HAKUNA KITU KISICHO NA
MWISHO;
Laiti
tungekuwa tunaona mwisho kabla ya mwanzo tungekuwa watu wengine sana ila kwasababu
hatujui mwisho ndo mana tunajiachia mwanzo!
Binadamu yeyoyote
anaposikia kauli hii bila shaka anakuwa na hali ya KUJITATHIMINI… ili kuona
yuko sahihi kwa Mungu na kwa wanadamu, na kama katika pande zote hakuna
mwelekeo mzuri basi mwenye akili uweza kufikiri namna ya kuitimisha katika
mwisho ulio bora unaotoa mwanga wa milele ulio na matumani mema.
Mbali na neno la Mungu
hakuna kisicho na mwanzo au mwisho bali vyote vina mwisho haijalishi ni kizuri
kiasi gani au kibaya kiasi gani? Bali ilimradi kina mwanzo basi pasipo mashaka
mwisho wake upo…..ni Mungu pekee yeye hana mwanzo wala mwisho!
Wako watu upenda
kuonekana kuwa wako juu wakati wowote, hivyo ufanya kila haina ya udhalimu kuwa
hakikisha heshima yake na hadhi inabaki palepale lakini pamoja na hayo yote jua
kuna MWISHO ambao haujui na endapo utakukuta na sijui utakuwa wapi au utakua na
hali gani na utakuwa unahatima gani?
Na endapo utaishi
maisha haya bila shaka utakuwa na maisha yenye mwelekeo unaoeleweka wenye
kukupa nafasi nzuri ya wakati ujao………lakini jambo hili sio rahisi kulitambua na
kulipa uthamani katika moyo na utendaji wako.
Binadamu wengi wanaishi
maisha ambayo wanasema lolote na liwe maana ndicho nilichokiamua na ndicho
nitakachokifanya kwa moyo wangu wote na hakuna kile cha kunitenga tena na
maamuzi haya niliyoamua….pasipo kujali nini hasa matokeo katika jamii
inayokuzunguka na taifa lako kwa ujumla.
Wako watu waliojiingiza
katika maisha hatarisho kama ujambazi na hata ukahaba ukiwauliza watakwambia
maisha yamechangia ya mimi kuwa vile nilivyo wala haya maisha sio chaguo langu
sikuwai kuota ndoto wala kufikiria nitakuwa na maisha haya…..mimi sisemi uache
wala kuendelea lakini nipo hapa kukukumbusha kuwa HAKUNA KISICHO NA MWISHO, na
sio kuwa na mwisho tu bali huo mwisho utatoa mustakali gani katika maisha yako
yaliyobaki!
Katika maisha ya
ukahaba yako madhara mengi yanaweza kukupata na ukajuta kwanini niliingia
katika uchaguzi wa maisha ya namna hii tukianza upande wako binafsi afya yako
inaweza kuathirika katika kiwango kikubwa sana hata ukajuta kwa nini nimezaliwa
kwani magonjwa yatashamiri katika mwili wako mathalani ukimwi na magonjwa mengi
ya zinaa…na kupelekea mwisho ukawa wa simanzi badala ya furaha na shangwe
kwako,familia yako na kwa jamii kwa ujumla na pia unapojihusisha na mambo haya
basi hata jamii itakupa picha ambayo italeta simanzi katika maisha yako na
mbaya zaidi utajuta namna ulivyotumia vibaya wakati wako.
Unaweza sema fedha
haitaisha kwakua endapo itakapoisha basi nitaenda kutafuta nitapata tu! lakini
lazima utambue ili fedha iwepo lazima pawepo na chanzo na endapo chanzo….na
hikitokea hicho chanzo kikifungwa basi ni wazi ustawi wako utakuwa umefikia
kikomo………na najua kabisa kuwa fedha ndio
shina la maovu mengi na endapo kutakuwa na na mbadala wa fedha basi pangekuwa
na unafuu mkubwa sana japo sangine watu wangekuwa wavivu au chenyenguvu
kingetawala kile kisichokuwana nguvu.
►Ni
Mungu pekee yeye ana mwisho wala mwanzo na wala ajui nini maana ya kuishiwa
kwakua vyanzo vyake havina mwisho na wala hakuna uwezo wowote unauwezo wa
kuharibu chanzo mbacho Mungu anakiambata.
Imeandaliwa na;
Cothey Nelson…………………………………..0764
018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni