Jumanne, 30 Januari 2018

MAONGOZI YA ROHO MTAKATIFU






Moja ya tatizo kubwa linalowakabili watu wengi hata kupelekea kushindwa kuelewana, kuwa pamoja na hata kushikamana ni UBINAFSI. Uwa tatizo la ubinafsi linazidi kuwa tatizo pale mtu anaposhindwa kutambua kuwa  mwenendo wake kuwa ni tatizo. ( hali ya mtu kuwa na tatizo na kushindwa kujua kuwa hilo ni tatizo na kuona ni maisha ya kawaida ili mradi nafsi yake ina jisikia raha ni hatari ).

Hautashindwa kukuta ugomvi/kutoelewana kwa watu wanaoishi katika nyumba moja kama kila mmoja akiangalia na kufanya vile anavyoona sawa machoni pake pasipo kuangalia mwenzangu ata athirika au atachukuliaje?

Yohana 6: 38  Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka

Wakati mwingine kukubali kujikana kwa ajili ya mwenzako ni ishara kubwa ya kuheshimu na kupenda ushirikiano pamoja na kutunza umoja thabiti ulio kati yenu.

Ni muhimu kila mtu aone jinsi gani mwenzangu atafaidika nae kuliko mtu mmoja angoje kupata mambo mazuri kutoka kwa mwenzake! ( mimi kwanza-ubinafsi).

Kama unataka kujivunia wokovu na kuona fahari basi kwanza hunabudi kujitathmini na kuona ni kweli utendaji wa Mungu ndani yako ndio una nguvu au utendaji wako ( ubinafsi ).

Moja ya raha ambayo Mungu anaiona kwako pindi anapokuona ni pale anapoona utawala wa Roho mtakatifu unaoshamiri ndani yako. Na hapo ndipo kauli ya kusema wokovu ni mgumu itaanza kukosa nguvu kwako, kwakuwa kama yeye alivyoweza kuushinda ulimwengu ndivyo atakavyo yashinda yote kupitia wewe.

Nikubaliane tu kuongozwa na Roho mtakatifu sio lelemama/kitu chepesi kwani kinahitaji uhuru wako upotee kwa kiasi kikubwa japo hakuna kitu kizuri kama hiki.

Kama hautakubali kupoteza uhuru wako basi sahau maongozi makamilifu ya Roho mtakatifu.
Na pindi utakapokosa kuwa tayari kwa ajili ya Mungu ( Roho mtakatifu ) sahau kupata raha ya Mungu iliyo kamilifu.

Kuruhusu utawala wa Roho mtakatifu kuchukua nafasi ndani yako hiyo ndio ishara kubwa ya KUMPENDA MUNGU.

Unapokubali kuongozwa na Roho mtakatifu maisha ya wokovu hayakuumizi kichwa kwakuwa yatakuwa yakiongozwa na kusukumwa na PENZI LAKE hivyo uzito na kutojisikia hakuta kuwa sehemu yako.

Ni muhimu unapoongozwa nawe ukubali kuongozwa kuliko kutoa njia zako hama kuona njia zako zinaweza kukusaidia.

Mithali 14: 12 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

Ni kweli unapokua ndani ya wokovu unakuwa hunatofauti na mtu mwingine kwa maana ya mahitaji ( chakula, mavazi na makazi ) lakini maongozi ya Roho mtakatifu ndio funga kazi itakupa kila kitu upasacho kukipata maana yeye ndiye anayejua ulikotoka na kule unako kwenda.

Uwa inakuwa haina maana sana kama ukiwa na marafiki wengi wazuri wenye uwezo na busara na hekima za kutosha kama hauna urafiki nae maana hao wote wanaweza fanya sawa na uelewa wao ulio na kikomo na hata kubashiri kesho yako namna itakavyokuwa lakini sio Roho mtakatifu yeye abahatishi anachokwambia ndicho kinakuwa!

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………. 0764 018535

Jumanne, 23 Januari 2018

ACHA YAWE YAO!





Katika ulimwengu tulionao, mambo mengi yanafanyika na yanaweza onekana mazuri au mabaya kutokana na mtazamo wa mtu husika lakini sio kila jambo lazima na wewe ufanye au uache atakama linaonekanaje! Au limesaidia wangapi? Kila tendo utegemea majira yake, namna yake pamoja na aina ya watu husika.

Kuna mvutano mkubwa na mwingiliano wa mfumo wa dunia na wa Mungu, kwa maana yale yanayo endelea kwa watu wasiookoka kwa kiasi kikubwa ndio yale yanayo watokea wale waliookoka! usiniulize kwa nini kwani hata mimi nashangaa!;

Mathalani,

Ø  MAHUSIANO YA KIMAPENZI

(a)   Kuangalia muonekano kama chanzo cha mvuto wa kimapenzi .
-          Sifa zote hana lakini muonekano wake tu unaweza kummaliza mtu kabisa.

(b)   Anajulikana sana nami nitajulikana
-          Ukitembea na waridi nawe utanukia! Inategemea waridi la wapi?

(c)    Nitadumu nae kama mfuko wake hauta pungua.
-          Imekuwa kama ulimbo kivutio kwako , anapokuwa vizuri basi hapo tabasamu ataliona tofauti na hapo itakuwa sawa na chozi la samaki majini( hataliona tabasamu lako ).

(d)   Niko nae lakini bado natafuta.
-          Na hisi kama bado sijafika ngoja nizuge naye kwanza lakini akitokea mwingine aliyekizi vigezo vyangu kumwaga ni jambo la kawaida tu/ lisilopingika au kuhitaji mjadala.

-          Sina uhakika kama tunaendana sana ngoja niangalie kwanza.

-          Jinsi tunavyoenenda tukifika mwezi mmoja sijui! Maana dalili zinaonyesha muda wowote lolote linaweza kutokea.

Mambo haya yote yamekuwa ni mfumo wa dunia ( mwenendo wa watu katika dunia) na yamekuwa na nguvu hata katika maisha ya watu waliookoka na kupelekea kupoteza radha na ushawishi wa wengine kuokoka.

utendaji wa watu wengi unafanana hakuna utofauti wa utendaji picha ya kristo katika maisha ya wengi inapotea,

Ni kweli ili mradi unaishi katika dunia mambo yanayoendelea duniani utaendelea kuyasikia na pengine hata kukuathiri katika mwenendo wako.

Katika mambo yote usipoteze asili yako!

I petro 1: 23 Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.

Kuyaona mambo au kuyasikia na hata kuyafahamu mambo hautakiwi kupoteza dira au mwelekeo wa maisha yako kama umeokoka kweli, jua tayari unao misingi mizuri katika maisha yako juu ya kila kitu kwa kuwa mwenye asili ya vyote yuko ndani yako.

Luka 1: 37 kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.

Ni muhimu ujue;
(a)   Katika mwingiliano wowote hatupo kustarehe tu au kuonyesha matambo bali tupo kulitekeleza/kulikamilisha kusudi la Mungu pamoja.

-          Raha na furaha inakuwepo tu kwakuwa mleta raha yuko ndani yenu haijarishi mna nini au hamna nini?

(b)   Jambo la msingi kwa Mungu kwa mwanae uwa ni kumstawisha kwa majira yake na hakuna msamiati “ Nimechelewa” kwa Mungu.

-          Unapokuwa wake yeye anaanza kushughulika na maisha yako.

Unapopita katika hali yoyote yeye anakuwa pamoja nawe.

Zaburi 23: 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………….. 0764 018535

Jumanne, 16 Januari 2018

ANZA NA MWANZO!






Sio vibaya kupenda kitu kinachoonekana vizuri maana chochote kinachoonekana vizuri basi kitavutia hama kushawishi kuangalia japo si lazima uwe nacho.

Mara nyingi kitu kilichofanyika pasipo kuhusika hama kuhusishwa, uhuru na kujiamini unakuwa mdogo sana maana ujui uimara wake utadumu kwa muda gani hama kujigharimu kwa hao watu waliofanikisha jambo hilo?

Kuanza mwanzo kunakuwa ni jambo la kupendwa na watu wengi lakini shida inakuja pale unapoona hakuna haja ya kuanza upya hama ushirikiano mdogo katika kukutia nguvu katika kuanza upya au unawaza ni kuchelewa tu katika kuanza upya!

Moja ya changamoto inayowafanya watu kuona ugumu katika kuanza upya ni namna ya utofauti uliopo/ utakaojitokeza kati yake na watu wengine walio tangulia hapo unyonge na uzito uweza kuchipuka ndani ya mtu na hapo ukashindwa kuanza upya kwa kuhofia nitaonekanaje?

Jambo lolote linalokutokea haijarishi upana wake au limepelekea uharibifu kwa kiasi gani? Jenga hali ya utayari wa kuanza upya ili ufanye kitu katika hali ya ubora.

Hauhitaji kuhisi umechukua au itachukua muda mrefu kiasi gani kurudi katika hali uliyokuwanayo awali ( usijipe uzito mwenyewe au usifanye mambo kuwa magumu ) ni muhimu ujue nafanya hivi ili kupelekea kesho yako yenye kishindo zaidi.

Haupaswi kuangalia sana watu bali jali sana hatma yako ( ubinafsi wa maana ) maana ni wewe utatengeneza ubora wa ustawi wako na kizazi chako na sio mwingine maana hakuna anayeweza kukutengenezea maisha yako kama wewe mwenyewe ukiyashindwa.

Akili yako iwe katika hali ya kufanya vizuri na sio kushindana na wala watanionaje? Uwa wanakuona kama unavyoonekana!

Hata watu waliotengeneza au kufanya mambo makubwa yaliyosaidia katika jamii na ulimwengu tulio nao mathalani umeme, taa, meli na hata ndege walijali sana kile wanacho kifanya kuliko wanachokisikia kutoka kwa watu.

Mwanzo 6: 22 Ndivyo alivyofanya Nuhu, sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu, hivyo ndivyo alivyofanya.

Na hapo ndipo utakapoona / kujua upekee wako na kuona kuwa haina haraka sana kufanya kitu maadam wengine wanafanya.

Kufanya kitu kitakacho kuonyesha wewe kwa uhalisia wako haijarishi kitachukua muda gani hiyo inakuwa ni ishara kubwa ya kujikubali na kujiamini kwa kuwa wewe nawe uliumbwa duniani kwa kusudi maalum nalo ndilo unalolitekeleza.

Unaweza kufanyika baraka katika mazingira uliopo kwa wewe kufanya jambo lenye manufaa katika jamii yako haijarisha hilo jambo au hicho kitu kili kugharimu kiasi gani hama kuchukua muda gani la msingi tu umetimiza ndoto yako.

Kubali kuanza mwanzo katika jambo husika maana hatima yako haiko katika muda bali iko katika mikono ya Mungu kama wewe ukizidi kuwa wa Mungu.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………… 0764 018535

Jumanne, 9 Januari 2018

NAREJEA!





Mahali / wakati ambapo unaweza kuona tabasamu la mgonjwa ni pale anapoona anaanza kurejea katika hali ya uzima wake aliokuwa nao awali na hii furaha uwa inaenda mbali hadi kwa wanao muuguza mgonjwa, kwani nao uwa na furaha na matumaini uweza kuzidi kuimarika.

Na uzuri katika dunia tuliyonayo hakuna jambo ulilolipoteza au uliloliona umelikosa lisiweze kurejea tena katika hali ya ubora zaidi na mvuto wa kipekee maadamu tu unaishi.

Hichi ni kipindi ambacho majeraha na machozi ya moyoni yanaanza kuwa adimu na furaha kuanza kuchipuka kwa namna nyingine.

Matendo 3:19 Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

Na ni vizuri kukubali kuanza upya hata kama iki kugharimu kitu gani kuliko kuendelea katika kukosea na maumivu.

Ni kama asubuhi yenye kuchipua tabasamu lililoadimika hama kupotea kwa muda mrefu itakapo chipua hadi nywele na ngozi uweza kuhisi furaha.

Hakika ni kipindi kinachopendwa na wengi japo mchakato wake usipokua mwangalifu unaweza usione kama kuna siku itafika ile raha uliyoipoteza muda mrefu itarejea tena!

Kila mtu anarejesha furaha yake kutokana na jambo husika na sio kila jambo tu linalomtokea mtu uweza kusababisha jibu katika maswali ya moyo wake:

(a)   Wako watu waliokosa watoto wakiwa katika ndoa zao kwa muda mrefu lakini pindi dalili za mtoto zilipoanza na hatimaye kupata mtoto basi hapo furaha na shangwe uweza kuwa dhahiri na mengine kubaki historia.

(b)   Pia wapo watu waliosota sana katika kusoma na kupitia changamoto nyingi kiasi cha kupoteza matumaini kama atakamilisha safari yao ya elimu inapotokea kufanikisha hazma yake ( kusudio la moyo wake ) basi hapo furaha isiyo ya kifani uzaliwa.

(c)    Inawezekana mtu alikosa kazi kwa muda mrefu mara tu baada ya kuhitimu masomo yake hama alishawai kupata kazi baadae akafukuzwa au kuacha mwenyewe baadae akapitia msoto mkubwa kiasi cha kupelekea kujuta maamuzi ya awali lakini mwishoe akapata nafasi iliyobora sana na hapo changamko la moyo uweza kuchipuka.

(d)   Sekta ya mahusiano (sekta pendwa ) inawezekana ulipitia katika misukosuko mingi ( uliyoitegemea na usiyoitegemea ) na hata kutembea na wapenzi wako ili wafurahie urembo wako ili waweze kutulia na wewe tu lakini mawazo yako haikuwa nia yao na baada kufaidi uzuri wako waka kuacha solemba ( hewani pasipo kujua/kujali utaangukia wapi ) pamoja na hayo bado ujana wako unaweza kuhuishwa kama tai na kusahau jana, na kuipenda sana leo na kujiandaa kwa ajili ya kesho.

UREJESHO WAKO UPO! NEVER GIVE UP.

INAITWA SIKU! BARIKIWA.

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………0764 018535