Ijumaa, 24 Aprili 2015

MAUSIANO SALAMA-2



MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI;


Karibu tena katika nafasi ya pili tukiendelea kuhusu swala zima la MAUSIANO, kwakua limekuwa janga na changamoto kubwa katika jamii tuliyonayo kwa kiasi kikubwa na kuzaa matokeo ambayo yameleta muonekano wa pande mbili yaaani POSITIVE SIDE au NEGATIVE SIDE,yote juu ya yote bado tunaona ni matokeo ya yanayotekea katika dunia.

Katika kuendelea na maswali ili kupata hali uelewa wetu hivi kweli unaweza kujishawishi au kushawishika na hata kushawishiwa katika kuingia katika mausiano……….wakati mwingine watu ufurahia au huzunika na wengine walisema kwamba hawakuwa katika utayari wakuingia katika hayo mausiano lakini kutokana na kushindwa kuimiri katika nguvu ya ushawishi kutoka katika upande mwingine wamejikuta wameingia pasipo hiyari yao wenyewe!

Hivyo kutokana na dhana hiyo wako watu wanaojilaumu wenyewe kwa kukubali kushawishika na wako watu wanawalaumu watu ambao waliwashawishi na kufikia katika hali walio kuwa nayo, na wakati mwingine watu wanapoanza uhusiano wao wanakuwa na furaha kubwa pasipo mashaka yoyote na wala kutojua kama ipo siku ambayo watachukizana na kuwa kama maadui wakubwa ambao kama hawajawai kuwepo katika dunia.

Ni kweli matokeo yanapokuwa mabaya katika mapenzi ya wahusika basi kinachofuata hapo ni uhasama wa kudumu na ni watu wa chache tu ambao wanaachana na bado wakaendelea kuusiana kama marafiki katika mausiano mengine mbali na uhusiano uliokuwako hapo awali……na wapo ambao wanadumu katika hili na wako ambao wanashindwa kuimiri kuwa mbali na baadaye kuamua kurudiana tena!

Na amini kabisa yako maumivu makali sana kati ya watu wawili waliopendana sana na baadae kutengana pamoja na hayo yote hayo maumivu hayamshindi YESU alipokuwa msalabani akibeba dhambi za dunia na kututoa mateka katika ufalme wa giza.

MAMBO YA MSINGI KATIKA KUYAJUA KABLA KUCHUKUA MAAMUZI SAHIHI YA KIMAPENZI

I.UTAYARI WA KIMWILI
   
  II.UTAYARI WA KIUCHUMI
                                                   
                                                       III.UTAYARI WA AKILI
            
     IV.KIBALI KATIKA MOYO WAKO
                                                    
                                                     V.KIBALI CHA MUNGU

Haya ni mambo matano ambayo nitaenda kuyanyambua ilikuleta mwanga zaidi katika maamuzi yako na kuleta ujasiri katika maamuzi yako! Na kuwa msaada kwako au katika rafiki zako unaowapenda.

Imeandaliwa na;

Cothey  Nelson……………………………………………0764 018535

Ijumaa, 17 Aprili 2015

FAHARI YA KIJANA



FAHARI YA KIJANA,



 Ninapozungumzia neno FAHARI uwanazungumzia kitu au hali hama namna inayokufanya ujivune,ujisikie bora au ujione unastahili. Na katika hili kuna ushindani mkubwa katika vijana wa pande mbili na wengi wao wakitumia vibaya wakati wake(misuse of time) na wengine kati yao wanautumia wakati wao vibaya wanautumia huku wakilia na wengine wakicheka! Lakini yote tunaona ni maisha na siku zinaenda na hatimae kuishia.

Katika hili naomba niseme wazi tu……….kunafahari ya kijana katika mtazamo wa kidunia na mtazamo wa kimbingu(Mungu) na hapa pamekuwa na mvutano usio kuwa wa kawaida kwani hata waliokuwa nuruni wamekuwa wakijifunza mambo yanaendelea gizani eti wakisema yako mengine ni mazuri yanayofaa kuigwa, lakini cha ajabu waliogizani hawajifunzi mambo yaliyo nuruni zaidi ya uigizaji (kutokua na uhalisia).

Wako vijana ambao wanaamini kuitumikia DUNIA hapo ndipo kunakuwa na fahari ya ujana kwenda sawa na dunia inavyoenda kuutendea haki basi ndipo ilipo fahari ya kijana na wenyewe wanaona wako sahihi sana kuliko walio kinyume chao STAREHE katika matumizi mabaya ya miili yao na matumizi ya fedha isiyofaa na kwa mtu mtumiaji anaweza kuona yuko sawa lakini wengine walio nyuma yao WANALIA na KUSIKITIKA kwa nini ndugu huyu kafikia hatua hii.

Na lipo kundi la wachache linatambua ufahari wa ujana wao kumtumikia Mungu kama ishara ya kumshukuru Mungu kwa kuruhusu atokee dunia na hata kumlinda na hata kufikia mahali alipo sasa hivyo anavyojitazama nakuona kule alikotoka na kumuona Mungu zaidi ya kuona jambo lolote katika maisha yake hivyo anavyojitazama anaona hakuna namna ya kumshukuru Mungu zaidi ya kutoa maisha yake yawe ya Mungu tu siku zote za maisha yake! Hakika ni kundi jema.

Katika pande mbili hizi za vijana kila mtu anakwambia yuko hapo au anafanya hayo akiwa na sababu za kutosha sana ambazo wakati mwingine ukimsikiliza vibaya unaweza kusema hata mimi ningekuwa ni yeye basi nami ningeingia kule huyu alipo, laweza kuwa katika ufahari wa dunia au mbingu!

Usishangae kijana anaweza kukaa katika baa,mitaa usiku wa manane wakati wote pamoja na      yale yanayofanyika katika baa mathalani biashara haramu kama madawa ya kulevya au kuuza miili yao ndo mana nimesema wako watu wanaoutumia fahari ya ujana wao wakiwa wanalia na wengine wanacheka!

Cha ajabu sana unaweza kuwa kuta vijana walianza kumtumikia Mungu kama fahari yao lakini sasa wako kuitumikia dunia kama wakiona hiyo ndiyo fahari yao……hii ni mbaya sana japo hali inatokea na inawatoa machozi watu wengi……kwakua mtu huyo kurudi katika kumtumikia Mungu sio jambo rahisi maana alishaona fahari ya Mungu na sasa yuko gizani na akishaingia huko ujikita uko siku zote, hii ni mbaya kwani huzuni ya Mungu inafanyika furaha kwa ulimwengu wa giza.

Ningependa utambue kama kijana mwezangu mimi sina tatizo na matumizi ya ujana bali nina huzuni na hatima yale unayo yafanya…..laiti ungepata neema yakujua hatima ya yale unayofanya na amini usingeweza kwendelea….kwa mtu mwenye akili awezi weka bidii kufanya kazi uku akijua jua mwisho wa siku hakuna anachokipata!

►Fahari ya DUNIA ina mwisho kwakua dunia itaondoka na fahari yake pale itakapo fika mwisho wake kwakua ilikuwa na mwanzo basi bila shaka kutakuwa na mwisho lakini fahari ya MUNGU kamwe haina mwisho kwakua haina mwisho wala mwanzo hakika hili ni fungu ni jema!

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson…………………………………………….0764 018535

Ijumaa, 10 Aprili 2015

NJIA YANGU



HAKUNA KITU KISICHO NA MWISHO;




Laiti tungekuwa tunaona mwisho kabla ya mwanzo tungekuwa watu wengine sana ila kwasababu hatujui mwisho ndo mana tunajiachia mwanzo!

Binadamu yeyoyote anaposikia kauli hii bila shaka anakuwa na hali ya KUJITATHIMINI… ili kuona yuko sahihi kwa Mungu na kwa wanadamu, na kama katika pande zote hakuna mwelekeo mzuri basi mwenye akili uweza kufikiri namna ya kuitimisha katika mwisho ulio bora unaotoa mwanga wa milele ulio na matumani mema.

Mbali na neno la Mungu hakuna kisicho na mwanzo au mwisho bali vyote vina mwisho haijalishi ni kizuri kiasi gani au kibaya kiasi gani? Bali ilimradi kina mwanzo basi pasipo mashaka mwisho wake upo…..ni Mungu pekee yeye hana mwanzo wala mwisho!

Wako watu upenda kuonekana kuwa wako juu wakati wowote, hivyo ufanya kila haina ya udhalimu kuwa hakikisha heshima yake na hadhi inabaki palepale lakini pamoja na hayo yote jua kuna MWISHO ambao haujui na endapo utakukuta na sijui utakuwa wapi au utakua na hali gani na utakuwa unahatima gani?

Na endapo utaishi maisha haya bila shaka utakuwa na maisha yenye mwelekeo unaoeleweka wenye kukupa nafasi nzuri ya wakati ujao………lakini jambo hili sio rahisi kulitambua na kulipa uthamani katika moyo na utendaji wako.

Binadamu wengi wanaishi maisha ambayo wanasema lolote na liwe maana ndicho nilichokiamua na ndicho nitakachokifanya kwa moyo wangu wote na hakuna kile cha kunitenga tena na maamuzi haya niliyoamua….pasipo kujali nini hasa matokeo katika jamii inayokuzunguka na taifa lako kwa ujumla.

Wako watu waliojiingiza katika maisha hatarisho kama ujambazi na hata ukahaba ukiwauliza watakwambia maisha yamechangia ya mimi kuwa vile nilivyo wala haya maisha sio chaguo langu sikuwai kuota ndoto wala kufikiria nitakuwa na maisha haya…..mimi sisemi uache wala kuendelea lakini nipo hapa kukukumbusha kuwa HAKUNA KISICHO NA MWISHO, na sio kuwa na mwisho tu bali huo mwisho utatoa mustakali gani katika maisha yako yaliyobaki!

Katika maisha ya ukahaba yako madhara mengi yanaweza kukupata na ukajuta kwanini niliingia katika uchaguzi wa maisha ya namna hii tukianza upande wako binafsi afya yako inaweza kuathirika katika kiwango kikubwa sana hata ukajuta kwa nini nimezaliwa kwani magonjwa yatashamiri katika mwili wako mathalani ukimwi na magonjwa mengi ya zinaa…na kupelekea mwisho ukawa wa simanzi badala ya furaha na shangwe kwako,familia yako na kwa jamii kwa ujumla na pia unapojihusisha na mambo haya basi hata jamii itakupa picha ambayo italeta simanzi katika maisha yako na mbaya zaidi utajuta namna ulivyotumia vibaya wakati wako.

Unaweza sema fedha haitaisha kwakua endapo itakapoisha basi nitaenda kutafuta nitapata tu! lakini lazima utambue ili fedha iwepo lazima pawepo na chanzo na endapo chanzo….na hikitokea hicho chanzo kikifungwa basi ni wazi ustawi wako utakuwa umefikia kikomo………na najua kabisa kuwa fedha ndio shina la maovu mengi na endapo kutakuwa na na mbadala wa fedha basi pangekuwa na unafuu mkubwa sana japo sangine watu wangekuwa wavivu au chenyenguvu kingetawala kile kisichokuwana nguvu.

►Ni Mungu pekee yeye ana mwisho wala mwanzo na wala ajui nini maana ya kuishiwa kwakua vyanzo vyake havina mwisho na wala hakuna uwezo wowote unauwezo wa kuharibu chanzo mbacho Mungu anakiambata.

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson…………………………………..0764 018535

Alhamisi, 2 Aprili 2015

MAUMIVU YAKE NDIO FURAHA YANGU



MAUMIVU YAKE NDIO FURAHA YANGU;




 Sio kibinadamu wala alipendezi katika uso wa mwanadamu yeyote…..maumivu ya mtu yawe furaha kwa mtu mwingine na hicho ndicho kinachotutofautisha kati ya mwanadamu na Mungu kwa mateso na dhihaka yake ili sisi tuwe watoshelevu ulio na usalama wa mwilini na rohoni.

Isipokuwa kwa mzazi mwenye mapenzi mema na familia yake yuko radhi mateso yake yawe na tija katika familia yake tu japo sio siku zote……..na hii ni tofauti kubwa kati ya mwanadamu na Mungu ambaye alikuja kwa ajili ya wote waliompenda na waliomchukia kwa kujua au kuto kujua…..lakini yeye aliwajali wote na alikubali dhihaka yake iwe na tija katika wanadamu wote pasipo kujali rangi, muonekano au uwezo wa uchumi wa mtu husika.

Tunaona watu wakijitoa mwanga na kujiua kwa njia mbalimbali lengo likiwa katika kufanya ibada yao kwa Mungu wao na kile wanachokiamini pamoja na kuleta ustawi mzuri katika familia zao….kwakua zinakua ni ahadi kwa wale wanawatuma.

Lakini yesu alikubali kupata maumivu kwa furaha pasipo kinyongo na kujua kile anachokifanya kinaleta faida katika dunia nzima……na hapo ndipo ilipo furaha yangu na majivuno yangu na kuwa jasiri sana kwakua yupo aliniye nigharimia na kuniweka katika nafasi yake tena katika hali ya upendo uliopitiliza.

Maumivu yake yamenipa mwanga maisha yangu ya sasa na hata ya baadae kwakua toni ya damu yake ina maanisha maana kubwa katika maisha yangu kwakua ni udhihirisho wa  kumleta Mungu katika maisha yangu katika kunifanya kuwa niwe wake katika maisha ya umilele.

Maumivu yake yalimaanisha kitu kikubwa katika maisha yangu……….upendo usioweza kujibiwa aliona bora na kuwa tayari kutekeza maisha yake kwa ajili yangu nimeona huu upendo ambao sitakaa nione wala kupata katika maisha yangu yote, kwani kila binadamu anaweza akakupenda lakini bado akaweka kuna sehemu ya mashaka na wewe au hali ya tahadhari kwa lolote litakapotokea yeye anakuwa salama.

Yohana 15:13
“hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”

Kiukweli kupitia maumivu yake leo kunanifanya nione dunia kwana namna nyingine kuona naweza kufanya jambo la maana likawa jambo jema katika maisha yangu na mbele ya uweza wake, kwakua bila yeye ingekuwa ngumu ya mimi kujitambua na kuweza kusimama katika maisha yangu pasipo kuwa na shaka yoyote.

Nguvu yangu katika dunia hii  inatokana na maumivu yake niko salama sana dhidi ya nguvu za giza kwa sababu ya yeye yuko nami na kama akipo cha kumshinda yeye basi hakuna kitakacho nishinda!

Imeandaliwa na;
         
           Cothey Nelson……………………………………0764 018535