Alhamisi, 2 Aprili 2015

MAUMIVU YAKE NDIO FURAHA YANGU



MAUMIVU YAKE NDIO FURAHA YANGU;




 Sio kibinadamu wala alipendezi katika uso wa mwanadamu yeyote…..maumivu ya mtu yawe furaha kwa mtu mwingine na hicho ndicho kinachotutofautisha kati ya mwanadamu na Mungu kwa mateso na dhihaka yake ili sisi tuwe watoshelevu ulio na usalama wa mwilini na rohoni.

Isipokuwa kwa mzazi mwenye mapenzi mema na familia yake yuko radhi mateso yake yawe na tija katika familia yake tu japo sio siku zote……..na hii ni tofauti kubwa kati ya mwanadamu na Mungu ambaye alikuja kwa ajili ya wote waliompenda na waliomchukia kwa kujua au kuto kujua…..lakini yeye aliwajali wote na alikubali dhihaka yake iwe na tija katika wanadamu wote pasipo kujali rangi, muonekano au uwezo wa uchumi wa mtu husika.

Tunaona watu wakijitoa mwanga na kujiua kwa njia mbalimbali lengo likiwa katika kufanya ibada yao kwa Mungu wao na kile wanachokiamini pamoja na kuleta ustawi mzuri katika familia zao….kwakua zinakua ni ahadi kwa wale wanawatuma.

Lakini yesu alikubali kupata maumivu kwa furaha pasipo kinyongo na kujua kile anachokifanya kinaleta faida katika dunia nzima……na hapo ndipo ilipo furaha yangu na majivuno yangu na kuwa jasiri sana kwakua yupo aliniye nigharimia na kuniweka katika nafasi yake tena katika hali ya upendo uliopitiliza.

Maumivu yake yamenipa mwanga maisha yangu ya sasa na hata ya baadae kwakua toni ya damu yake ina maanisha maana kubwa katika maisha yangu kwakua ni udhihirisho wa  kumleta Mungu katika maisha yangu katika kunifanya kuwa niwe wake katika maisha ya umilele.

Maumivu yake yalimaanisha kitu kikubwa katika maisha yangu……….upendo usioweza kujibiwa aliona bora na kuwa tayari kutekeza maisha yake kwa ajili yangu nimeona huu upendo ambao sitakaa nione wala kupata katika maisha yangu yote, kwani kila binadamu anaweza akakupenda lakini bado akaweka kuna sehemu ya mashaka na wewe au hali ya tahadhari kwa lolote litakapotokea yeye anakuwa salama.

Yohana 15:13
“hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”

Kiukweli kupitia maumivu yake leo kunanifanya nione dunia kwana namna nyingine kuona naweza kufanya jambo la maana likawa jambo jema katika maisha yangu na mbele ya uweza wake, kwakua bila yeye ingekuwa ngumu ya mimi kujitambua na kuweza kusimama katika maisha yangu pasipo kuwa na shaka yoyote.

Nguvu yangu katika dunia hii  inatokana na maumivu yake niko salama sana dhidi ya nguvu za giza kwa sababu ya yeye yuko nami na kama akipo cha kumshinda yeye basi hakuna kitakacho nishinda!

Imeandaliwa na;
         
           Cothey Nelson……………………………………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni