UKIIPOTEZEA KWELI UTUMWA UTAKUTESA
Kama binadamu unayeishi
katika sayari ya tatu (dunia) yenye mchanganyika wa mambo mengi……..kwa hakika bila
shaka utakuwa umewai kusikia MTU akisema maneno haya…. kama ningelijua
nisingelikuwa rafiki yake! Ningelijua mapema nisingelikuwa mchumba wake au
ningelijua nisingelikubali au ningelijua nisingelikataa au ningelijua nisinge
liangalia au ningelijua nisingelitazama au nisengelinyamaza kimya……….bila shaka
maswali haya uibuka baada matokeo fualni kutokea katika maisha yako.
Unaweza usione umuhimu wa kujua noti bandia au
feki kwakua bado ujakutwa na mkasa wa kupata noti feki na kisha ikakuweka
katika mazingira mgumu sana, hivyo usione haja kwanini nijue noti bandia na
feki, na wako watu wanaweza wasione umaana wa kusoma kwakua hawajajua pindi asiposoma
nini atapungukiwa au hasara gani au changamoto gani zitamkabili, mbali nao kuna
aina ya watu kutokana na nafasi walizonazo mathalani cheo, fedha, na mengine
mengi hivyo uweza kujisahau hivyo
kutumia muda wao hawawezi kuona umuhimu wake lakini pindi atakapo pita mahali
ambapo ataona yuko tofauti wa vile
alivyofikiria na hali halisindipo atakapoona thamani ya kule alikotoka.
Na ni kawaida wanafunzi
wengi wanaweza kukosa swali moja kwa sababu ya kukosa uelewa au kukariri pasipo kuelewa
unakuta mtu amekariri tu na pindi anapoingia kwenye mtihani na kukuta swali
linafanana na lile analolijua basi ufurahia na kufanya harakaharaka sana pasipo
kuwa makini labda kunamitego ambao mwalimu ameuweka na kujikuta kuwa na
matumaini ambayo hayapo na mwisho kujikuta anakosa lakini mwelewa sikuzote huwa
hana harakaharaka kwani anaamini anajua
hivyo hakuna mitego itakayo msumbua kwakua afanyi sawa na alivyo kariri bali
ufanya sawa na alivyoelewa hivyo kupata kunakuwa ni haki yake.
Mambo mengi yanatokea
katika maisha mtu yanaweza kuwa mabaya na mwisho wake ukaathiri maisha ni
kutokana watu kutojua ukweli halisi kuhusu hicho kitu au huyo mtu!
Niseme vijana wengi
wanapata mimba(wasichana au mwanamke) ni kwasababu ya kukosa uelewa wa kweli
kuhusu jambo hilo inawezekana kutokana kutojua kinaga ubaga akajikuta
akadumbukia katika hali hiyo kwani kunakipindi unaweza sema siku moja hauwezi
kupata mimba inawezekana alikuwa anajua lakini pindi alipoingia katika uwanja
wa jambo hilo(field) katika mgongano wa hisia akajikuta akisema kuwa kweli nilisema
siku moja siwezi kushika mimba lakini hali hiyo inaweza kutokea tofauti na alivyojipa
akili na uhalisia ukajitokeza (kushika mimba).
Na wakati mwingine
ukweli kwa tendo la siku moja unaweza usipate mimba lakini huo ukawa mwanzo wa
mtindo huo kuendelea siku kwa siku katika akili na uku ukisema tuwe makini
katika jambo hili au tutumie kinga ili tutunze hekalu la Mungu kwa kuwa
unapokuwa katika mfumo huo unaweza kujipa moyo na kujilinda na hata kujiliwaza
katika kila jambo unalolifanya pasipo kujua hapo unaelekea gizani haijarishi
utaki au unataka lakini yote yatabaki kama yalivyo.
Niseme kuwa mateso
mengi watu wanayopitia ni kwasababu waliitupilia mbali kweli na kujitia giza
katika akili zao na mwisho mateso yakawa ndio maisha yao pasipo kujali kuwa walikuwa
watu wema kiasi gani au walikuwa chagua la Mungu.
Waefeso
4:18 ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa
sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao;
Na ni kweli kila
binadamu utamani uhuru sana katika maisha yake kwani katika uhuru kuna
kujiamini, kunakujisimamia, kunakujiheshimu na zaidi kunakujipenda lakini nisipende kukunganya uhuru utokana na
kweli unayoiishi kutokano na kuijua uwezi kuwa uhuru zaidi na ulimwengu wako
unao unaoujua
Yesu alisema “mataifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru”
nje ya hapo sina neno zaidi kusema kweli uliyo nayo ndio uhuru ulio nao, kwani
utofauti wa wewe na mwingine katika kufanya jambo moja utegemea sana uelewa
wenu na ndipo apo nazungumzia kweli.
Yohana
8:32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
Na ndoma usemekana
kwamba ukitaka kumsaidia mtu fungua ufahamu wake uwe na nuru na ndipo atambue yuko
wapi na anakwenda wapi? Na ndipo mwendo wake uanze kwenda kwa uhakika pasipo
kupapasa.
Katika maamuzi yoyote
utakayo yachukua kubwa sana kwako ni kutambua usahihi wa jambo hilo sio lile la
kuambiwa kwa upande mmoja bali kila kitu kipe muda wa kutosha katika kuwa imara
ili uweze kuimiri vishindo vyake.
Imeandaliwa
na;
Cothey Nelson……………………………………………..0764 018535
UHURU
HAUTAFUTWI BALI UNAKUJA BAADA YA KUIJUA KWELI