo yaona kwa macho yako hivyo hali hiyo ikampelekea mipaka katika utendaji wake.

Kuna baadhi ya watu huwa hawaamini kuwa na maisha mazuri, ni mpaka uwe mshirikina au uwe mwizi ndivyo uweze kutoboa/ kushamiri, mbaya zaidi hali hiyo inajijengea hata kwa mtu aliyeokoka na kujazwa na Roho mtakatifu bado haoni hayo maisha yana mhusu au yanawezekana kwake bali hujiweka na kuona ni maisha ya watu wengine.

Kuna baadhi ya watu hawawezi kulala peke yao usiku wanahisi kuna kitu kigumu/kibaya kitatokea au yatamrudia baadhi ya matendo aliyofanyiwa nyuma hivyo huona kulala peke yake ni adhabu.

Pia kuna watu wengine huwa hawanatabia ya kusema kitu hata kama wakishuhudia kwa macho yao ubaya unafanyika au watu wanafanyiana ama yeye binafsi anafanyiwa hata nyamaza kimya hata pale madhara makubwa yatakapojitokeza kwake au kwa jamii husika lakini yote inatokana na mipaka aliyowekewa/ kujiwekea kuwa hatakiwi kusema kila kitu katika maisha yake.

-          Unaweza kuwa ni utumwa wa kisakolojia.

Ni muhimu kutambua kuna mipaka ya Mungu na mipaka ya dunia lakini usiruhusu mipaka ya dunia kutawala maisha yako na kukuendesha japo unapaswa kuiheshimu na kuizingatia ila isichukue nafasi ya Mungu katika utendaji wake.

Ni muhimu ujue mipaka yako imebebwa na neno la Mungu sio maneno ya watu ( wakubwa au wadogo )!

Inakupasa kujua neema ya Mungu ipo ili kukufanya uwe bora sio uwe mnyonge.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na;

Cothey  Nelson……………………………………………………………………………….0764 018535

 

Jumamosi, 1 Juni 2024

AKILI YA MUNGU:



Akili ndio kitu pekee kinachomtambulisha mtu kwa ufasaha zaidi, unapomuangalia na kuona namna anavyofanya mambo yake unaweza kugundua uwezo wa akili yake au mapana au ufinyu wa akili yake!

Unapokuwa na akili ya Mungu unakuwa na neema ya kufanya mambo ambayo akili ya kuzaliwa imeshindwa kutoa matokeo sahihi.

Ni dhana ya kawaida sana, ina aminika kwa asilimia kubwa ili uweze kuufurahisha moyo wa mtu lazima ufanye kitu kinachoendelea kwenye akili yake haijalishi ni kidogo au kikubwa.

Ukifanya kitu ambacho  hakizunguki kwenye akili ya mtu sio rahisi kugusa moyo wa mtu huyo, hata ukifanya kwa ustadi gani au kwa muda wa kutosha kiasi gani bado hautaweza kuleta ushawishi kwa mtu husika.

Naam njia rahisi ya kuwa kitu chochote basi pata/ kuwa na akili yake, mathalani unapokuwa na akili za mnyama basi utafanya matendo ya mnyama, vivyo hivyo unapokuwa na akili ya wadudu basi nawe utakuwa mdudu japo kwa muonekano utaonekana ni binadamu lakini matendo yako yatadhihirisha akili iliyo beba wadudu.

-          Ndio maana kuna matendo binadamu akifanya watu utakuta wanasema “ wewe sio binadamu bali ni mnyama……maana hauwezi kufanya ukatiri mkubwa kiasi hiki “

Kwa kusema hivyo sina maana kwamba kila atendalo mnyama, ndege au mdudu halifai kuigwa au kupata funzo kutoka kwao. La hasha! Yako matendo mengine ya myama au ndege ni mazuri hata kuliko ya wanadamu mathalani hauwezi kuona jogoo kampanda jogoo mwenzake lakini binadamu unaweza kukuta mwanaume anamuoa mwanaume mwenzake na kuishi kama mke na mume kitu ambacho huwezi kukuta kinafanyika kwa wanyama au ndege hata wadudu.

Sio hilo tu pia kuna ndege kama vile kuku anatabia ya kupigania vifaranga vyake kwa gharama yoyote inawezekana yuko radhi yeye asile vizuri lakini ahakikishe vifaranga vyake vimekula vizuri na hata ikitokea kifaranga kimeumia yuko tayari akae hapo kwa muda wote maadamu kifaranga chake kinahitaji uwepo wake, lakini sio baadhi ya wazazi hasa wanaume huweza kutelekeza familia zao kutokana na sababu mbalimbali na kuiacha familia wakati familia inategemea uwepo wake ili maisha yaende.

Moja ya kitu kinachoweza kukusaidia kukaa na mtu yeyote awe kichaa, mwendawazimu, mshirikina, mwizi au kibaka ni uwezo ulionao katika kutambua kinachoendelea katika akili yake na kuwa tayari kukibeba kwa upendo wa dhati pasipo kuangalia gharama yake.

Naam na hata katika dunia ya sasa neno ugonjwa wa akili limekuwa na mdahalo mkubwa katika kutafuta muafaka wake, watu wengi wamekuwa wakichukua maamuzi ya kujiua au kujichukia kwasababu ya mambo wanayo ya kabili yaliyo kosa majibu katika akili zao.

Unahitaji akili yako kuwa salama ili maisha yako yawe salama na pindi akili yako ikishindwa kung’amua fumbo linalo kukabili basi ujue hapo maisha ya mateso yanakuwa ni fungu lako.

Na akili yako ikiwa kifungoni basi hapo ujue na maisha yako yako kifungoni.

Na moja ya msaada mkubwa unaoweza kumpatia mtu mbali na hitaji la haraka alilonalo ni kumpa mtu majibu katika maswali yanayoendelea katika akili yake.

Na mara zote pindi akili inapokosa majibu inamfanya mtu ashindwe kwenda mbele au kurudi nyuma maana anaona mbele hapawezekani na wakati mwingine hata nyuma anaona haiwezekani tena ni kama mbwa kurudia matapishi yake.

Kwa kiasi kikubwa ukichunguza vizuri utendaji wa akili yako unaweza kupunguza lawama juu ya watu unaoweza kuwaona wamechangia matatizo yako.

“ unahitaji akili ya Mungu ili uyafanye yaliyo ya Mungu “

Unapotembea katika akili ya mtu unakuwa wewe umemvaa huyo mtu wakikuona wewe wana muona yeye anayetembea katika akili zako.

Hivyo unavyotembea katika akili ya Mungu watu wanamuona Mungu akitatua shida zao na kuwapa mwelekeo uliobora.

Katika akili ya Mungu kuna uhai na nguvu kupitia neno la Mungu ambalo linafanya akili yako iwe kama Mungu alivyo.

Unapaswa kujua ustawi wako unabebwa katika akili ya Mungu, kwa kutembea katika akili ya Mungu hauwezi kuchoka wala kukata tamaa.

Na sikuzote akili ya Mungu inatembea katika kalenda ya mbingu na sio ya wanadamu au kalenda ya dunia.

Ishi kwenye akili yake uone maajabu yake!

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na;

Cothey  Nelson ……………………………………………………………………………………………….0764 018535