Ijumaa, 29 Mei 2015

HE KNOWS MY TOMORROW



ANAIJUA KESHO YANGU




Hakuna kitu kizuri kama kuwa na KESHO yenye uhakika, yenye matumaini mema yenye furaha ya kudumu, yenye maisha mengine yenye daraja linguine lilibeba jambo jema katika maisha yako.

Hakuna mtu mzuri ambaye unaweza kukaa nawe katika furaha na kujiamini kama mtu anaye ijari kesho yako……..na katika dunia ya sasa watu wengi wana amini kuwa kesho inatengenezwa na leo na hasa wako watu wengine wana amini pia kuwa kesho inakutegemea wewe!

Ni jambo la kawaida kwa mtu anapoona kesho yake itakuwa ni nzuri au imebeba jambo jema kwa  mtu mathalani mfanyakazi uweza kujibidisha sana pindi anapo ahidiwa kitu kizuri ambacho kitaboresha maisha yake…mfano bosi akamwambia mfanyakazi wake akisema kama ukiendelea na moyo huu kufanya bidii katika kazi nitakupa nyumba,gari au mshahara uliobora zaidi.

Na wengine uweza kushusha bidii zao katika kazi pindi anapotambua kesho yake haina mabadiliko chanya au manufaa katika maisha yake, uwa katika kipindi hiki mtu uweza kuacha kazi anayoifanya………..hauwezi kuendele mbele tu wakati ukijua mwisho wa njia yako kuna shimo litakalo hitimisha maisha yako.

Hakuna jambo la maana sana kama kutambua yuko mtu anayeitambua, kuijali na kuithamini kesho yako ni jambo linalo kukupa kushinda hata kabla ujapigana!

Lazima utambue kuwa yuko Mungu anayeipenda kesho yako na kutaka kuwa ya maana zaidi unavyofikiria……….japo wakati mwingine tunaona sisi kuijali kesho yetu kuliko yeye ambaye anairuhusu kesho ije kwa ajili yako.

Ni seme wazi kuwa kesho yako hauwezi kuielewa na kuibeba na hata kuistahimili pasipo Mungu kuweka wazi kwako…….mkulima japo anaamini baada ya kulima katika kufuata kanuni za kilimo chenye tija lakini bado anaweza asiifurahie kesho yake kwani matatizo mengi yanaweza kujitokeza mfano mafuriko na kuondoa mazao shambani na kupeleka mtoni, wakati mwingine unapozalisha vizuri unaweza ukakosa soko la kuuza, hata mkono wa serikali ukashindwa kukutoa pale ulipo kwa kununua yale mazao na hatimae ukabaki na yohayo mazao na hatimae kuoza na kupata hasara baada ya kupata faida,

Hivyo kuanza vizuri sio kuonyesha kutakuwa na ishara nzuri ya kuendelea katika ustawi wake bali vyote vinamtegemea Mungu!

Hivyo ni seme kesho yako uiweke mikononi mwa Mungu haijarishi nini kitatokea baki hapo kwa kua katika yeye hakuna maumivu bali kuimarisha, hakuna kuachwa bali kuna kukumbatiwa, hakuna kutengwa bali sikuzote kuna kukumbukwa ndo mana Mungu anasema mama anaweza kumsahau mtoto anyonyae lakini yeye hawezi kumsahau mtu wake na kamwe hawezi kukusaliti kwa kuwa ndani yake hakuna kisasi.

Wako watu wanaiweka kesho yao katika mali,wenzi na hata ndugu wa wapendao hivyo kuyaweka maisha yao rehani kwakua hao wote wana kesho yao na inaweza kuwa kuwa ni tofauti na kesho yako………..naomba ni kuhakikishie kuwa hakuna mtu anaweza kuitunza kesho yako kwakua kila mtu anahitaka kesho yenye manufaa yaliyo bora na yenye mantiki na katika hali hiyo unaweza kuwa na mtu ambaye mnashindana katika kuitafuta kesho iliyo bora, sio kesho ya maana sana pindi unaweza mkatembea na msichana mwenzako wote mkawa na kiu inayo fanana katika hayo pakawa shida kutoelewana baada ya kusaidiana mkawa mnakandamizana!

Lazima ujue kesho yako nzuri ni fahari ya Mungu!!

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………..0764 018535

ANAIJUA KESHO YAKO MWACHIE AINDAE!!!

Ijumaa, 22 Mei 2015

UFANYE WOKOVU KUWA NI KITU BORA



UBORA WA WOKOVU


 Kufanya wokovu kuwa kitu cha kutamanika au kuvutio na chenye maana kuliko chochote hilo ni jukumu lako……..na unaweza kudaiwa endapo tu! utafanya wokovu ukaonekana hauna thamani katika maisha ya mwanadamu, kwa maana ya wokovu wenyewe umepita viwango vyote vya ubora wa dunia na hata wa mbingu.

Mungu ameshamleta mwanae wa pekee ambaye ni yesu kristo kwa ajili ya ulimwengu kama zawadi yenye thamani kubwa kuliko chochote na ili kuwapatia wanadamu nguvu na kuimarika katika yeye.

Ukweli sio kitu chepesi kuonyesha wokovu kuwa ni kitu bora katika mahali ulipo unaposoma,unapofanya kazi na hata unapoishi na majirani zako kwa kuwa watu utaka kuona utofauti uliopo kati yako na mwingine au na yeye……mathalani unaweza kuwa umeajiriwa na bosi ambaye ajui wokovu maana yake nini? Anaweza kukujia na kutaka kuona maana ya wokovu kupitia wewe japo! Anakulipa mshahara kwa maana nyingine anachangia jeuri yako au furaha yako.

Ki ukweli wako watu wanaishi maisha katika wokovu kiasi kwamba marafiki zake au ndugu zake na hata mahali anapofanyia kazi wasione maana ya yeye kwenda kanisani au kujiita au kujitambulisha ameokoka kwakuwa hawaoni tofauti kati yao na yeye  na hivyo kuwa ni  changamoto kwake katika kuwafanya jamii inayo mzunguka katika bidii katika kujua zaidi fahari yake katika imani au mwenendo wake!

Wako watu ambao wamekuwa wakijitenga na watu wasio mwamini Mungu katika imani yao  kama wazazi wake, familia yake kwa ujumla na hata wafanyakazi wenzake na kuona hao watu hawapaswi kuchangamana nae…na akiona kuwa huo ndio ufahari wake wakujitenga na wasio amini!  

Wamekuwa wakiishi maisha hayo na kuona huo ndio wokovu.

Ukweli kwamba wokovu umepewa wewe ili kwanza uwefaida kwako na ukawe faida kwa wengine na hivyo basi kama usipo ona wakovu kuwa wa faida kwako ni wazi hakuna mtu ataona kuwa wokovu ni kitu bora sana kwakua wewe umeanza kuona kuwa sio kitu bora.

Sio furaha ya Mungu kuona wokovu unakuwa kuwa sio kitu bora kwa maana kwake yeye ni kitu bora sana kuliko chochote hivyo anaamini kuwa kitakuwa cha maana sana kwako na katika jamii wanayokuzunguka kwakua katika yeye hakuna kinachoshindikana……japo havifanyiki kwakua umesha mpokea bali namna unamfanya aweze kuwa msaada kwako na kwa wengine.

Lazima ujue kuwa pindi waokovu unapokosa nguvu katika jamii inayokuzunguka tambua kuwa hiyo ndio huzuni ya Mungu kuliko chochote kile ambacho unaweza kuwaza au kufikiria katika njia yeyote.

Ni vizuri ujue kwamba furaha ya Mungu ni kuona wewe unafurahi na hivyo hata furahi kuona wewe binafsi unaona wokovu kama janga au mateso katika maisha yako na ikiwa yeye ameachilia ni kitu chenye ushindi zidi na chenye thamani kubwa kuliko kitu chochote ulimwengu wa sasa na hata wa baadae!

Unaweza kuufanya kuwa wokovu kuwa ni kitu bora sana na wengi waka mfuata Mungu kupitia wewe binafsi kwa namna unavyoenda mbele za Mungu kwa ukamilifu kuliko chochote.

Kuna vitu viwili nataka ni viweke wazi japo kuwa sitavielezea kinagaubaga;

i.baba wa kiroho
huyu ni mtu muhimu sana hakikisha unamsikiliza na kuona kupitia yeye upo vile ulivyo na utakuwa zaidi kwakua katika yeye unamuona Mungu.
Hakikisha unamshirikisha katika jambo jema na hata baya na kuona kile atakachofanya au kukisema katika yote muone kuwa ni baba bora na wa maana sana katika maisha yako.
Popote unapoenda hakikisha moyo wako uko vizuri na yeye japo wakati mwingine yeye kama mwanadamu anaweza akafanya yale yasio upendeza moyo wako lakini katika hali yoyote jua ni baba mpaka pale Mungu atakapo amua jambo jingine katika maisha yako

Ii. Roho mtakatifu
Huyu ni zaidi ya baba wa kiroho na mtu mwingine yeyote kwani nafasi yake hakuna mtu atakaye weza kufanya, Mungu amempa heshima kubwa sana….dhambi zote unaweza kusamehewa lakini sio dhambi ya kumkufuru Roho mtakatifu!! Hapa kuna nini ni jambo la kushangaza sana.

Lakini katika yote msikilize ili akupe dira yako hatua zako furaha yako na maisha yako kwa ujumla wake, na ukimuelewa na kumkubali kamwa hauwezi kuchoka, kupotea na hata kuto timiza ndoto yako.
MWAMINI YEYE UTAKUWA SALAMA!!!
Imeandaliwa na;
Cothey Nelson………………………………………………. 0764 018535

Jumatatu, 4 Mei 2015

MAUSIANO SALAMA-5



MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI;


 Tukiwa bado tunaendelea na mfululizo wetu wa MAUSIANO katika ujumla wake, na leo pia tunaendelea katika sehemu ya tano……………hivyo karibu sana rafiki katika kuendelea kupata mwanga katika kuzidi kusonga mbele!

III.UTAYARI WA AKILI

Hapa ni uwanja hatari sana kwakua katika hali ya akili kupevuka na kutaka kujua kila kitu kwa zaidi sana….na siku zote akili uweza kushawishika na mwili na hata katika kuona,kusikia na hatimae ikazalisha kiu ya kutaka kufahamu kitu zaidi ambacho kinaendelea katika jamii husika japo yako mambo mengi yanaendelea katika jamii husika lakini yako mambo ambayo yanashawishi zaidi na kuwa kivutio katika macho na kinachobeba hisia.

Hivi sasa katika jamii husika kuna mambo ambayo ni kivutio kwa watu wazima kwa maana watu wenye rika kubwa zaidi na vijana kama watu wenye rika la wastani na kundi la watoto, na ndani ya jamii yetu katika ulimwengu wa sasa mambo mengi yasiyo ya maana sana yamekuwa yakitawala katika akili ya watu wengi hasa walio na rika 14 mpaka 35 ambao ndio tegemeo katika jamii husika katika kuleta chachu ya maendeleo katika jamii husika.

Watu wengi wamekuwa wakiichosha akili zao katika kutumia mambo ambayio yanaridhisha miili yao na sio jambo lililo na manufaa sana katika maisha yake mathalani kuangalia picha za ngono na kuanagalia staili za kufanya mapenzi na kuziweka katika maisha yao kwa hakika akili zao zimetiwa giza na kuona giza zaidi ya kuona nuru ambayo italeta matumaini katika maisha husika.

Matumizi hayo ni shida kubwa katika maisha yake pamoja na jamii inayomzunguka hawajui kuwa “MISUSE OF MIND”  ni shida kubwa kuliko jambo lolote lile ambalo wanaoliona wenyewe wanaona kuwa ni kwenda sawa na dunia inavyoenda na sio kuangalia mwisho wa safari ya dunia, ukweli hakuna kitu cha maana na chenye thamani kubwa zaidi ya akili lakini namna unavyotumia akili yako ni ishara kubwa kuwa unajipenda au haujipendi kila kitu unachokiangalia kizuri ujue ni matumizi sahihi ya akili lakini sasa tumekuwa tuko tayari kupokea kila kitu tunacholetewa hivyo hatujui kuwa kinamanufaa kwetu au la! Bali kwakua kimetengenezwa na mtu mwenye ngozi nyeupe kila kitu anachokifanya basi sawa.

Akili inapokuwa na upofu uwezi kujua maana ya msemo huu LINALOWEZEKANA LEO LISINGOJE KESHO  msemo huu una maana yake lakini akili yako inavyotiwa giza uwezi kuona maana ya matumizi sahihi ya akili ambayo italeta maana kubwa sana katika maisha yako

Ukweli akili ya mtu ndio dereva wa maisha ya mtu husika akili ikishachafuka tu hakuna la maana linaloweza kuonekana katika maisha ya mtu husika, hivyo unahitaji kuwa makini sana kuliko sehemu yoyote……unahitaji kuona fahari ya akili yako katika matumizi yaliyo sahihi kuliko chochote kwa maana hakuna fahari ambayo itaipita fahari ya akili uliyonayo kwa maana ni jambo la maana sana kwa mtu kujivunia akili yake katika MUNGU.

Pasipo mashaka tukutane wakati ujao…………………!!!

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson……………………………………………….0764 018535

Ijumaa, 1 Mei 2015

MAUSIANO SALAMA-4



MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI;



 Tukiwatunaendelea na hatua inayofuata katika kuleta mwanga katika fahamu zetu na hatima kuwa na maamuzi yaliyosahihi ilikuleta mafanikio katika swala zima la mausiano na leo tuko katika sehemu ya nne, na yote haya ni katika kuhakikisha na fanyika baraka kwako na kwa jamii yetu kwa ujumla.

II.UTAYARI WA UCHUMI

Hii hali ya utoshelevu wa kiuchumi imekuwa janga katika jamii husika, kwani watu wanafikiri uwezo wa kijimudu katika uchumi imekuwa moja ya sababu katika mtu kuingia katika mausiano ni kweli kabisa katika mausiano hasa ya kimapenzi swala zima la uchumi muhimu sana!

Lakini katika jamii yetu wametumia fedha au uwezo walionao katika kujionyesha umaridadi wao na kuweza kutumia fedha kwa namna wanavyofikiri pasipo kujua hayo ni matumizi sahihi au sio sahihi,wako waliowengi wametumia fedha katika kubadilisha wanawake wakiamini kuwa baada ya kuwa na fedha hivyo msichana yeyote unaweza kumpata haijarishi yuko katika maadili au sivyo bali ana amini katika nguvu ya fedha anaweza kubadilisha mazingira yeyote pasipo kujali chochote au hata athari baada ya kitendo hicho………na mbaya zaidi hivi sasa hata wanawake wamekuwa wakitumia fedha zao katika kubadilisha wanaume kadili ya jinsi mtu anavyoamua kulingana na fedha zake au uwezo wake ili kutimiza matakwa ya nafsi yake.

Najua kuwa hakuna kitu kigumu kama mtu kuishi tofauti na hadhi aliyokuwa nayo kwa sababu kila hadhi katika dunia ya sasa kila hadhi ina namna ya kuishi japo wako watu wanaishi vile wanavyoona kunamwelekeo mzuri wa maisha na wako watu wanaishi katika ulimbukeni na kutumia uwezo wao vibaya tofauti na hali ilivyo au vile inavyotakiwa!

Nipende kusema tu kwamba uchumi na mausiano HAKUNA  muungamaniko wa moja kwa moja au kutoa fursa wa wewe kuingia katika mausiano kwa sababu unauchumi wa kutosha japo sichochei kwa mtu yeyote kuingia katika mausiano ukiwa hauko na mipango thabiti ya uchumi uliyonayo…….kwakua kuna kuwa na uchumi na matumizi ya uchumi!!!.

Niseme kuwa na uchumi ni haki yako kwakua unahuhitaji katika kuendesha maisha yako ya kila siku lakini katika upande wa mausiano unahitaji kutambua kwa msaada wa Mungu na uelewa wako katika kubaini lilojema na lenye mwisho uliojaa matumaini.

Niombe ujue kwamba mausiano sio maisha japo ni muhimu ila wako watu wanaishi katika maisha yao kila siku pasipo kuwa na mausiano hayo ya mapenzi wako wametoka katika mausiano ya kimapenzi kutokana na maumivu waliyo yapata au mateso na ukatiri waliofanyiwa katika maisha yao……hivyo hawawezi kusahau na hivyo wameamua kuishi maisha yao wenyewe kama wanavyoona kuwa watapata matumaini na amani katika mioyo yao.

Kuwa na uchumi mzuri ni kitu kimoja na kuingia katika mausiano ya kimapenzi kunahitaji wakati wake haupaswi KUCHANGANYA!

Wakati ujao……………………!!!

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson…………………………………………….0764 018535