Ijumaa, 1 Mei 2015

MAUSIANO SALAMA-4



MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI;



 Tukiwatunaendelea na hatua inayofuata katika kuleta mwanga katika fahamu zetu na hatima kuwa na maamuzi yaliyosahihi ilikuleta mafanikio katika swala zima la mausiano na leo tuko katika sehemu ya nne, na yote haya ni katika kuhakikisha na fanyika baraka kwako na kwa jamii yetu kwa ujumla.

II.UTAYARI WA UCHUMI

Hii hali ya utoshelevu wa kiuchumi imekuwa janga katika jamii husika, kwani watu wanafikiri uwezo wa kijimudu katika uchumi imekuwa moja ya sababu katika mtu kuingia katika mausiano ni kweli kabisa katika mausiano hasa ya kimapenzi swala zima la uchumi muhimu sana!

Lakini katika jamii yetu wametumia fedha au uwezo walionao katika kujionyesha umaridadi wao na kuweza kutumia fedha kwa namna wanavyofikiri pasipo kujua hayo ni matumizi sahihi au sio sahihi,wako waliowengi wametumia fedha katika kubadilisha wanawake wakiamini kuwa baada ya kuwa na fedha hivyo msichana yeyote unaweza kumpata haijarishi yuko katika maadili au sivyo bali ana amini katika nguvu ya fedha anaweza kubadilisha mazingira yeyote pasipo kujali chochote au hata athari baada ya kitendo hicho………na mbaya zaidi hivi sasa hata wanawake wamekuwa wakitumia fedha zao katika kubadilisha wanaume kadili ya jinsi mtu anavyoamua kulingana na fedha zake au uwezo wake ili kutimiza matakwa ya nafsi yake.

Najua kuwa hakuna kitu kigumu kama mtu kuishi tofauti na hadhi aliyokuwa nayo kwa sababu kila hadhi katika dunia ya sasa kila hadhi ina namna ya kuishi japo wako watu wanaishi vile wanavyoona kunamwelekeo mzuri wa maisha na wako watu wanaishi katika ulimbukeni na kutumia uwezo wao vibaya tofauti na hali ilivyo au vile inavyotakiwa!

Nipende kusema tu kwamba uchumi na mausiano HAKUNA  muungamaniko wa moja kwa moja au kutoa fursa wa wewe kuingia katika mausiano kwa sababu unauchumi wa kutosha japo sichochei kwa mtu yeyote kuingia katika mausiano ukiwa hauko na mipango thabiti ya uchumi uliyonayo…….kwakua kuna kuwa na uchumi na matumizi ya uchumi!!!.

Niseme kuwa na uchumi ni haki yako kwakua unahuhitaji katika kuendesha maisha yako ya kila siku lakini katika upande wa mausiano unahitaji kutambua kwa msaada wa Mungu na uelewa wako katika kubaini lilojema na lenye mwisho uliojaa matumaini.

Niombe ujue kwamba mausiano sio maisha japo ni muhimu ila wako watu wanaishi katika maisha yao kila siku pasipo kuwa na mausiano hayo ya mapenzi wako wametoka katika mausiano ya kimapenzi kutokana na maumivu waliyo yapata au mateso na ukatiri waliofanyiwa katika maisha yao……hivyo hawawezi kusahau na hivyo wameamua kuishi maisha yao wenyewe kama wanavyoona kuwa watapata matumaini na amani katika mioyo yao.

Kuwa na uchumi mzuri ni kitu kimoja na kuingia katika mausiano ya kimapenzi kunahitaji wakati wake haupaswi KUCHANGANYA!

Wakati ujao……………………!!!

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson…………………………………………….0764 018535



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni