Jumanne, 19 Januari 2016

UKIIPOTEZEA KWELI UTUMWA UTAKUTESA!



UKIIPOTEZEA KWELI UTUMWA UTAKUTESA

 Kama binadamu unayeishi katika sayari ya tatu (dunia) yenye mchanganyika wa mambo mengi……..kwa hakika bila shaka utakuwa umewai kusikia MTU akisema maneno haya…. kama ningelijua nisingelikuwa rafiki yake! Ningelijua mapema nisingelikuwa mchumba wake au ningelijua nisingelikubali au ningelijua nisingelikataa au ningelijua nisinge liangalia au ningelijua nisingelitazama au nisengelinyamaza kimya……….bila shaka maswali haya uibuka baada matokeo fualni kutokea katika maisha yako.

 Unaweza usione umuhimu wa kujua noti bandia au feki kwakua bado ujakutwa na mkasa wa kupata noti feki na kisha ikakuweka katika mazingira mgumu sana, hivyo usione haja kwanini nijue noti bandia na feki, na wako watu wanaweza wasione umaana wa kusoma kwakua hawajajua pindi asiposoma nini atapungukiwa au hasara gani au changamoto gani zitamkabili, mbali nao kuna aina ya watu kutokana na nafasi walizonazo mathalani cheo, fedha, na mengine mengi hivyo uweza kujisahau  hivyo kutumia muda wao hawawezi kuona umuhimu wake lakini pindi atakapo pita mahali ambapo ataona yuko tofauti  wa vile alivyofikiria na hali halisindipo atakapoona thamani ya kule alikotoka.

Na ni kawaida wanafunzi wengi wanaweza kukosa swali moja kwa sababu ya  kukosa uelewa au kukariri pasipo kuelewa unakuta mtu amekariri tu na pindi anapoingia kwenye mtihani na kukuta swali linafanana na lile analolijua basi ufurahia na kufanya harakaharaka sana pasipo kuwa makini labda kunamitego ambao mwalimu ameuweka na kujikuta kuwa na matumaini ambayo hayapo na mwisho kujikuta anakosa lakini mwelewa sikuzote huwa hana harakaharaka  kwani anaamini anajua hivyo hakuna mitego itakayo msumbua kwakua afanyi sawa na alivyo kariri bali ufanya sawa na alivyoelewa hivyo kupata kunakuwa ni haki yake.

Mambo mengi yanatokea katika maisha mtu yanaweza kuwa mabaya na mwisho wake ukaathiri maisha ni kutokana watu kutojua ukweli halisi kuhusu hicho kitu au huyo mtu!

Niseme vijana wengi wanapata mimba(wasichana au mwanamke) ni kwasababu ya kukosa uelewa wa kweli kuhusu jambo hilo inawezekana kutokana kutojua kinaga ubaga akajikuta akadumbukia katika hali hiyo kwani kunakipindi unaweza sema siku moja hauwezi kupata mimba inawezekana alikuwa anajua lakini pindi alipoingia katika uwanja wa jambo hilo(field) katika mgongano wa hisia akajikuta akisema kuwa kweli nilisema siku moja siwezi kushika mimba lakini hali hiyo inaweza kutokea tofauti na alivyojipa akili na uhalisia ukajitokeza (kushika mimba).

Na wakati mwingine ukweli kwa tendo la siku moja unaweza usipate mimba lakini huo ukawa mwanzo wa mtindo huo kuendelea siku kwa siku katika akili na uku ukisema tuwe makini katika jambo hili au tutumie kinga ili tutunze hekalu la Mungu kwa kuwa unapokuwa katika mfumo huo unaweza kujipa moyo na kujilinda na hata kujiliwaza katika kila jambo unalolifanya pasipo kujua hapo unaelekea gizani haijarishi utaki au unataka lakini yote yatabaki kama yalivyo.

Niseme kuwa mateso mengi watu wanayopitia ni kwasababu waliitupilia mbali kweli na kujitia giza katika akili zao na mwisho mateso yakawa ndio maisha yao pasipo kujali kuwa walikuwa watu wema kiasi gani au walikuwa chagua la Mungu.

Waefeso 4:18 ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao;
Na ni kweli kila binadamu utamani uhuru sana katika maisha yake kwani katika uhuru kuna kujiamini, kunakujisimamia, kunakujiheshimu na zaidi kunakujipenda  lakini nisipende kukunganya uhuru utokana na kweli unayoiishi kutokano na kuijua uwezi kuwa uhuru zaidi na ulimwengu wako unao unaoujua

Yesu alisema “mataifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru” nje ya hapo sina neno zaidi kusema kweli uliyo nayo ndio uhuru ulio nao, kwani utofauti wa wewe na mwingine katika kufanya jambo moja utegemea sana uelewa wenu na ndipo apo nazungumzia kweli.

Yohana 8:32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
Na ndoma usemekana kwamba ukitaka kumsaidia mtu fungua ufahamu wake uwe na nuru na ndipo atambue yuko wapi na anakwenda wapi? Na ndipo mwendo wake uanze kwenda kwa uhakika pasipo kupapasa.

Katika maamuzi yoyote utakayo yachukua kubwa sana kwako ni kutambua usahihi wa jambo hilo sio lile la kuambiwa kwa upande mmoja bali kila kitu kipe muda wa kutosha katika kuwa imara ili uweze kuimiri vishindo vyake.

Imeandaliwa na;

Cothey  Nelson……………………………………………..0764 018535

UHURU HAUTAFUTWI BALI UNAKUJA BAADA YA KUIJUA KWELI

Jumanne, 12 Januari 2016

UTUMWA WA HIARI



UTUMWA WA HIARI



Katika hali ambayo watu wengi hawapendi kuishi wala kusikia ni hali hii inaitwa UTUMWA kwani ndani ya hali hii inaambata na mateso ya nafsi na wakati mwingi ina ambatana na mateso ya mwili, kiukweli unapozungumzia utumwa lazima uendane sambamba kufanya jambo nje ya hiari binafsi (matakwa binafsi) lakini katika dunia ya sasa  kuna utumwa wa kupenda au utumwa wa hiari binafsi na wakati mwingine utumwa uendana sana na majonzi hasa katika moyo.

Hili neno UTUMWA alina rafiki katika dunia, na kama ukiamua kuanzisha maandamano ya kuondokana na utumwa wa nafsi basi bila shaka utapata wafuasi wengi na hasa tabaka la chini.
Kwa jinsi watu wanavyolichukia hili neno watu wangekuwa na uwezo wa kuliondoa neno hili katika kamusi basi wangeliondoa maana neno linachefua moyo! Kwakua alipendezi kutamkwa wala maana yake bali linaonekana kama JANGA.

Adui mkuwa wa utumwa ni uhuru, kwani palipo na uhuru basi hapo hakuna utumwa na palipo na utumwa basi hapo hakuna uhuru hawa ni maadui ambao hawawezi kukaa sehemu moja na kuamua jambo hilo kwa kushirikiana kama timu.

Kuna mambo mengine mtu anaweza akaona ni ya kawaida kwakuwa watu wengi wanafanya na kwa mtazamo wa kawaida unaweza kuona kama yanafaida katika maisha ya watu wanavyoishi kutokana na hali ya kuzoelea kwa watu wafanyao mambo hayo au kutokana na tafsiri inayotolewa na macho yako.

Utumwa wa hiari ni hali ya mtu kujikuta kufanya jambo yeye binafsi kutokana kushindwa kufanya tofauti na hali iliyopo na akili yake ikiona kuwa hakuna njia ila inabidi nikubaliane na hali hii kwa maana wakati mwingine unaweza kujikuta katika hali mbaya zaidi kwa kushindwa kufanya jambo unalopaswa kufanya.

Huu ni utumwa ambao unajikuta wewe binafsi unatengeneza nafasi katika kukamilisha swala au jambo unalolifanya kila siku au kila wakati, na huu ni utekwa katika upande wa akili na mwili unakuta unafanya kwakujua lakini hauna njia mbadala nyingine ya kufanya tofauti na vile unavyopaswa kufanya. Wakati mwingine utumwa huu unaweza kufanya hata bila ya kusimamiwa na mtu na wakati mwingine unaweza kufanya kwa shinikizo au kusimamiwa na mtu ila katika hali ya kupenda.

Huu ni utumwa ambao wewe binafsi ndio unajua kwanini nafanya hivi na sio mtu aliye karibu yako au mwenye nafasi yeyote katika maisha yako, kwakua kile unachokiamini wewe na namna unavyopenda uwezi kuamini kama kuna mtu mwingine anaweza kukuelewa kama unavyoelewa/unavyoamini.

Huu ni utumwa ambao hauwezi kuchoka katika kuenenda katika mtindo maisha ambao umeuchagua pasipo kukata tamaa bali ni katika kuridhisha akili yako na mwili wako, wakati mwingine unawezajua kuwa kitu hiki au jambo hili mwisho linaweza kuniweka katika hali ngumu lakini bado utakuwa ukiendelea kufanya hivyo maana katika kufanya hivyo ndio uleta burudiko la nafsi yako.

Kwakua huu ni utumwa unaohusisha hiari yako hivyo inakuwa sio kitu rahisi tu kwa wewe kuwaza tofauti na hasa katika hali unayostahili kuwa nayo, wakati mwingi unakuwa katika giza japo unajikuta una hali ya kupenda pasipo kujua hasa maana yake nini na kujua faida yake au matokeo yake katika jambo ambalo unalolitaka kulifanya.

Na ukumbuke kuwa utumwa wa hiari unazaliwa pale tu akili inapokosa kutawala jambo Fulani katika mwenendo mzima wa maisha yako, jambo hilo linaweza kuwa la siri au wazi lakini linakuwa lina nguvu hata kushindwa kuzuiwa na akili au mwili wako, utumwa huu unakupa nguvu hasa unapotambua hakuna mtu anayekuona hivyo unakuwa huru kutumia uhuru wako.

Hakuna nguvu ya kweli inayoweza kuzaliwa hapa ikiwa tu tayari utumwa wa hiari utakuwa ukisababisha giza kuzidi kuchukua nafasi katika maisha yako, na mwisho utakapojitokeza unaweza ukaweka wazi yale yote yaliyo uteka mwili wako na akili yako.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………………………0764 018535

UTUMWA NI TESO LA NAFSI

Jumanne, 5 Januari 2016

UTUKUFU WA MUNGU: ACHA NIUTE USIKU KUWA GIZA

UTUKUFU WA MUNGU: ACHA NIUTE USIKU KUWA GIZA: ACHA NIUITE USIKU KUWA GIZA  Ni jambo la kawaida tu pindi inapokuwa usiku basi watu hupenda kusema habari za usiku au usiku mwe...

ACHA NIUTE USIKU KUWA GIZA



ACHA NIUITE USIKU KUWA GIZA


 Ni jambo la kawaida tu pindi inapokuwa usiku basi watu hupenda kusema habari za usiku au usiku mwema…… wakiwa wanaenda sawa na majira yaliyopo, hali kadhalika pindi inapokuwa mchana watu usema mchana mwema au habari za mchana, imekuwa ni kitu kimoja kizuri sana katika utamaduni wa kusalimiana hasa waafrika,japo salamu ya mchana imekuwa ikitumika sana kuliko ya usiku kutokana na wingi wa watu unaokutana mchana kuliko usiku!

Ni vizuri kuita usiku kuwa ni usiku ili uweze kuishi kulingana na hali iliyopo hasa mwanga unakuwa hafifu hivyo unahitaji kuwa makini katika mwenendo wako katika usiku huo na pia katika mchana lazima ukubali kuwa huu ni mchana yanipasa nitembee katika hali stahiki nikijua kuwa huu ni mchana kila mtu nirahisi kuniona kwahiyo lazima nitembee katika hali iliyo sawa kulinganisha na wakati.

Na ndomana watu wengi katika ulimwengu wa sasa hasa huu wa utandawazi wamekuwa wakitembea na kuvaa mavazi yanayo ashiria huu ni usiku na mchana (tunahita maendeleo) na pindi ukavaa mavazi ya usiku wakati wa mchana bila shaka unaweza kuibua maswali kwa jamii inayokuzunguka, kwakua jamii inategemea kila vazi linawakati wake na jamii ya sasa imekwenda mbali kidogo kusema pia kila hali ya hewa inamavazi yake mathalani majira ya joto, masika,baridi n.k kila hali inapotokea ina aina ya mavazi yake stahiki ambayo kama binadamu anapaswa kuvaa pasipo kuchanganya!

Na unaweza kushangaza watu pindi utakapoanza kuita usiku kuwa ni mchana hata kama kunataa zenye uwezo mkubwa ambao mwanga wake unafanana kuwa kama mchana lakini ukweli utabaki kuwa huu ni usiku ila taa zilizopo zina mwanga mkali sana.

Acha niuite usiku kuwa giza nini maana yake!
Nipende kusema kuwa usipokubali hali uliyonayo ni ngumu tu kuvuka sehemu nyingine iliyo hatua bora katika maisha yako!

Wako watu walikuwa wanaumwa sana na wakati mwingine magonjwa ya aibu mtu anaona hawezi hata kumwambia rafiki yake anabaki kutumia madawa katika duka la dawa kununua dawa za kutuliza maumivu hawezi kwenda hospitali wala kutafuta suluhuu ya tatizo linalo mkabili kwa kuogopa kuwa ataweza kuchekwa au heshima yake itapungua katika familia au katika jamii inayomzunguka.

Wako wanawake na wanaume wanajua kuwa hawana uwezo wa kuzaa kabisa kutokana na ushahidi wa kimadaktari lakini pindi wanapokuwa wamepata wenzi wao wanakuwa sio wa wazi katika kueleza hali zao za kiafya na matokeo yake wamekuwa wakileta shida katika jamii zao na hata kupelekea ndoa zao kuwa na wakati mgumu sana tofauti na hali sahihi inayotakiwa kuwepo katika ndoa.

Wako na wanafunzi wamekuwa na matokeo mabaya katika hali ya mwanzo kabisa katika masomo yao lakini wamekuwa sio wa kweli pindi wanapoulizwa na ndugu zao au walezi wao na kukuta kusema tofauti na hali ilivyo na mwisho hali ikawa mbaya sana na hata kupelekea kufeli katika masomo yake.

Wako watu wengine wamekuwa wakisema Mungu pekee yake anajua na ndiye ataye jibu na kunipa haja ya moyo wangu lakini wakati mwingi imekuwa ni vigumu tu kuwa Mungu kushuka kwako kwa namna unavyofikiri anaweza akamtumia mtu naye akawa jibu katika swali lako linalo kukabili.

Usipokubali na kutambua kasoro zako ipo siku itakuweka katika mazingira magumu sana na hata kukupelekea kujuta kwanini ukuwa wazi toka mapema na hatimae yakakufikisha mahali ulipo sasa ambapo kiukweli ukupatarajia.

Pindi unapokubali tatizo sio kwamba unataka likae na wewe milele bali njia sahihi katika kulitambua marefu yake na mapana yake ili iwe rahisi kutoka pale ulipo kwakua utajua chanzo chake  na utafanya akili yako ifanye kazi katika hali ya utulivu na kupata jibu sahihi na ikawa suluhu ya kudumu!

Na hali ya kukubali jambo kuwa limekukuta sio ishara ya kuonyesha Mungu ameshindwa kuliepusha lisikupate hapana kunawakati mwingine Mungu anataka wewe uwe ushuhuda kwa wengine waone jinsi ulivyoteseka na hatimae ukaibuka kuwa mshindi.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………..0764 018535