UBORA
WA WOKOVU
Kufanya wokovu kuwa
kitu cha kutamanika au kuvutio na chenye maana kuliko chochote hilo ni jukumu
lako……..na unaweza kudaiwa endapo tu! utafanya wokovu ukaonekana hauna thamani
katika maisha ya mwanadamu, kwa maana ya wokovu wenyewe umepita viwango vyote vya
ubora wa dunia na hata wa mbingu.
Mungu ameshamleta
mwanae wa pekee ambaye ni yesu kristo
kwa ajili ya ulimwengu kama zawadi yenye thamani kubwa kuliko chochote na ili
kuwapatia wanadamu nguvu na kuimarika katika yeye.
Ukweli sio kitu chepesi
kuonyesha wokovu kuwa ni kitu bora katika mahali ulipo unaposoma,unapofanya
kazi na hata unapoishi na majirani zako kwa kuwa watu utaka kuona utofauti uliopo
kati yako na mwingine au na yeye……mathalani unaweza kuwa umeajiriwa na bosi
ambaye ajui wokovu maana yake nini? Anaweza kukujia na kutaka kuona maana ya
wokovu kupitia wewe japo! Anakulipa mshahara kwa maana nyingine anachangia
jeuri yako au furaha yako.
Ki ukweli wako watu
wanaishi maisha katika wokovu kiasi kwamba marafiki zake au ndugu zake na hata
mahali anapofanyia kazi wasione maana ya yeye kwenda kanisani au kujiita au
kujitambulisha ameokoka kwakuwa hawaoni tofauti kati yao na yeye na hivyo kuwa ni changamoto kwake katika kuwafanya jamii inayo
mzunguka katika bidii katika kujua zaidi fahari yake katika imani au mwenendo wake!
Wako watu ambao
wamekuwa wakijitenga na watu wasio mwamini Mungu katika imani yao kama wazazi wake, familia yake kwa ujumla na
hata wafanyakazi wenzake na kuona hao watu hawapaswi kuchangamana nae…na akiona
kuwa huo ndio ufahari wake wakujitenga
na wasio amini!
Wamekuwa wakiishi maisha hayo na kuona huo ndio wokovu.
Ukweli kwamba wokovu
umepewa wewe ili kwanza uwefaida kwako na ukawe faida kwa wengine na hivyo basi
kama usipo ona wakovu kuwa wa faida kwako ni wazi hakuna mtu ataona kuwa wokovu
ni kitu bora sana kwakua wewe umeanza kuona kuwa sio kitu bora.
Sio furaha ya Mungu
kuona wokovu unakuwa kuwa sio kitu bora kwa maana kwake yeye ni kitu bora sana
kuliko chochote hivyo anaamini kuwa kitakuwa cha maana sana kwako na katika
jamii wanayokuzunguka kwakua katika yeye hakuna kinachoshindikana……japo
havifanyiki kwakua umesha mpokea bali namna unamfanya aweze kuwa msaada kwako
na kwa wengine.
Lazima ujue kuwa pindi
waokovu unapokosa nguvu katika jamii inayokuzunguka tambua kuwa hiyo ndio
huzuni ya Mungu kuliko chochote kile ambacho unaweza kuwaza au kufikiria katika
njia yeyote.
Ni vizuri ujue kwamba
furaha ya Mungu ni kuona wewe unafurahi na hivyo hata furahi kuona wewe binafsi
unaona wokovu kama janga au mateso katika maisha yako na ikiwa yeye ameachilia
ni kitu chenye ushindi zidi na chenye thamani kubwa kuliko kitu chochote
ulimwengu wa sasa na hata wa baadae!
Unaweza kuufanya kuwa
wokovu kuwa ni kitu bora sana na wengi waka mfuata Mungu kupitia wewe binafsi
kwa namna unavyoenda mbele za Mungu kwa ukamilifu kuliko chochote.
Kuna vitu viwili nataka
ni viweke wazi japo kuwa sitavielezea kinagaubaga;
i.baba wa kiroho
huyu ni mtu muhimu sana hakikisha unamsikiliza na
kuona kupitia yeye upo vile ulivyo na utakuwa zaidi kwakua katika yeye unamuona
Mungu.
Hakikisha unamshirikisha katika jambo jema na hata
baya na kuona kile atakachofanya au kukisema katika yote muone kuwa ni baba
bora na wa maana sana katika maisha yako.
Popote unapoenda hakikisha moyo wako uko vizuri na yeye
japo wakati mwingine yeye kama mwanadamu anaweza akafanya yale yasio upendeza
moyo wako lakini katika hali yoyote jua ni baba mpaka pale Mungu atakapo amua
jambo jingine katika maisha yako
Ii. Roho mtakatifu
Huyu ni zaidi ya baba wa kiroho na mtu mwingine
yeyote kwani nafasi yake hakuna mtu atakaye weza kufanya, Mungu amempa heshima
kubwa sana….dhambi zote unaweza
kusamehewa lakini sio dhambi ya kumkufuru Roho mtakatifu!! Hapa kuna nini
ni jambo la kushangaza sana.
►Lakini katika yote msikilize ili
akupe dira yako hatua zako furaha yako na maisha yako kwa ujumla wake, na
ukimuelewa na kumkubali kamwa hauwezi kuchoka, kupotea na hata kuto timiza
ndoto yako.
MWAMINI YEYE UTAKUWA SALAMA!!!
Imeandaliwa
na;
Cothey
Nelson………………………………………………. 0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni