MAMBO
YA KUZINGATIA KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI;
Tukiwa bado tunaendelea
na mfululizo wetu wa MAUSIANO katika ujumla wake, na leo pia tunaendelea katika
sehemu ya tano……………hivyo karibu sana rafiki katika kuendelea kupata mwanga
katika kuzidi kusonga mbele!
III.UTAYARI
WA AKILI
Hapa ni uwanja hatari
sana kwakua katika hali ya akili kupevuka na kutaka kujua kila kitu kwa zaidi
sana….na siku zote akili uweza kushawishika na mwili na hata katika
kuona,kusikia na hatimae ikazalisha kiu ya kutaka kufahamu kitu zaidi ambacho
kinaendelea katika jamii husika japo yako mambo mengi yanaendelea katika jamii
husika lakini yako mambo ambayo yanashawishi zaidi na kuwa kivutio katika macho
na kinachobeba hisia.
Hivi sasa katika jamii
husika kuna mambo ambayo ni kivutio kwa watu wazima kwa maana watu wenye rika
kubwa zaidi na vijana kama watu wenye rika la wastani na kundi la watoto, na
ndani ya jamii yetu katika ulimwengu wa sasa mambo mengi yasiyo ya maana sana
yamekuwa yakitawala katika akili ya watu wengi hasa walio na rika 14 mpaka 35
ambao ndio tegemeo katika jamii husika katika kuleta chachu ya maendeleo katika
jamii husika.
Watu wengi wamekuwa
wakiichosha akili zao katika kutumia mambo ambayio yanaridhisha miili yao na
sio jambo lililo na manufaa sana katika maisha yake mathalani kuangalia picha
za ngono na kuanagalia staili za kufanya mapenzi na kuziweka katika maisha yao
kwa hakika akili zao zimetiwa giza na kuona giza zaidi ya kuona nuru ambayo
italeta matumaini katika maisha husika.
Matumizi hayo ni shida
kubwa katika maisha yake pamoja na jamii inayomzunguka hawajui kuwa “MISUSE OF MIND” ni shida kubwa kuliko jambo lolote lile ambalo
wanaoliona wenyewe wanaona kuwa ni kwenda sawa na dunia inavyoenda na sio
kuangalia mwisho wa safari ya dunia, ukweli hakuna kitu cha maana na chenye
thamani kubwa zaidi ya akili lakini namna unavyotumia akili yako ni ishara
kubwa kuwa unajipenda au haujipendi kila kitu unachokiangalia kizuri ujue ni
matumizi sahihi ya akili lakini sasa tumekuwa tuko tayari kupokea kila kitu tunacholetewa
hivyo hatujui kuwa kinamanufaa kwetu au la! Bali kwakua kimetengenezwa na mtu
mwenye ngozi nyeupe kila kitu anachokifanya basi sawa.
Akili inapokuwa na
upofu uwezi kujua maana ya msemo huu LINALOWEZEKANA LEO LISINGOJE KESHO msemo huu una maana yake lakini akili yako
inavyotiwa giza uwezi kuona maana ya matumizi sahihi ya akili ambayo italeta
maana kubwa sana katika maisha yako
Ukweli akili ya mtu
ndio dereva wa maisha ya mtu husika akili ikishachafuka tu hakuna la maana
linaloweza kuonekana katika maisha ya mtu husika, hivyo unahitaji kuwa makini
sana kuliko sehemu yoyote……unahitaji kuona fahari ya akili yako katika matumizi
yaliyo sahihi kuliko chochote kwa maana hakuna fahari ambayo itaipita fahari ya
akili uliyonayo kwa maana ni jambo la maana sana kwa mtu kujivunia akili yake
katika MUNGU.
Pasipo
mashaka tukutane wakati ujao…………………!!!
Imeandaliwa
na;
Cothey
Nelson……………………………………………….0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni