Ijumaa, 17 Aprili 2015

FAHARI YA KIJANA



FAHARI YA KIJANA,



 Ninapozungumzia neno FAHARI uwanazungumzia kitu au hali hama namna inayokufanya ujivune,ujisikie bora au ujione unastahili. Na katika hili kuna ushindani mkubwa katika vijana wa pande mbili na wengi wao wakitumia vibaya wakati wake(misuse of time) na wengine kati yao wanautumia wakati wao vibaya wanautumia huku wakilia na wengine wakicheka! Lakini yote tunaona ni maisha na siku zinaenda na hatimae kuishia.

Katika hili naomba niseme wazi tu……….kunafahari ya kijana katika mtazamo wa kidunia na mtazamo wa kimbingu(Mungu) na hapa pamekuwa na mvutano usio kuwa wa kawaida kwani hata waliokuwa nuruni wamekuwa wakijifunza mambo yanaendelea gizani eti wakisema yako mengine ni mazuri yanayofaa kuigwa, lakini cha ajabu waliogizani hawajifunzi mambo yaliyo nuruni zaidi ya uigizaji (kutokua na uhalisia).

Wako vijana ambao wanaamini kuitumikia DUNIA hapo ndipo kunakuwa na fahari ya ujana kwenda sawa na dunia inavyoenda kuutendea haki basi ndipo ilipo fahari ya kijana na wenyewe wanaona wako sahihi sana kuliko walio kinyume chao STAREHE katika matumizi mabaya ya miili yao na matumizi ya fedha isiyofaa na kwa mtu mtumiaji anaweza kuona yuko sawa lakini wengine walio nyuma yao WANALIA na KUSIKITIKA kwa nini ndugu huyu kafikia hatua hii.

Na lipo kundi la wachache linatambua ufahari wa ujana wao kumtumikia Mungu kama ishara ya kumshukuru Mungu kwa kuruhusu atokee dunia na hata kumlinda na hata kufikia mahali alipo sasa hivyo anavyojitazama nakuona kule alikotoka na kumuona Mungu zaidi ya kuona jambo lolote katika maisha yake hivyo anavyojitazama anaona hakuna namna ya kumshukuru Mungu zaidi ya kutoa maisha yake yawe ya Mungu tu siku zote za maisha yake! Hakika ni kundi jema.

Katika pande mbili hizi za vijana kila mtu anakwambia yuko hapo au anafanya hayo akiwa na sababu za kutosha sana ambazo wakati mwingine ukimsikiliza vibaya unaweza kusema hata mimi ningekuwa ni yeye basi nami ningeingia kule huyu alipo, laweza kuwa katika ufahari wa dunia au mbingu!

Usishangae kijana anaweza kukaa katika baa,mitaa usiku wa manane wakati wote pamoja na      yale yanayofanyika katika baa mathalani biashara haramu kama madawa ya kulevya au kuuza miili yao ndo mana nimesema wako watu wanaoutumia fahari ya ujana wao wakiwa wanalia na wengine wanacheka!

Cha ajabu sana unaweza kuwa kuta vijana walianza kumtumikia Mungu kama fahari yao lakini sasa wako kuitumikia dunia kama wakiona hiyo ndiyo fahari yao……hii ni mbaya sana japo hali inatokea na inawatoa machozi watu wengi……kwakua mtu huyo kurudi katika kumtumikia Mungu sio jambo rahisi maana alishaona fahari ya Mungu na sasa yuko gizani na akishaingia huko ujikita uko siku zote, hii ni mbaya kwani huzuni ya Mungu inafanyika furaha kwa ulimwengu wa giza.

Ningependa utambue kama kijana mwezangu mimi sina tatizo na matumizi ya ujana bali nina huzuni na hatima yale unayo yafanya…..laiti ungepata neema yakujua hatima ya yale unayofanya na amini usingeweza kwendelea….kwa mtu mwenye akili awezi weka bidii kufanya kazi uku akijua jua mwisho wa siku hakuna anachokipata!

►Fahari ya DUNIA ina mwisho kwakua dunia itaondoka na fahari yake pale itakapo fika mwisho wake kwakua ilikuwa na mwanzo basi bila shaka kutakuwa na mwisho lakini fahari ya MUNGU kamwe haina mwisho kwakua haina mwisho wala mwanzo hakika hili ni fungu ni jema!

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson…………………………………………….0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni